

Tarehe Mon Feb 11, 10:20:00 PM, Mtoa Maoni:
Tarehe Tue Sep 29, 11:16:00 AM, Mtoa Maoni:
kaka michuzi hawa wasanii wa bongofleva badala ya kujenga wanajengua zaidi kuliko kujenga.angalia sasa ni wao ndiyo waliofanya neno nyimbo litumike katika umoja wakati lenyewe asili yake ni wingi,hivyo kuua neno wimbo ambalo hasa ktk umoja ndiyo linastahili na si nyimbo.kama mdau kutoka 'us' alivyoandika "nyimbo yako hii super----" badala ya kusema "wimbo wako huu super----"ni ulemavu ambao umekomaa tangu hapa tz hadi huko ughaibuni kwa kweli inasikitisha na kuuma sana.hebu wasaidie hao wasiojua makosa kama haya.na hasa hawa wasanii kwakweli wanaharibu kama si kubananga lugha yetu ni aibu huko duniani hasa ukutane na mkazi wa huko ambaye alikuja hapa tz kujifunza kiswahili halafu karudi kwao.umeongea hivi halafu yeye anakusahihisha utajisikiaje? kwakuwa wao ndiyo waliharibu,basi ni wao ndiyo watengeneze hasa kwakuwa watu wengi huwasikiliza kupitia vyombo vya habari ama kwenye matamasha yao mbalimbali.
mwanangu kassim nyimbo yako hii super ile mbaya mademu wakibongo hata wakikenya waliopo u.s wanaifagilia sana hasa hasa wa new york na D.C yani tukiwa na mawazo tunaifungulia nyimbo yako basi mawazo yote yanayayuka mwanangu hongera sana, hivi sasa niko offisini namuaza mpenzi wangu huku nakula nyimbo yako na kuburudika. hongera sana, njo u.s ku perform, njoo njoooo kassim weeee.