mwandishi mwandamizi wa daily news kilasa mtambalike anashindwa kuizuia furaha yake baada ya kumvisha pete mai waifu wake moulid ahmed wa habari leo walipofunga pingu za maisha wikiendi hii ukumbi wa makete, mbezi. magazeti ya daily news na habari leo yote ni ya serikali na makao yake makuu ni mtaa wa samora avenue jijini dar ambako maharusi wanafanyia kazi pamoja na mpigaji wa picha hizi mrokimroki a.k.a faza kidevu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. Weweeeee.. hina stailo hiyo walai nabada ushungu yakheee ah kaka michu asante kutuletea aina nyengine ya michiro, sisi wapenzi wa hina tunaijua hiyo stailo inaitwa makarachee, makarasia au magarashaa

    ahaa wamependeeeza unaweza kutofautisha kirahisi upi mkono wa baba na upi mkono wa mama teeeena.

    ila michu umetughini bwana ungutuibia na mguu tuone manakshi naksh yalivyokolea

    ReplyDelete
  2. I know well the couple. Kilasa and Maulid truly love each other. You deserved a knot. Sasa fanyeni chap kumtafuta dogo (a child)- Muhimu sana kwenye ndoa, otherwise maneno yatazungumzwa juu yenu kila pahala atiiii!!!

    ReplyDelete
  3. Hina hiyo mwanawane, Bibi harusi anameremetaaaaa! Amependeza kweli kweli Mashallah!

    Sasa yule aliyesema hina uchafu mtupu aje aone vitu hapa, alaa. Jambo usilolijua!!!!!

    Hongera bwana na bibi Kilasa kwa kuamua kufunga ndoa, maana siku hizi vijana wengi wanaogopa kufunga ndoa eti ni usasa. Hongereni sana, utango na utambaae!!!

    Mswahili!

    ReplyDelete
  4. Michu ehe! leta pics za lazaro na faraja kwenye harusi yao kama siyo issue..ndio hayo tu mkubwa

    ReplyDelete
  5. Ooh safi sana!Yaani napenda kitu kinachoitwa NDAFU!! Hii ni mila yetu ya kiafrika ya siku nyingi ndafu kutumika kama ishara ya upendo pia, lakini kwa kupenda mambo ya kizungu tumesahau kabisaaaaaa na kuhusudu KEKI! Haaaa safi sana NDAFU ni babu kubwaaaa!!

    ReplyDelete
  6. Jamaa kapendeza, ila kilicho muharibu demu wake ni hiyo hina. Otherwise, hata naye kapendeza.

    ReplyDelete
  7. Wamependeza sana hasa bibi harusi na hizo hina watu wa pwani tunaita nakshi nakshi urembo

    Heeh! huyu Single Mtambalike (richie) mbona kamtolea macho sana huyu ndafu, hahaha nahisi njaa ilimbana kiasi

    ReplyDelete
  8. HUKU NI KUDHALILISHA WANYAMA, HUWEZI KUMCHUNA MBUZI WA WATU HIVYO HALAFU UITE NDAFU!!!

    ReplyDelete
  9. Mambo si ndo hayo! Lisheni ndafu kwenye arusi! Haya mambo ya keki ni ya kizungu!

    ReplyDelete
  10. Hongera sana Kilasa, mwanafunzi wa mama yangu mama Nyalusi, hongera sana ndugu yangu, mmependeza sana, nawatakia maisha mema.

    ReplyDelete
  11. Unajua nini mimi kinaniudhi kuhusu ndafu.. huwa imepoaaa yaani inakuwa imepikwa sijui tangu asubuhi sijui jana yake! basi hapo inakuwa ya baridiii hata mtu huwezi kuifakamia inavyotakiwa! vinginevyo hao maharusi wamependeza, kaka bonge la handsome, bibie nae mzuri kinoma!

    ReplyDelete
  12. hii fasheni ya kuoa sasa naona imepamba moto

    ReplyDelete
  13. Duh...ukatili wa hali ya juu...mbuzi huyo kawakosea nini jamani...mbona hata huruma hamnayo...wako wapi hao jamaa wa 'animal welfare???

    ReplyDelete
  14. watu wengine bwana unasikitika hujui mbuzi kawakosea nini huoni kidhibiti mdomoni? alipokua anakula mihogo yao shambani ilikua ni vizuri eeh! sasa hiyo ni hukumu na somo kwa mbuzi wote watukutu mwanawane.mate yao huwa hatari sana wakitafuna tu mihogo inadumaa, adhabu hiyo nimeipenda wamenilipizia na mimi ndugu zake pia wanasumbua sana shambani kwangu

    ReplyDelete
  15. kuuliza sio ujinga ni mtu kutaka kujua au sio?
    Inaonyesha jamaa kwa jina lake ni Mkirsto na bibi harusi muislamu je harusi yao ilifungiwa wapi?kanisani au ofisi ya serikali?
    kwani inajulikana kwa mwanamke wa kiislamu haruhusiwi kuolewa na mtu wa dini nyingine mpaka huyo mume abadili dini yake na kuwa muislamu.
    NAOMBA JIBU

    ReplyDelete
  16. ohooooooo!hata wao wenyewe wanalijua hilo naona tuwaachie wenyewe na wewe simama na imani yako na vile uunavyojua na kuona ni sahihi.

    ReplyDelete
  17. Shoga umefurahi umejiachia ulimwengu wote wako tuu..Mmh hawana maana hao atakuletea mwingine sasa hivi vijana wa sasa wamecharuka na ndoa za mitala jiandae.. kama unabisha muulize eshe muhidin alivyotendwa na maulid kitenge

    ReplyDelete
  18. Didi hongera sana,mtoto mashallah umependeza.I hope your marriage last longer than the time you dated,once you find the one you love,you know you want to spend the rest of your life with them.Nakuombea Dua wasuuza vinywa wengi na waharibifu pia wamejaa,kama hawakuweza kuwa tenganisha mlipokua mna date then dont let them get between you now,lenu moja.

    ReplyDelete
  19. wewe mshamba unae sema unahisi Kilasa mkristo kilicho kufanya uelewe ni mkristo ni nini?wafrika si mmejaaliwa na majina ya miti shamba,sasa cha ajabu ni nini unamjua baba yake Kilasa (Mzee Mtambalike)ungemjua baba yake usinge sema hayo.Kilasa katoka matumbo ya Kiislamu muache babu ajilie vitu vya kingazija.

    ReplyDelete
  20. Hivi hao anon wote wanaosema oh sijui haki za wanyama ni uonevu wa mbuzi.
    sasa mimi ninaswali, huyo mbuzi akishachinjwa bado anasikia maumivu?
    mijitu mingine bwana, kwani nyie hamjalelewa mkila nyama au ndio siku hizi mnajitia ma-vegan.
    hamna lolote washamba wakubwa nyie

    hongereni maharusi mmependeza na keki yenu nzuri

    mdau
    canada

    ReplyDelete
  21. ISSA MIMI NIMEKUELEW NA HONGERA SANA MAHARUSI MEPENDEZA...HUYO NDAFU NI "HALAL" AU MAMBO YAENDA YAKIONGEZEKA..

    ReplyDelete
  22. We Mtambalike si wewe umesoma Oysterbay primary we.....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...