Mashaka akila pozi
Mashaka akihutubia mamilionea kwenye hafla ya Rotary
John Mashaka na milionea Joan Cooper


Hoya Wadau,


Nyuzi hiyo hapo nimeipigani kwa udi na uvumbi kuipata. I am proud of this guy. He is a Tanzania na story yake ilitokea kwenye gazeti la Charlotte Observer.
Bwana Michuzi, lazima tuwape watu hongera wanazostahili, hiyo dola 200 niliyolipia kuipata hii story ni kidogo sana kulinganisha na kazi anayoifanya jamaa kwa ajili ya nchi yetu. Hata na wewe siku moja nitakutumia kizawadi kwa maana unaifanyia kazi nzuri sana Tanzania.
Nadhani wengi sasa inabidi watambue mchango wako kwa Nchi yetu. Huyu kijana ni mdogo sana, miaka 30 tu! Huku anawika kwenye ma business week magazine.Kadhalika anafanya kazi Wall-Steet, sehemu hata wazungu wengi wanaiotea ndoto.
Wazungu na vituo vyao vya redio na televisheni wanamhoji kila mara, anapanda sana chati, lakini kikubwa ni moyo na bidii aliyo nao, ni kijana wa ajabu sana. Mimi sijamuona huso kwa uso, lakini namsikia kila mara.
Wabongo tunapanda Chati, vijana wetu wanaamka sana sasa hivi.


Mdau Jumanne Kavishe






JOHN MASHAKA, A PEACE- MAKER IN THE MAKING

By our Staff Writers
04 March 2008
The Charlotte Observer

He sat quietly in a business, navy blue suit, amidst prominent, well known corporate heads in the Cozy and exclusive, South Park Manzetti Restaurant Board Room. Until he rose to speak, everyone, all members of the prestigious Rotary Club International, wondered what this quite, humble young man was up to.

As the say goes, that, do not judge a book by its cover, well, he proved those who judged him by his quietness wrong; he had more for his listeners than the expensive suit he wore. His heart spoke louder than his voice

His soft tone did not stay soft for a long time; his eloquence rented the room and pierced through many hearts; John Mashaka, delivered a well thought concise and poignant speech that touched different aspects of human suffering.

“Why must we kill each other? Why must we hate each other? And how for how long are we going to stand while seeing the world burn in ashes? I am not a philosopher or a politician; I am only a concerned private citizen who wants to see the best out of men.

I only want to see human living by each other happiness not by each other’s misery. I want to see a world where humans are not being treated as charity cases but as humans” These were Mashaka’s concluding sentences.

Not a stranger to the podiums or headlines, John Mashaka, is becoming a household name by his emotional and inspiring speeches across the state.


Joan Cooper, Cooper & Company’s, CEO, a well known millionaire, could not help herself, but break in tears to hear Mr. Mashaka narrate his horrific stories of suffering while visiting Tanzania, last August.

He is indeed God sent servant. The world needs more of Mr. Mashaka, I was particularly touched by his humility and love towards humanity, recounted Ms. Cooper.

Wachovia’s Investment Banker, Mashaka, balances his busy, fast paced Wall-Street work by donating his time to charitable organizations across the country, and takes three weeks annually without pay, to help people in his native country of Tanzania with his own funds
Mashaka narrated seeing 20 children at Safina-Orphanage in the middle of the slams go without food, and the most touching story was about a two year old boy, suffering from Meningitis at Shirati-Hopsital who could not receive treatment, due to lack of $12

John Mashaka, a native of Tanzania, grabbed headlines in 2005; after he sold his car and returned to his homeland to help his village during famine, with food and clean water. His latest trip to Tanzania was featured in Business Week Magazine’s, December edition.

He is currently planning to establish his own foundation that will cater for his village’s social needs such as a secondary school, a clinic and a fund to sponsor bright kids into higher learning institutions

A 2004 UNC graduate, Mr. Mashaka is not your typical young man; he is a man with a mission, he is well respected, and stands tall in his peer group, and could not have come at a perfect time, when the world need millions of generous and passionate people like him




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 58 mpaka sasa

  1. Hongera kaka yetu Mashaka,sasa Michuzi hizi ndio habari za kutuletea maana zinatupa changamoto na sisi vijana kujiendeleza kama huu mfano mzuri anaouonyesha Mashaka. Sasa zile ulizotoa za mdada wa Play Boy sijui inanisaidiaje mimi binti wa kitanzania. Inabidi watanzania tuwe tunatoa mifano kama hii kila wakati ili kupeana changamoto na sisi kujiendeleza sehemu yoyote tuliyoko ulimwenguni na tujue kwamba vitu kama hivi vinawezekana na sio kwamba ni njozi tu. Kama Mashaka ameweza hata wewe na mimi pia tunaweza, so keep up the good work bro, and God bless.

    ReplyDelete
  2. It's an inspiring story and we are proud of what he's achieved and yet to achieve.

    ReplyDelete
  3. michuzi unajitahidi basi anakaribishwa tanzania kusaidia jamii hasa katika kipindi hiki, hongera zake jamani, mpeni moyo ndo maisha yanavyokwenda, sasa aendelee na moyo huo huo, sio kukatishwa tamaa.

    ReplyDelete
  4. Kweli huyu Kijana nastahili sifa,nimesearch nikamuona na kusoma katika hii link.

    http://www.wsoctv.com/family/15032767/detail.htmlatika hii link .
    Wewe pia uliyetoa habari hii asante watu kama nyinyi ndio mnaotakiwa. Anataka kuanzisha foundation keep us informed tunaweza kuchangia chochote maana sisi tuliohuku nje saa nyingine tunahitaji kushiriki pamoja. keep it up Mashaka

    ReplyDelete
  5. Keep up the gud spirit!

    ReplyDelete
  6. Mashaka, endelea na kazi hiyo nzuri.
    Hongera sana. Kaka Michuzi vitu kama hivi vinafurahisha na kutupa moyo wa kuifuata mfano kama ya akina Mashaka.

    ReplyDelete
  7. Mashaka alikuwa Shirati?? Shirati- Tarome !! well hapo kweli amenikumbusha mbali sana kwani miye nnandugu huko Mr mashaka.

    Wishing you all the best.

    Robert.

    ReplyDelete
  8. THIS IS THE REAL BONGO CELEBRITY; HUYU NDIYE CELBRITY WA KWELI, HACHANA NA WALE MACHANGU DOA WA VITUKO

    BRO, VIPI, MIMI NINACHOOMBA NI KAZI, MZEE KIKWETE MBONA VIJANA KAMA HAWA WASILETWE TANZANIA NA USOMI WALIO NAO WABADILISHE JAMII YETU. BRO MICHUZI, HONGERA SANA, HII NDIYO NEWS YA KUTUTIA MOYO HATA NA SISI TULIOCHANGANYIKIWA NA MAISHA

    ReplyDelete
  9. Kudos to you John Mashaka!!!
    What an inspiring atory, kuna msemo usemao "kutoa ni moyo usambe si utajiri"
    Keep it up John!

    & hopefully michuzi utatuletea stories nyingi za hivi, inabidi kupeana moyo tusingojee misaada na kukimbizana na never ending drama

    ReplyDelete
  10. Mashaka... Saafi sana mtu wangu!! Peperusha bendera letu hilo huko ughaibuni kaka....Michu, chukua tano mtu wetu manake ma dataz yako si utani!!!!

    Mungu Ibaraiki Tanzania..........

    ReplyDelete
  11. hivi kikwete amekuja hapa marekani ana utaratibu gani wa kuonana na watanzania, ni swali tu mbona wengine hapa us hatujamuona, ni vizuri kama akitangazia watanzania wote, maana sio rahisi huu ubalozi kutupa habari, ni za kuficha ficha tu.

    ReplyDelete
  12. I am very touched with the guy and God bless him. Watu wenye moyo safi na wa huruma kwa wenzao wako wengi, lakini wanaokwenda mbele zaidi na kuamua kujitoa kusaidia jamii zao wako wachache.

    Tubadilike na kufanya yale tunayoamini kwamba tunaweza kuyafanaya katika kubadili maisha yetu na ya jamii zetu.

    Real tears are not those that fall from the eyes and cover the face, but are those that fall from the heart and cover the soul...Mashaka yors are real tears!

    To worry about what you can influence is stupid, to worry about what you can’t influence is useless...You go Mashaka

    Never deprive someone of hope; it might be all they have. A word of encouragement during a failure is worth more than an hour of praise after success....You are on the right truck Mashaka, yes you are!

    ReplyDelete
  13. Asante sana Mashaka mungu akubariki,achana na mafisadi.Keep it up!Sure,hii ni challenge kwa vijana wengine.Michuzi haya ndiyo mambo tunayohitaji siyo mambo ya udaki.Tunataka ku-brainstorm,hatutaki machangu.(Michuzi Uwe unaweka machangu kimtindo wanasaidia kusafisha macho!)

    ReplyDelete
  14. No ability without oportuinity!

    ReplyDelete
  15. Hawa ndio wasomi wa Kitanzania. This is a Brainy, huyu kijana yetu macho tu, hachana na washenzi kama Richard, akili tupu, mamiss wanaochafua magazeti yetu, Huyu ndio Superstar wetu

    Kaka Michuzi, mimi ni dada mrembo sana na mzuri kitabia, natafuta mchumba, hivi huyu kaka ameshaoa au bado, jamani si uniunganishe naye niwe mama watoto wake, simtaki kwa sasabu ya umaarufu wake au utajiri wake, na mtaka kutokana na moyo alionao

    Jamani mbona wasio na bahati hawabahatiki.

    ReplyDelete
  16. Hivi huyu ni mtanzania au mzungu mweusi, mbona tabia zake siyo za kiafrika? wee mwafrika gani atauza gari lake kusaidia masikini? Thubutu

    Kaka mashaka, hongera sana, mungu akuzidishie. You are our hero, naomba tuwasiliane

    Kama michuzi naomba uniunganishe na huyu kaka

    Irene

    ReplyDelete
  17. Excellent post kaka Michuzi. Habari kama hizi ndio tunazotaka kusoma sio za hao machangudoa. Hongera sana kwa kijana mwezetu mashaka, anatutia moyo sana sana.

    Pia nampongeza mdau alitoa hoja kuhusu rais anapotembelea Marekani, ubalozi wafanya kuficha ficha habari za ujio wake. Wenzetu wa UK habari zinasambazwa kwa kasi na ubalozi, au sababu balozi wa kule ni mwanamke hivyo anakuwa anaushirikiano wa karibu sana na wafanyakazi wake na kufuatilia mambo kwa pamoja?

    ReplyDelete
  18. michuzi nakubaliana na huyo hapo juu, huu ubalozi wetu hapa dc, unaonekana kuwa na siri sana, raisi akija hapa, wengine hata hatupati habari inasikitisha na kukatisha tamaa, au hata kama waziri mku anakuja watu wa ubalozi wana wivu sana, wanasambaza ujumbe kwa watu wanaowajua kama wanakuonea wivu hawakuambii, utasikia tu mahali, asante sana kaka michuzi blog yako inanufaisha wengi kwani haabri ziko wazi na sio za siri, jamani tutafika kwa mambo haya.

    ReplyDelete
  19. sidhani kama kikwete anajua mambo hayo ya watu wa ubalozi, wengine wana wivu na wanafaidi, wanajifanya wana siri hamna tena, utasikia tu raisi alikuwepo. asante sana kaka michuzi ubarikiwe na mungu wa mbinguni milele.

    ReplyDelete
  20. Mimi naona Ubalozi wa Tanzania nchini marekani unahitaji kureshuffle sana....Ni mambo mengi tu hayana mpangilio.

    Simu yao inasema mon-fri 9-5 lakini ukifika pale asubuhi hawafiki mapema.Yule mwanadada pale atakuambia wao hawajaja bado.

    Ukipiga simu unaambiwa wako kwenye mikutano kila mara.

    Wanahitaji kutengeneza database ya watanzania watakao penda kuweka contact zao kuwa alert kwa mambo ya muhimu kama raisi akija USA etc. Zamani watasema ni expensive kusend barua kwa kila mtu lakini email ni free sasa sijui kwanini hawataki kufanya hivyo.

    Sasa hivi walipokua wanarenew passiport za watu wote ndio ingekua muda mzuri wa kutengeneza contact database ya kila mtu anaye hold passiport ya tanzania lakini wameachia hiyo chance sidhani itakua rahisi tena kufanya hivyo...na hawajui hata mbongo mmoja yuko wapi.

    They need a wake up call...kwa vile hata mtu mwenye sifa kama hizi sidhani kama wanafahamu alipo au kumfanya ashirikiane nao ili kusaidia mambo mengine au kurahisisha mambo mengine akitaka kupeleka misaada bongo...Sifa zote hizi lakini sidhani kuwa wanajua kuna wabongo wengi wanafanya mambo ya kujivunia kwa taifa letu lakini ubalozi ulivyojidistance na wananchi wake wala hauna habari....wak o watanzania wengi tu wanafanya mambo ya kufurahisha na kuipatia sifa nchi yetu lakini ubalozi hauna hata habari na hawafikiri kuw a hayo ni ya muhimu kwao...

    ReplyDelete
  21. nakubaliana na huyo hapo juu hili swala la passport sio dogo, unadhani hawa watu wanajali, maana wanazungusha sana sijui lengo ni nini, kuzungusha mara njoo kesho mara hiki hakijakamilika, ili mradi wanakukatisha tamaa ndio furaha yao, michuzi asante sana muungwana.

    ReplyDelete
  22. Kwanza kabisa nimetokwa na machozi, na kupata moyo kwamba siku zote mungu usikia vilio vywa watoto wake na kuwapa wakombozi. Marekani walipewa Martin Luther king, india Mahatma Ghandhi, Afrika Kusini Nelson Mandela, Tanzania Nyerere, na sasa Tumepewa John Mashaka….

    There is no question, this is God sent

    Ndugu zangu watanzania, ni swala la kutia moyo kuona kwamba kijana mdogo kiasi hichi anafanya mambo makubwa ya aina hii.

    Mawaziri wengi Tanzania, kazi zao ni kuweka mileage feki na kuzidi kuinyonya nchi, ilhali kijana kama huyu anafanya kazi za maana kiasi hichi.

    Nani anafaa pongezi zaidi ya huyu; Au Jack Pemba ndo tumpe sifa kwa kuja Bongo na uzushi? Huyu siamini ni MTANZANIA, nadhani huyu ni Mzungu mweusi.

    Jonnie Mashaka, Hongera sana, tunakutakia kila la kheri urudi nyumbani uikombea Tanzania, hela za Wall-Street isikufanyehuisahau Tanzania, tunakuhitaji sana na Usomi wako.

    Tungekuwa na vijana 10 wa Tanzania, kama Mashaka, Tungefika mbali sana kimaendeleo. Huyu akirudi, wizara atakoyopewa, msahau ufisadi kwa maana amesharidhika kabisa, hana sabau kuiba chochote. Niamini, huyu anakuja kuwa Rais Tanzania, there is doubt...

    ReplyDelete
  23. mICHUZI,
    MIMI NI MOJA WA MA MISS, HUYU KAMA NINAMFAHAMU SANA, NIMEPOTEZA CONTACTS ZAKE, UNAWEZA KUNISAIDIA KUZIPATA? NASHIDA NAYE SANA. HE IS GOOD FRIEND OF ME, AND I LOV HIM TOO MCUH

    ReplyDelete
  24. Rais Kikwete
    Mchukue huyu jamaa, aje akusaidie, huyu ni asset kubwa sana kwa taifa letu. Hachana na wakina Chenge

    Shukarni sana

    ReplyDelete
  25. Very inspiring story, I may sound gullible, but why did you have to pay $200 for the story??????????
    I thought once the story posts in a magazine/newspaper it's kind of free???!!!!!!!!!?????? Or was it the pic? I'm puzzled...

    ReplyDelete
  26. Hivi hapa US tuna balozi? Maana mimi passport yangu bado ni yazamani na imexpire four years ago. Every time nikipiga simu yao nakutana na crazy msg.

    I don't understand why Tanzanian government keep funding that sorry Embassy. I can't wait to see whoever works on that embassy.

    Michuzi, please send our complains to top bosses in the government about their nightmare embassy.

    Mdau wa US

    ReplyDelete
  27. Ni jana tu Forbes imekuja na list ya mabillionare duniani, namba ya pili imeshikwa na Carlos Slim Helu ambaye ni M-mexico aliyesema kuwa " He doesnt belive in charity to solve povert in the world", I think and I belive thats is very true , So My points is

    1. nachukia sana tena sana nikiona raisi wetu anaomba omba hela uku ulaya

    2. Vijana kama hawa wanajitolea kuutangaza umaskini wetu kwa matajiri ili watusaidie

    Please tena please naomba wa-aafrica hasa watanzania wenzangu tuamke tuache tabia ya omba omba tujitegemee....ila sivyo hamna maana ya uhuru ambao Nyerere aliupigania miaka 40 iliyopita.

    mdau
    Kwa bi Mkubwa!(USA)

    ReplyDelete
  28. sidhani kama kikwete anajua au kufanya research yeye si alikua foregin affairs jamani, awe anafanya uchunguzi, maana hata ile kesi wa afisa mizengo sijui iliishia wapi, michuzi asante sana unatusaidia kwa swala hili.

    ReplyDelete
  29. wadau nampongeza huyu jamaa kwa upande mmoja kwa kujituma na kuonyesha moyo wa kujali ambao sio wote walio nao!
    kwa upande wa pili naungana na mheshimiwa aliye kosoa tabia ya kujiendekeza na kusubiri kusaidiwa.
    nikweli waafrika sio tz tu, utadhani hii kitu ni genetical, wengi najua mtasema mazingira yetu yali tudumaza kwa kuokota matunda na kutopigwa na snow! wengine watasingizia historia ya utumwa.lakini ukweli unabaki palepale kuwa babuzetu walilala na hadi wakakutwa huko wamelala. nasisi tunaanza kufuata nyayo za kuwa maombaomba huku tukijisifia umaskiniwetu! hii inakera.
    ukiuliza zaidi ya 90% ya wananchi individualy ana plan gani hata kwa familia yake ya watoto 5, jibu hana! lakini analalamika serikali haina plani ya kumuendeleza, wakati yeye hana. by this i mean hata kama atapata opportunity kwa kuwa plan hana basi hataweza kuitumia.
    nacho sema hapa ni tuamke sasa tusiendekeze ujinga wa kujisifia umaskini na kuombaomba, hii inadhalilisha na kuondoa hadhi ya mwafrika. utadhani jamani hii kitu ni genetical??? maana waafrika karibia tunafanana tabia! hili nimekuja kuligundua baada ya kuishi na watu wa mataifa na mabara mbalimbali na kulinganisha tabia!
    we need to change!!! otherwise tuamue ku-give up and wait to go to the heaven if we believe in heaven!!

    ReplyDelete
  30. To the publisher of this story!
    If you are not Mashaka himself then you must be someone with close affiliations to him. With my humble you have too much exagurate the story, its rubbish! Dont be such ridiculus to fool people that you have paid $200 to get a story of so called "Mashaka"...that doesnt make any sense to me neither will to any broad thinker! With modern technology, internet, local newspaper and radio..why do you to pay for a story of Mashaka?Anyway, the dude is doing fine so as to many Tanzanians living abroad. I have been work tireless to address issue of povety and ignorance in Scotland, in my normal life i have a good job and stable family, i dont find any big deal whatsoever to what i have done so far. So congrats to Mashaka and yourself for your little effort to help your own family, its your responsible anyway..however the story have been too emphasized and overhyped!

    Nimeindika kiingereza ili michuzi asiiminyie..you not he is not rechable! haha ahaha
    Mdau wa blog,
    dogo Glasgow.

    ReplyDelete
  31. HUKO MAREKANI MMELIA SANA KUHUSU BALOZI. NAWASHAURI HIVI: MUOMBENI RAISI AWAPATIE BALOZI WETU KUTOKA HUKU SWEDEN AJE MAREKANI, MATATIZO YENU YOTE YATAISHA. UBALOZI WETU SWEDEN SAFI SANA, BALOZI YUKO MAKINI SANA NA NI MTU WA WATU SANA. HUYO WA MAREKANI ALETWE HUKU, TUTAMNYOOSHA, MAANA WATU HUKU NI EFFICIENT SANA NA UBABISHAJI WAMESHASAHAU..AJE HUKU SCANDNAVIA AJIFUNZE EFFICIENCY!

    ReplyDelete
  32. The so called Mdau Dogo from Scotland, first of all; you need to go back to class, and learn your English before you can Insult Mr. Michuzi's ability to understand English.

    You are a looser, who does not want to see the best out of his people. This young man has done so much, more than many of us, rather than encouraging him, you are laying some very baseless accusations. Do research, go to the internet, with your same medicine TECHNOLOGY, you will find plenty of this young man's story

    I do believe the story was paid for, due to copy rights reasons, as far as I know that is the only reason, to charge for that amount; Re-publication. Otherwise, you need to move from Scotland, urudi uchagani kuchuma kahawa

    ReplyDelete
  33. Jamaa nilikutana naye STAR-TV, he is a very simple guy, na ni mtu wa watu......... ila mademu ndo walimzingira sana

    Hongera sana, bwana, ila hawa watu wa porojo kibao ndo husiwajali kabisa. Wee endelea na hii kazi nzuri..... safi sana

    ReplyDelete
  34. michuzi kaka angu naomba tafadhali usinibanie hii comment, wanasema wa marekani aletwe sweden, watanzania hivi hamjui huyo wa marekani aliwahi kufanya kazi sweden, na ni ndugu na huyu wa hapa sweden, na alikotoka ndugu yake alikuwepo, wamefanya rotation, nyie mnataka rotation ngapi, hao ni ndugu ambao wote bado wako ubalozini, watanzania muwe mnafanya research. wana ndugu bado watawala.

    ReplyDelete
  35. michuzi asante sana sana, kweli unaweza kwenda kwa mambo ya passport, unazungushwa na kukatishwa tamaa, basi tu wivu na chuki, bila sababu ndio furaha yao kubwa, asante sana michuzi.

    ReplyDelete
  36. Barack Obama kila siku anavaa "expensive suits". Ila sijawahi kusikia CNN wala MSNBC wakizisifia suti zake. Hii inanifanya nifikirie mara mbili about the authenticity of this story.

    Hii story kaiandika mwenyewe Mashaka. He wants cheap publicity. Mind you, Cheap publicity is not the way of life.

    Naungana na mdau wa hapo juu alielieleza hili, ingawa mmemshambulia kwamba ana kiingereza kibovu, wakati na nyie mnashindwa kutofautisha kati ya neno "loser" na looser"

    Ni rahisi kuwadanganya watu wasio na exposure. Ila ni vigumu mno kudanganya critical thinkers na wengine wanaoelewa mambo.

    We know a couple of guys who are doing wonders in the US. None of them has ever appeared in primitive newspapers like the one quoted in this story.

    Kuhutubia mikutanoni na kusikilizwa na matajiri ni kitu kirahisi mno. Kinachohitajika ni kuwa-inform waandaaji wa shughuli na kama wakiona una jambo wanaloweza kulisikiliza (hata kama zikiwa ni chenga) they'll let you do it.

    Mashaka, you are still young to tell all these lies. You still have a very long way to go. Watch out!!!!

    Nakushauri... Mweleze kaka Michuzi ukweli kwamba ulikua unatafuta cheap publicity ambayo kuna jamaa wachache wameshakushtukia.

    Have a great day!!!!

    ReplyDelete
  37. naungana na mdau hapo juu, na so called "dogo". Kuuza gari lako bovu ($6000) kwenda kusaidia wazazi wako kijijini you are not a hero, its part of your responsibilities. Watu wengi wana kazi za maana na wanasaidia charity nyingi na sijaona big deal yeyote ya kutafuta publicity for the cheap shots. Wa bongo acheni ushamba wa kurukia meli msizojua zinaenda wapi, ili mradi anazungumza kiingereza na kuhutubia as ''guest speaker''. I see the story everywhere in every swahili blog..some anonymous say hurey, may be mashaka himself, how can you tell? Although critical thinkers have always looked for tangible critics to lay critics on, which are no where to be found.Wacheni ujinga amkeni!
    Bon, TX

    ReplyDelete
  38. I dont buy at face value without critical analyse the real worthy of a story. May be the so called ''John Mashaka'' as an Investment banker would know this and can emphasize publicly what he has done worthy that applaude! To me this story seems to be a junky story, cheap shot, overvalued and overcooked to gain publicity, unless you convince me otherwise rather than criticise my grammer.The same tactics are being used by politicians and potential politians to make people believe they are something to the society from nothing. I would never carried away with those kind of speculations without critical analye the whole saga behind it.
    The story appeal to the readers to applause for the ''new hero in Bongo'', new Mahtma Gandh and so many fancy titles without emphasize what he has done to acclaim those hoorays
    !...to me that was relatively a "cheap shot". I would love to know more than working for Wachovia, being invited for a speech at gala dinner and a hero for helping your peoples..because everybody does that collectively without such robust publicity.
    Wabongo tuwe makini!
    dogo, glasgow

    ReplyDelete
  39. Ukiangalia hizi comments zinazomsifia huyu jamaa utastukia kwamba the majority zina same flow. Ni rahisi kufahamu kwamba jamaa kajiposti humu kwemye michuzi blog, then akaanza kujichangia comments nyingi kujisifia... Eti expensive suits, eti mademu wanamfata... what the hell!!! Huu ni utoto by asilimia 100%. Mtu mwenye akili nzuri hawezi anza kujisifia kua alienda kituo cha televisheni halafu watoto wakaanza kumfatilia.

    Michuzi, tunakuomba uwe unachuja majigambo na vitu vyenye kueleweka. Visivyofaa uwe unavibwaga. Nakubaliana na anon wa Sunday, March 9, 2008 8:38:00 AM EAT kwamba huyu jamaa yumo mbioni kutafuta "cheap publicity"

    ReplyDelete
  40. WATANZANIA MAJUU, TUACHENI MAJUNGU

    Bwana Michuzi, ukiniruhusu, kwanza kabisa ningependa kukutaharifu ya kwamba huyu kijana nilimuona live na kumhoji pale Maelezo habari. Nilimuuliza, kwamba vipi, unajisafishia njia ya ubunge nini?

    Siyo lazima niwe Mbunge au mwanasiasa ndo niweze kuisaidia jamii yangu, wote tuna majukumu kuisaidia jamii, siyo lazime uwe tajiri, hii inatokana na ukweli kwamba amani haiwezi kuwepo, wengi wetu wakiishi katika hali tuliyonayo sasa hivi.Alinijibu bwana mashaka

    Kwa mtazamo wangu, naona huyu kijana ni mfano wa kuigwa na hawa wanaojiita DIASPORA ambao ni watu wenye wivu kupita kiasi, badala ya kejeli zao na wivu, watuonyeshe ni nini wameifanyia Tanzania.

    Huyu kijana hajajigamba hata kidogo, ila mwandishi wa Mwisho katika hii forum ameonyesha chuki kubwa sana kwa Bwana Mashaka, hebu atuletee hao watanzania waliopo Marekani wanaofanya makubwa. Hau wall-street ndo imewachanganya, fanya bidii na wewe ufike huko, badala ya kutangaza chuki.

    Tunawahitaji watu wanaotuunganisha siyo kutugawa, hawa pengine baba zao waliiba mabillioni ili wapelekwe kusoma, sasa hivi wamegeukia ulevi na maisha imewachanganya kwa hiyo hawataki kumuona yeyote akiwashinda.

    Mashaka, tunakuhitaji, wachanganye akili wajiangalie kwenye vioo ili watambue ni wapi wametoka na ni wapi wanakwenda.

    Habari za Mashaka kusaidia katika hospitali ya shirati tumezisoma hapa bongo, Kuchimba maji katika kituo cha mayatima na katika kijiji chake tumezisoma pia.Wazungu wakualike ovyo hovyo kwenda kuongea chenga au Ushuzi, toka zako hapa usitudanganye !!! Mbona wewe haujaalikwa?

    Tovuti inatupa habari zingine ambazo hatuzijui, kwa hiyo kwa upande wangu, Pongezi sana bwana mashaka, usiwajali hawa wanachuki, wakirudi makwao waongee kidhungu na bibi zao.......... ndo maendeleo yao kutoka majuu

    Watanzania, tuamke, watazameni wenzeti wakenya, Redio Zetu ni wao, ofisi nyingi ni wao, Lazima tuwapongeze wawakilishi wetu wachache, hasa sehemu nyeti kama Wall-Street

    Steven Mlawa

    ReplyDelete
  41. Bwana steven mlawa kama ni kweli, basi wewe inaonyesh utkuwa ni mwandishi wa magazeti ya udaku, ambao mnapewa hela kidogo muandike habari. mimi nipo bongo na nimefuatilia habari z huyu jamaa sioni ni kitu gani amefnya cha ajabu mpaka kuwaita waandishi wa habari kusema amechimba kisima na kupeleka pamba hospitali. hivyo ni vitu vya kawaida sana, hata mamiss wetu wanafanya kila siku na hawjitngai hivyo. Naona hao wadau wanauliza ni kitu gani cha msingi wana points. Tunakubali ujinga ndio sababu tunauza kazi kwa wakenya, ni wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
    Asante kaka michuzi kwa kazi nzuri,
    Ali baba, k'koo, dezim.

    ReplyDelete
  42. Kwenda kwenye mikutano ya watu na kuomba pesa ndio kunahesabika kama ndio kufanya makubwa majuu? Oh My God! Mungu ibariki Tanzania.

    Fanyeni kazi. Acheni majigambo

    ReplyDelete
  43. WADAU WENZANGU, NADHANI TUSIWAHUKUMU WATU BILA YA KUSIKIA HOJA ZAO !!! Nimefanya utafiti wa kutosha. Naomba msamaha kwa msimango wangu hapo hawali

    Tarehe 29/02/2008 kuna makala maalum katika gazeti la mwananchi ambayo yameandikwa kwa kina kumhusu jamaa Nadhani ukipata nakala hautakuwa na la kusema tena. Inabidi tuwe na ushirikiano,

    Faraja--DSM

    ReplyDelete
  44. mbona wanaolumbana ni watu wa majuu, kwani huko mliko hampatani? Nyie watu wajinga sana, mkichoka kusafisha vyoo vya wazungu mrudi kwetu, bado tutawakaribisha kwa maana ni watoto TZ Bongolandi! ila hachani mabo ya kuvurundana. Jua linatupiga sana ila bado tupo tunapiga mzigo kariakoo, na hatuwachukii wenzetu wanaojaribu hata na hizo hela zao kidogo kutusaidia

    ReplyDelete
  45. WABONGO WA MAJUU MTAKUFA MNASAFISHA NYUMBA ZA WAZUNGU KUTOKANA NA KUTOKUSHIRIKIANA KWENU NA WIVU KUPITA KIASI. KILA STORY KWENYE HIZI BLOGS ZIMEJAA KEJELI NA MATUSI...NI KIPI KIZURI MTAKUBALIA AU KUTULETEA KAMA MIZIKI MIPYA NA TABIA CHAFU ZA KUIGA

    MAMA HAMISI
    TZ

    ReplyDelete
  46. Kwa kweli hii blog ya michuzi ni kama kioo amabacho kinaanika mawazo ya watanzania wengi walioko nje. Ukiangalia comment nyingi za humu ndani zimejaa chuki na wivu usiokuwa na maana. Watu hawapendi kuona mwenzao kapiga hatua ya kimaisha na kufanya kitu positive. Kuweni na wivu wa maendeleo mtafanikiwa sana na kuleta positive impact kwenye society. Lakini kama mkiwa na wivu mbaya na chuki itakua affect wewe mwenyewe. Ukiangalia watu wengi ambao wametoa comment utakuta toka wamefika ulaya hawajafanya kitu cha maana. Wengi wako huko miaka 15 na waliondoka huku tanzania kuja kupata elimu huko nje. lakini wamesahau ni kitu gani kiliwaleta huko na kujiingiza katika masuala ya kipumbabvu na mashindano yasiyokuwa na msingi wowote. Kazeni buti na kurudi shule na acheni majungu yasiyokuwa na maana.

    ReplyDelete
  47. Wala vumbi, hao jamaa walioeleza apo juu wanawasaidia kuwaelewesha jinsi mlivyo rahisi kupigwa fixi ila nyie mnasema wanamwonea wivu huyu mshkaji. Haya basi, endeleeni kudanganywa basi na muendelee kusaini mi-buzwagi, mi-kiwira na kadhalika. Mnafunguliwa macho yenu muelewe jinsi mnavyodanganywa kirahisi na watu dizaini ya Mashaka nyie hamkubali. Endeleeeni kupigwa vumbi forever.

    ReplyDelete
  48. HUYU JAMAA TUNAFAHAMIANA SANA, NI MLINZI SUPERMARKET HAPA NY- CITY. ZAMANI ALIKUWA MLINZI PETROL STATION !!!!! MICHUZI NAOMBA HII TOPIC UIWEKE JUU WATU WASEME UKWELI, HUYU MBWIGA ANADANGANYA WATU NA KUJIFAGILIA BURE. KUOMBA MSAADA ROTARY SIO KITU CHA AJABU NA KUUZA GARI BOVU $6000 KUWASAIDIA WAZAZI WAKO SIO KUWA HERO. HAYO NI MAMBO YA KAWAIDA, HATA MAMISS WETU WANAFANYA KILA SIKU BILA KELELE NA KUDAI ETI..MADEMU WANANIFAGILIA, NINA SUTI KALI MPYA, NINA VIATU VYEUSI KIMOJA CHA KUSHOTO KINGINE CHA KULIA...THATS VERY OBVIOU! BAZAZI WEWE

    ASWILE
    MI

    ReplyDelete
  49. michuzi asante sana kwa kazi yako.
    OMBI BINAFSI , NINAOMBA HII TOPIC UIPUBLISH JUU NA IANZE UPYA. WADAU WENGI WANA MAWAZO LAKINI IKO MBALI.

    Chamungwana

    ReplyDelete
  50. Mheshimiwa Michuzi, mwaka huu ndo umetoa mpya! Vijana wa Kibongo wanahitajii hii injini kubwa imewasha moto ambao utawaamsha vijana wetu wanaojifanya wako majuu SAFI Sana

    Imekuwa kichekesho sana hata wanamuita Mlinzi wa Supermarket

    SAFI sana, vijana waone machungu!!

    ReplyDelete
  51. Kwa wale wasiojua Wall-Street, ni sehemu nyeti sana. Weusi wachache sana, ni sehemu ya nguvu ya mzungu, siyo rahisi huyu kaka kuingia huko. Ni millionaires

    Mabenki Makubwa ya Wall-Street Wachovia, Bank of America, Merril-Lynch, Goldman Sachs yanachukua top of the line brains kuingia huko, hata wanasheria wengi uacha kazi zao kuingia Wall-Street, kwa hiyo siyo rahisi hasa kwa Mtanzania kuingia huko.

    Nina MBA, pHD, nimeshindwa kuingia huko itakuwa sembuse huyu, hawezi kupata kazi Wachovia. Wachovia ndio ni namba tatu kwenye Investment Banking na mara nyingi uchague wanaofanya kazi kwenye investment bank toka vyuo vikuu moja kwa moja, handpicked.

    Yeye anaingia huko kama nani, mimi namfahamu sana, ni muhudu kwenye BAR, pale Dallas TEXAS amekuja marekani 2006 sasa hiyo wall-street amengiaje

    Benedito
    TX

    ReplyDelete
  52. Michuzi,

    Ukiangalia dictionary, neno "Wall Street" linamaanisha collective name for the financial and investment community, which includes stock exchanges and large banks, brokerages, securities and underwriting firms, and big businesses. Wachovia anakofanya kazi ndugu Mashaka nako kumo included kwenye definition hii.

    Mimi pia niko US. Nafanya kazi Bank of America. Sifanyi kazi ya ki-white collar, ila najipatia mahitaji ya maisha pamoja na kutuma pesa za kusaidia ndugu zangu nyumbani Tanzania. Kulingana na hiyo definition na mimi pia naweza kujigamba kwa wenzangu kwamba nafanya kazi "Wall Street", kama Mashaka alivyodai. Au uongo?

    Mimi naona hapa Mashaka anajaribu kuwaingiza mjini watu wa bongo wasioelewa mambo yanakwendaje. Kama wengi walivyosema hapo juu, Mimi nafikiri huyu dogo angepunguza kujikwaza kwani hauendani kabisa na umri wake. Yes, Kikwete anasomaga hii blog.. Ila nafikiri michango ya watu walioiweka kwenye topic hii itakua imemfungua macho na Rais Kikwete pia.

    Kuna wa-TZ wengi wameshikilia nyadhifa kuu kwenye ma-universities, wengine ni ma-engineer huko NASA. Watu wa dizaini izo wala hawaendi "Charlotte Observer" kupublish story kwamba wameuza vigari vyao vya dola 6000 ili kusaidia watu nyumbani.

    Wanaomfahamu huyu dogo inabidi wamkalishe chini na kumweleza kwamba hii sio njia nzuri ya kujitangaza, kwani ukikosea step tu unakua umejimaliza mwenyewe, kama alivyofanya kwenye suala hili.

    ReplyDelete
  53. Watanzania wenzangu, the only problem we are facing, an which is mostly contributing to the downhill trend of our country ni Wivu.

    I hope you guys can read and understand the contents of this story.All you are rebuffing is the ACT of the young man being written in the paper which should not be the case. He should have given the help and shut up!

    What you are failing to analyse or understand is the fact that, some of these meetings do have media. When someone is adressing they are taking a story, and publishes it; if that was the case, what the deal, or whats is the alternative you have?

    Wengine wanasema ni MLINZI wa Supermarket, yeah? basi huo ulinzi wake unalipa sana, na sisi watanzania tunavutiwa sana kwa kuwaona vijana wetu walinzi wanavyoijali nchi yetu, sasa wewe White collar in Bank of america what have you done for your country?

    In my opinion, even if this guy would have helped a single child with $100 for food, it was going to be 1000 times better that your words full of hate.

    Mimi Naishi Arizona for the past 17 years, natamani sana kurudi Tanzania na kusaidia, lakini hali ya uchumu imekuwa ngumu siwezi, hata nauli ya kurudi inanishina kupata, nimeenda shule and now teaching at a local community college, however with 4 kids to support, I cant simply afford helping anybody in Tanzania

    Sasa wewe Bank of america, au NASA, What are your plans for Tanzania, kama siyo kununua kila ya nguo na tamaa za magari? Gari lake bovu la $6000 limesaiia watu wake angalau !!!! Give us your alternative

    ReplyDelete
  54. Ikiwa kuna mtu hata mmoja wa kujinyima kutoa kila kidogo awezalo kuisaidia nchi yetu, lazima tumpe hongera

    Wangapi wenye mabillioni, na tena wenye nafasi nyeti wanaozidi kuinyonya tanzania bila kujali raia wa kawaida?

    Vijana nadhani hii ni chnagamoto kubwa sana kwetu....Ni lazima tuyatazame mambo kwa undani kabla ya kufungua vinywa vyetu in criticism " I guess this is human nature"

    I am sure you are also going to sell your FERARI and help your MASAKI friends and relatives, who cannot afford to pay for their Range-Rovers, hiyo ndo Tanzania yetu

    Masikini toka vijijini mwanza na bukoba endeleeni kuchangia kidogo kidogo, mwishoe juhudi zenu zitaonekana

    Kabula-Twamini
    Glasgow UK

    ReplyDelete
  55. TANZANIA, TANZANIA, TANZNAIA, nakulilia, wanao, wanauana, wanachukiana, TANAZANIA tuokoe Jamani tunaelekea wapi?
    Tunawezaje kushirkiana au kuwapongeza wenzetu, hao wale wezi na criminals ndio Watanzania wema?
    Tanzania, Tanzania,Hongera Tanzania

    ReplyDelete
  56. Kabula Kudo!! Mashaka, Hongera
    Hawa vitoto vya matajiri ndo vingi vinaingia humu kuchafua hii blog. Wanaandika ushuzi baada ya kushindwa maisha majuu. Hawataki kumuona mtu anawashinda. Wakimuona masikini anakuja juu, haya, sijui mlinzi, sijui mwizi, Zumbafu zenu wezi,walevi.Afadhali tunaye masikini mwenzetu anayetuwakilisha kuomba misaada siyo ile baba zenu wanaziiba. Heri raia moja moja waombe misaada siyo ile ya SIRIKALI za BoT na Richmond
    Vumilia kwani taratibu nchi nzima itakuwa nyuma yako....Bank of America mavi,huyu wamemuita Investment Banker, hayo yako yametokea wapi? Pelekini wivu zenu kijijini mkalime, mmetuchosha na madongo. Bongo hatunywi maji, ulaya ndo usiombe, kilichobaki ni kuanza kuwa......ili mkome adabu. Huu ni mwaka wa walalahoi, huyu ni mlalahoi mwenzetu siyo milevi nyinyi.Endeleeni kunywa na kustarehe, bongo mtarudi kwenye majeneza au ticket za one-way....Mashaka mungu akubariki

    ReplyDelete
  57. This gentleman has stretched his story to get publicity. A representative of shirati Hospital states that John Mashaka did come to Shirati Hospital. he came to pay the hospital bill of his sister in law. While there he ask if he could help pay for any hospital costs for children. They located 5 children who reported a need to pay the hospital bill and 1 mother who needed money to go home by bus. John Mashaka paid the bill in full which came to $73. There is a Safina orphange in shirati but there are no slums and children stay in homes and are supported by material aid from Safina organization.

    Also no child has been turned away for basic treatment at Shirati Hospital. Elective surgery does require a prepayment of part of the bill.

    John may have some good intentions but he is stretching the truth for money that will end up in his pocket.

    ReplyDelete
  58. To: Tuesday, March 18, 2008 5:36:00 AM EAT,

    Safina Orphanage is in Dar, a place called Mwananyamala

    I think the story is being read too much by too many people.I think this disqualifies the last comment. So is this guy from the hospital?

    I guess Wall-street people need money too

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...