wadau kunradhi. katika kupitia mitandao ya wadau wengine jioni hii, nilipofika jambo forums nimepata kitu hicho. nimejaribu tena sasa hivi mambo ni yale yale. je kuna anayejua kimetokea nini ama ni mimi tu mwenye kuikosa?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 46 mpaka sasa

  1. Wawili washikiliwa na Polisi kwa sababu ya Jambo Forums. Kwa maelezo zaidi visit www.klhnews.com

    ReplyDelete
  2. Even mi nimeanza kuitafuta muda mrefu sana kuanzia kwenye saa kumi na moja mpaka saa nne hii haipatikani, Lakini kwa data nilizonazo ni kwamba kuna mdau mmoja wa JF emechukuliwa na watu waliojiita ni maafisa usalama na wamemwambia wanamchukua kwa ajili ya mahojiano naye lakini wadau wengine wa JF wanaendelea kumtafuta baada ya kumtafuta katika vituo maarufu vya polisi bila mafanikio, sasa yawezekana kuwa haya ndo matunda yake baada ya huyo mdau mmoja kukamatwa....

    Inasadikika kuwa wanausalama wanahangaika kujua ninani haswa anayehost hii JF na ni nani haswa anayelikisha habari nyeti kwenye wanja la JF.

    Hope itakuwa sawa ngoja tuone maana pale ndo sehemu ya kujua mauozo ya mafisadi wa nchi hii.

    ReplyDelete
  3. Duh wameshafanyiza huko tayari! Yaani wamebenewa! Dalili zilionekana tangu jana! Tutakoma nchi hii!

    ReplyDelete
  4. Jamboforums imefungwa sasa hivi kwa vile polisi Tanzania wameanza kuwakamata memba wa JF walioko TZ wakidhani kuwa ndio Invisible au robot yule anayerekebisha mambo ya JF

    ReplyDelete
  5. Si wewe tu kaka,naona kuna tatizo kubwa. Nahisi hii site imeshafanyiwa ufisadi. Mapema kulikuwa na taarifa kwamba muendeshaji mkuu wa site hiyo na jamaa wengine wawili wamekatwa na watu wa usalama wa Taifa, mwenye taarifa zaidi atumegee humu pse.

    ReplyDelete
  6. Mimi nilianza lushindwa kusikiliza misiki jumapili jioni....Lakini labda wanafanya upgarade na hawatumii log na ndio inakua hii shida site inakua down...
    Natumaini watarudi soon kwa vile na miss nyimbo zao

    ReplyDelete
  7. Soma KLH news ya Mwanakijiji, wanadia wameifunga sijui kuna watu wamekamatwa na polisi ndio wameifunga. Nayo hiyo JF na KLH news nafikiri ni mali ya Chadema.

    ReplyDelete
  8. Nahisi hii ngoma JK ameomba msaada wa FBI wakaipiga chini kama wanazima kibatari vile, hili litakuwa bonge la zawadi kwake kwani ilikua inamnyima usingizi na ilikua inakua kwa kasi.

    ReplyDelete
  9. Leo Michu utapata maoni yenye akili sana kwa kuwa 'vipanga' wote wa JF hawana pa kwenda! LOL!

    ReplyDelete
  10. kaka michuzi,huu ufisadi sasa umezidi,naona sasa umeingia kwenye blog,hivyo wamiliki wa blog kaeni chonjo!

    ReplyDelete
  11. Hawajalipa subscription hao. Naona hawalipi mpaka wakatiwe!

    ReplyDelete
  12. Michuzi,

    Hiyo ndio demokrasia ya Kiafrika! Ukisema ukweli wewe mwongo na mzushi, yanayoandikwa Jambo forum yanawafichua mafisadi sasa imefikia wakati mafisadi kuchukua hatua kali.
    Navyosikia kuna wahusika wachangiaji wametiwa ndani na wengine wanatafutwa.
    Uhuru na Kadi?.... kazi ya chama!

    ReplyDelete
  13. Nimekutana na kitu kama hiyo.....

    Mafisadi oyeeee!!!!

    ReplyDelete
  14. Michuzi usishangae
    WanaHARAMU wametenda walichoamua kutenda. Kwani wewe hujui kilichoikumba JF?
    Wewe una bahati maana bado waoga kijani kijani ati! Najua unaweza kuamua kuuza IP zetu sie wadau wako. Hakuna neno itakuwa kheri tu ila naamini kwa moyo wako wa dhati hutafanya hivyo

    ReplyDelete
  15. kuna soo....jamaa wawili waku ndani..

    ReplyDelete
  16. Inawezekana wametumia "bandwidth" yao kwa siku, kwahiyo hosting account yao imesitishwa kwa muda au hawajalipia hosting kwahiyo wameisitishwa kwa muda...

    Ila sidhani tatizo ni pesa kwasababu wanatengeneza pesa nyingi kutoka adsense.

    Sitashangaa kama wanatengeneza zaidi ya $5000 kwa siku hasa ukiangalia wana matangazo mengi ya obama na clinton ambanyo yanawagarimu "adwords advertisers" zaidi ya $1 per click. Wacha bwana hawa jamboforum wana traffic isiyo yakawaida

    Michuzi weka adsense nawewe ili utengeze hiyo mihela. Kama unahitaji ushauri wa ku-monetize website yako nitakusaidi.

    Hata kama hatu nunui kitu tuta click hizo ads ili kaka yetu upate hiyo mihela.


    Ukiweka ads utaweza kutengeneza mpaka $10,000 per day and i'm not kiddin kwasababu traffic unayo tena FREE kutoka kwa loyal WADAUZ.

    I been running businesses online for more than five years... trust me I know what I'm talking about.

    Intrapreneur (internet entrepreneur) kutoka duniani-papaliko19@yahoo.com

    ReplyDelete
  17. Nenda http://www.klhnews.com/ utapata full information.

    ReplyDelete
  18. Michuzi kwa taarifa kuhusu Jambo Forums BOFYA HAPA

    Inaelekea kuna watu hawapendi uhuru wa habari. Lakini hawajui kuwa harakati za kwenye internet huwa haziwezi kuzimwa.

    Kama hawajui wakamuulize Mugabe ambaye ameonja joto wanaharakati wa internet.

    ReplyDelete
  19. Huko JamboForum moderator muhimu kasababisha hiyo suspension.Lakini kumbe wewe Michuzi na ujanja wako wote unatumia Internet Explorer?

    Mambo ni Firefox bwana, halafu naona unatesa na Vista yako mwenyewe - anyway wabongo wengi ni Windows sababu Mac ni gharama wakati Linux wengi hawaijui.

    Jambo itarudi, na ikishindikana itaundwa forum mpya.Kama ni njama za mafisadi basi watakwama.

    ReplyDelete
  20. mimi nawapata poa tu labda wewe na kilaptop chako kimeo

    ReplyDelete
  21. Wewe hapo juu labda unawapata jambo network...jambo forum hawapo hewani

    Yaani mafisadi walikua wanasubiri tu Bush aondoke nchini

    ReplyDelete
  22. HII SHUGHULI YA JACK PEMBA KAINGIA MITAMBONI KATIKA MAHAKAMA KUU YA UINGEREZA KAOMBA IFUNGWE KWA SABABU IMEMWARIA JINA, HIVYO MAHAKAMA YA UINGEREZA IMEWEKA INJUCTION IFUNGWE. FOR MORE INFORMATION GO TO GSB WEB SITE.

    ReplyDelete
  23. Duh, hata siamini. Yaani jamaa chupi zimewabana mpaka wameamua kifungia forum yetu yenye akili ya JAMBO FORUMS? Sasa hii ni kwa sababu jamaa wa JF ndio walioleta taarifa za kupigwa kwa wapinzani kule Kiteto?? Nadhani CCM sasa imeanza kutapatapa.

    Anyway, tutafika tu.

    ReplyDelete
  24. SIDHANI KAMA JAMBO FORUMS INAWEZA KUFUNGWA KWA SABABU YA KUTOKULIPA SUBSCRIPTIONS, NINAVYOJUA MIMI KUWA CHADEMA INASAIDIA KWA HALI NA MALI KUIWEZESHA JF IWEPO. NA CHADEMA HAIJASHINDWA KWA HILI.
    HUENDA LABDA KUNA TATIZO JINGINE.

    ReplyDelete
  25. Wakimbizi wa JAMBO FORUMS tushapata kambi nyingine ya kujistiri...hapa:

    http://wazalendo.wordpress.com/

    Brother michuzi tunashukuru kwa msaada unatupatia

    ReplyDelete
  26. HII INANIKUMBUSHA SOO LA BCSTIMES.COM ENZI HIZO NDIO FORUM ZA KWANZA KWANZA JAMAA YANGU POPE ALIPATA MATATIZO KAMA HAYA ALIWEKWA NDANI NA KUHOJIWA NA ILE FORUM ILIFUNGWA, NAWAKUMBUKA WATU KAMA
    POPE
    MWANAKIJIJI
    DUME
    LAPTTP
    MKANDARA NA WENGINEO NILIPATA KUJUANA NAO PALE NA LEO NAWAONA HADI HUMU.
    SO KWETU HAYA MAMBO BADO WANATAKA YAWE NA MIPAKA.

    MDAU MPONJIKA

    ReplyDelete
  27. Wana Jamboforums, inawezekana wameturn against us kwa sababu kadha wa kadha. So far, tutapatikana kwenye wwww.klhnews.com, at this particular moment watu watajadili njia mbadala kwenye hiyo website.

    Brother Michuzi thanks kwa kutupa hifadhi kwa muda hapa.
    Mtanganyika

    ReplyDelete
  28. forum haina matatizo ya kifedha,na wala hakuna chama chochote kile cha siasa kinalipia forum. Ni propaganda tu za serikali ya TZ na wale wezi wa fedha za serikali ndio maana imekuwa imekuwa blocked, lakini itarudishwa tu, msijali.

    ReplyDelete
  29. Jambo Forum is not affiliated to any political party in Tanzania. It is an independent institution that welcomes all Tanzanians who are pushing for changes for betterment of Taifa.

    Yes we are critical of malaise and poor governance by Serikali, that is why you will brand us Anti-Government.

    We are going to stay strong and keep up the fight.

    JF Premium members and Senior expert members please email me kishoka70@yahoo.com

    Rev. Kishoka

    ReplyDelete
  30. Finally the chickens have come home to roost!! Bora wameifunga na ningefurahi sana kama yule bishoo aliyekuwa anajiita "Invisible" wangemtia lupango pia.

    La ajabu ni kwamba kulikuwa hakuna uhuru wa kutoa maoni kwenye ile forum wakati wao walikuwa mstari wa mbele kudai uhuru huohuo wa kutoa maoni. Ile slogan yao ya "Where we dare to talk openy ilkuwa ni gimmicks tu

    Halafu kuna baadhi ya wachangiaji walikuwa wakijiona wao ni elite mle na ukiwapinga au kuwashutumu basi wanakutishia kukufuta uanachama (haswa yule primadonna aliyejipachika jina la "mwafrika wa kike"). Yote kwa vile wanajuana wakati wao hapohapo walikuwa wakilaani usiku na mchana dhana za cronyism, favoritism, nepotism etc.

    Na ule msemo wao wa eti walikuwa pale "kumkoma nyani giladi" naona sasa kibao wamegeuziwa wao ... bwahahaa! :-)

    Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!

    Mzee Avenue Mavuzi

    ReplyDelete
  31. hapo wanachemsha tu wabarikiwe kwa muda ,,,,,,,,,,mambo zenu tetehhhhh mnachekesha wanapoteza muda wao,,,bugup mwanakijiji invisible,,tupo pamoja jamani
    jamani haloooooooooooooooooo

    ReplyDelete
  32. kwa upande wangu mimi jambo forum naiona kama genge la wahuni tu! Ukisoma mawazo ya watu kwenye ile forum kwa hakika utaondoka siku hiyo hiyo ya kwanza.

    Mawazo mengi ya watu yamejikita kwenye vitu vya kufikirika tu! Uchochezi na uwongo! Dini, na upuuzi mwingine mwingi sana. Mtu anaweza kusoma section ya bible au Quran akaamua iwe thread! Waht is that?! Kwa kweli, kwa mtu ambaye ni intellectual, kwa hakika jambo forum atasikiliza music tu. Maana huo hauna shida. The rest ni garbage. Na dhani na watu wanaochangia huko ni GARBAGE pia.

    Laiti kama wangeweka majina yao, sina shaka ingedhihirisha ninayosema. Ndo maana wanaficha majina. Lakini ndo mambo ya DEMOCRARY

    ReplyDelete
  33. Ooh Kumbe JF na KLH news ni mali ya Wachaga oops sorry CHADEMA, sikujua hilo. Haya na nyie CCM tafuteni forum yenu sio kufungia forums za vyama vya upinzani ala!

    ReplyDelete
  34. Nyie vilaza mnaoponda na kukandia JF mna walakini katika uelewa wenu. Kumbukeni kwamba yale ni mawazo ya watu, na kamwe huwezi kumzuia mtu kuwaza! Huwezi kuzuia mvua ama jua! Kama mnadhani JF ndio imekufa poleni sana, kwani hamjui mtendalo, bado inaendelea huko kwingine kama kawaida. Kile sio chama cha kisiasa, ni vyama vya kisiasa, ni taifa huru, ni serikali huru, ni mawazo huru nk, kwa kifupi inatisha!
    We Avenue ******** ulifungiwa kwa sababu wewe ni mwendawazimu, kwani kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kutumia jina ambalo huwezi kulitamka hadharani.
    Michuzi usibane maoni yangu, kwa sababu bado tunaendelea na juhudi za kuiweka JF hewani very soon!

    ReplyDelete
  35. Wana JF nimecreate blog itakayo tuhost kwa muda huu.
    www.jamboforums.blogspot.com , vile vile kwa wale premium members unaweza kuwasiliana na Rev kishoka, au fika pale klhnews.com.
    unaweza kuni email kupitia mtanganyika01@yahoo.com
    Thanks kaka michuzi

    ReplyDelete
  36. Acheni propaganda zenu, mmetumwa sasa kuja kuichafua JF? Hamtafanikiwa, JF ina mizizi iliyokomaa na itarudi kwa nguvu zote.

    JF sio CHADEMA wala hailipiwi na CHADEMA. Inaendeshwa na Watanzania wenye moyo na mapenzi kwa nchi yao.

    Haya ni mapambano, njiani kunaweza kuwa na miiba na visiki, lakini tutavuka tu.

    Kama tulivyowaumbua Richmond na vibaraka wao, BOT na mafisadi wakiongozwa na Rostam. JF itaendelea kudumu na kutetea maslahi na maliasili ya Watanzania.

    Msiyumbishwe na hao wanaoleta siasa za mafisadi hata kwenye mambo ya maana.

    JF inakuja kwa nguvu zote, tunaomba muwe wavumilivu. Muda sio mrefu tutakuwa na nguvu zaidi ya hii tuliyokuwa nayo sasa.

    Kama kuna mtu ana visa na Mwanakijiji au Mwafrika wa Kike basi akapambane naye kwa hoja, at JF we dare to speak openly.

    Mwambie Lowassa kwamba JF ni garbage, mwambie JK, kwamba JF ni garbage, Mwambie Hosea kwamba JF ni garbage. JF imewakuna pasipokunika na ndio maana mnaanza kuleta propaganda.

    Hatutawaachieni mwaka huu mpaka kieleweke.

    ReplyDelete
  37. we will be back soon.i know it so sad for Tanzania,

    it is my hope Mungu atalipa kwa hili?kwanini iwe hivi.

    Mzee Pinda unaanza Vibaya,Naomba sana utusaide kwa hili!

    tatzi o ni lipi?

    Jf on Fire soon,I need the archives only.

    ReplyDelete
  38. Huyu mwanakijiji mnafki nambari wani anajifanya amesikitika kufungwa JF kumbe anafurahia watu wajae kwenye website yake ambayo siku zote imekuwa imezorota. Wadau wote wa JF njooni hapa kwa Michuzi tuendeleze libeneke. lakini tuache ushabiki wa Chadema ambao wameshindwa kulipia fee ya forum

    ReplyDelete
  39. Ebwanajamaa walikamatwa na polisi mmjo toka DAR TECK na mwingine akitokea ARUSHA.MDINGI wao ndo alitoa mchongo wakamatwe.

    ReplyDelete
  40. KWA KWELI IWE TU HAWAJALIPA FEE.ILA KAMA NDIO WAMESHIKILIWA NA POLISI TUTAANDAMANA HADI IKULU JK ATUELEZE KULIKONI AMA LA TUTACHUKUA SHERIA MKONONI.TUMECHOKA NA MAFISADI.WAISHI VIZURI KWA JASHO LA WENGINE.

    ReplyDelete
  41. Wanamjamvi, naomba niweke bayana JF na KLHnews vyote si mali ya CHADEMA. CHADEMA kwa sasa haina chombo chochote cha habari zaidi ya tovuti yake www.chadema.net. Ingawa baadhi yetu wanaCHADEMA tumeshikiriki mijadala JF na kwingineko kama watanzania wengine wanavyoshiriki. Tuelewe kuwa mabadiliko hayana chama, wapenda mabadiliko wanaweza kufananishwa kwa dhamira zao za kutaka mabadiliko. Hivyo, kupotea kwa mitandao ya namna hii ni hasara kwa wote bila kujali itikadi. Ni pigo kwa wapenda ukweli na fikra mbadala. Leo nilikuwa mambo ya ndani asubuhi na nimeonana na Mac na Mike pamoja na Wakili Tundu Lissu. Kwa kweli tumeelezwa mengi na wao na hata polisi waliokuwepo. Sitapenda kusema chochote kati ya yale tuliyoyazungumza. Furaha yangu ni kuwa vijana wenzetu wameshatoka polisi na sasa wako mtaani. Kama kuna mwenye kutaka chochote awasiliane nao. Na nimejikusuru kwenda huko leo kwa kuwa mimi ni mwanachama wa JF, na muumini mkubwa wa hizi jumuia za TEKNOHAMA. Lakini kwa upande mwingine, Mac ni rafiki yangu wa siku nyingi. Nawaombeni tuwaunge mkono vijana wenzetu katika harakati zao hizi bila kujali itikadi kwa kuwa faida yake ni kwa taifa letu. Lakini pia, waswahili wanamsemo kwamba 'mwenzio akinyolewa nawe tia maji'. Tukiruhusu JF ikazama, wakimalize JF jiulize, ni kijiwe gani kitafuata? Kwa maelezo zaidi wasiliana nami kupitia mnyika@yahoo.com au 0754694553. Nawatakieni heri. Pamoja tutashinda.

    JJ

    ReplyDelete
  42. Tamko langu kuhusu suala hili linapatikana hapa: http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/02/kwa-niaba-ya-baraza-la-vijana-wa.html

    Kijua ndio hiki, tusipouanika- tutautwanga mbichi.

    Mnaweza pia kutembelea www.klhnews.com naona Mwanakijiji na wengine wanaweka updates za mara kwa mara kuhusu suala hili.

    Bujiku Ngw'aka(kwa wale walio nyumbani)

    JJ

    ReplyDelete
  43. WE ANON FEB 20,2008 4:16:00 UNAAKILI KWELI WEWE?/ AU NA WE NDO WALE WALE??

    UHURU WA KUTOA MAONI AMBAO TUNAUPATA KLH NA TULIOKUWA TUNAUPATA JAMBOFORUMS KWA MICHUZI HUWEZI KUUPATA DAIMA.

    MICHUZI ANAOGOPE ASIJE AKABANIWA NA YEYE NA NDO MAANA UKIPOST COMMENTS ZENYE KUFICHUA MAOVU YA SERIKALI AU VIONGOZI WA SERIKALI HAWEZI KUYAPOST KABISA SASA WE UNAWAAMBIA WATU KUWA MWANAKIJIJI NI MNAFIKI WAPI NA WAPI BWANA??

    GROW UP MZEE AMKA SHITUKA PIGANIA NCHI YAKO.

    ReplyDelete
  44. sasa kanga zilizokua zimeandikwa we cherish democrasy alivyokuja Bush zilikua zina maana gani? Au ilikua kebehi tu....Where is the freedom of speech in our mother land...Sijawahi kusoma hiyo blog( I wasn't aware of it) Lakini kama ni kweli watu waliyoandika humu ...basi we have a long way to go....

    ReplyDelete
  45. Hakuna Demokrasia ya kweli Tanzania. Leo wanaanzia kwa Jambo Forums kesho watakuja mpaka kwa Michuzi au Mjengwa na kuwaambia wazifunge blog zao. Mambo mengi kuanzia Kashfa ya Richmond, Benki Kuu na nyingine nyingi zilianzia Jambo Forums.

    ReplyDelete
  46. jamani mimi niko bongo niko form one pale makongo cjui hiyo jambo forum inamaanisha nini naombeni mnisaidie kunielekeza ni kitu gani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...