April 2008
Wakati waandishi wa habari kutoka duniani kote wanafika kwa wengi katika mji mdogo wa Amstetten nchini Austria, polisi imeendelea kuchunguza nyumba ya familia ya mzee Josef Fritzl kutafuta ushahidi mwingine.
Wengi wanajiuliza vipi mzee huyu mwenye umri wa miaka 73 aliweza kumficha binti yake Elisabeth kwa muda huu mrefu wa miaka 24 pamoja na watoto wao katika chumba cha chini ya ardhi bila ya wengine kujua. Kwa muda huu wote alimbaka Elisabeth.

Polisi leo imechunguza ikiwa mlango wa chumba hiko uliweza kuwekwa na mtu mmoja bila ya msaada. Mlango huu una uzito wa kilogram 300 ulio wa chuma cha pua na mazege na wenye ufunguo wa elektroniki na unafunguliwa kwa kutia nambari ya siri. Mkuu wa upepelezi wa makosa ya jinai nchini Austria, Franz Polzer, alikanusha kwamba mzee Fritzl alikuwa na wasaidizi.

Bw. Joseph Fritzl alianza kumbaka binti yake Elisabeth alipokuwa na umri wa miaka 11. Wakati mtoto alifika umri wa miaka 18, baba yake alimtega kwenye chumba cha chini ya ardhi na kumficha huko.
Tangu hapo hakuwa tena na dalili yeyeto kuhusu binti huyo. Katika muda huu wa miaka 24 katika gereza lake, Elisabeth alizaa watoto saba, baba yake akiwa pia baba wa watoto hao.
Mtoto mmoja alikufa, wengine watatu mzee aliwapeleka juu kwenye nyumba na kumwambia mke wake kwamba Elisabeth aliwaacha mlangoni. Mbele ya familia yake, mzee huyu alisema, binti yake Elisabeth alikimbia nje ya Austria kuishi na kundi la kidini. Watoto wengine watatu waliishi na mama yao katika chumba cha chini ya ardhi.

Kulingana na mkuu wa polisi ya mji, Bw. Heinz Lenze, hakuna aliyejua kuhusu maisha ya wafungwa hao. Afisa alisema: “Aliunda picha kamili kabisa na mtuhumiwa alikuwa mwenye madaraka katika familia yake. Kulingana na uchunguzi wetu, si mke wala familia waliojua kuhusu maovu ya mzee huyo.”
Hata maafisa wa idara za serikali waliochunguza nyumba nzima miaka 9 iliyopita hawakugunda maficho chini ya ardhi.
Utekaji huu mzima uligunduliwa baada ya mfungwa Elisabeth aliweza kuzungumza na polisi baada ya kumsindikiza mtoto mmoja hospitalini. Polisi ilisema hali ya binti huyu ni mbaya sana, anaonekana kuwa miaka 20 mzee kuliko umri wake.

Kwenye picha zilizochapishwa na polisi unaweza kuona sehemu fulani ya maficho yaliyokuwa na jiko, choo na bafu pamoja na vyumba viwili vya kulala. Kwa ujumla maficho haya yalikuwa na ukubwa wa mita 60 za mraba.

Majirani wa familia hiyo bado wanashindwa kuelezea yaliyoendelea. Mmoja alieleza kuhusu namna, mzee aliweza kununua vyakula: “Alikwenda madukani kwa gari, lakini alikwenda hadi miji mingine, kwa hivyo haikujulikana kwamba ananunua vyakula vingi hivi.”

Kwa wakati huu, polisi pia inachunguza kesi nyingine ya mauaji na ikiwa mzee Fritzl alihusika naye. Pia kuna tuhuma nyingine ya ubakaji dhidi ya mzee huyu. Polisi inafikiria sasa kuwapa wahanga wa familia hiyo majina mapya.
HABARI HIZI ZINAKUJIA KUPITIA KWA www.malumbosjr.blogspot.com
MISS UNIVERSITY TALENT MUCCoBS -Moshi University College of Cooperatives and Business Studies - MWAMIN (BLUE GOWN) 1ST RUNNER UP ADELLA KIMAMBO (GREEN GOWN) NA 2ND RUNNER UP DARASIA (CREAM GOWN)
MR. UNIVERSITY TALENT-MUCCoBS EDSON TIBAIJUKA KATIKATI ,MSHINDI WA PILI ALFRED SENI ALEYEVALIA KOTI LA SUTI NA SURUALE YA KIJIVU MSHINDI WA TATU MIKONO MFUKONI GILBERT MUSHI

habari za uhakika zinasema dege aina ya airbus A320 (kama hilo piochani) la ATC linatarajiwa kutua uwanja wa juius nyerere dar kesho saa nane mchana tayari kuendeleza libeneke la usafiri wa ndani na nje ya bongo.

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda katika ikulu ya Entebbe jioni hii.
JK , Museveni wazungumzia Burundi
Rais Kikwete, Museveni wazungumzia Burundi Na Mwandishi Maalum Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo (Aprili 30, 2008) mchana amewasili mjini Entebbe, Uganda, na moja kwa moja kuingia katika mazungumzo ya faragha na Rais Yoweri Museveni wa Uganda katika Ikulu ya Entebbe.
Rais Kikwete amewasili Uganda akitokea Addis Ababa, Ethiopia ambako alikuwa kwa siku tatu kwa shughuli za nafasi yake kama Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).
Mazungumzo kati ya marais Kikwete na Museveni kwenye ziara hiyo ya kikazi ya siku mbili, yanahusu hali ilivyo katika Ukanda wa Maziwa Makuu, na hasa katika Burundi.
Rais Museveni ndiye Mwenyekiti wa hali ya Ukanda wa Maziwa Makuu, na Rais Kikwete ndiye Makamu Mwenyekiti.
Pamoja na kujadiliana kuhusu hali ya jumla ya Ukanda wa Maziwa Makuu, viongozi hao wawili walisisitiza hasa hali ya amani na usalama katika nchi ya Burundi.
Katika siku za karibuni, waasi wa kikundi cha PALIPHEHUTU-FNL wameanzisha tena mashambulizi dhidi ya majeshi ya Burundi, na dhidi ya mji mkuu wa nchi hiyo wa Bujumbura, kinyume cha makubaliano ya amani kati ya pande hizo mbili.
Kabla ya kuwasili mjini Entebbe, Rais Kikwete alikuwa Ethiopia ambako alishiriki katika shughuli za AU, ikiwa ni pamoja na kushuhudia mababidhiano ya madaraka kati ya uongozi wa zamani wa Kamisheni ya AU na ule upya.
Kamisheni ya Afrika ndiyo huendesha shughuli za siku kwa siku za AU. Katika makabidhiano hayo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya AU, Alpha Omar Konare wa Mali alimkabidhi madaraka ya kuendesha Kamisheni hiyo Mwenyekiti mpya, Jean Ping wa Gabon Jumatatu wiki hii katika sherehe iliyofanyika Makao Makuu ya AU mjini Addis Ababa.
Mbali na kushuhudia na kusimamia mabadhiano hayo, Rais Kikwete pia alihudhuria kikao cha Kamisheni ya Amani na Usalama ya AU ambacho kilizungumzia migogoro ya Afrika.
no image
'MCHAWI' MWINGINE ABAMBABWA TABATA
Siku tatu tu baada ya kijana kukamatwa na kichwa cha mtoto, kijana mwingine, safari hii msichana, amekamatwa katika hospitali ya Tabata iliyopo Wilaya ya Kinondoni jijini Dar kwa tuhuma za kutaka kuiba mtoto wodini.
Rehema Kefa(18) Mkazi wa Mkuranga alikutwa akitaka kumtorosha mtoto huyo jana aliyekuwa katika wodi ya mateniti hospitalini hapo jana.

Inasemekana Rehema alibambwa na nesi wa zamu katika wodi hiyo ambaye ni mlokole, ambaye baada ya kuona mauzauza ya huyo msichana inasemekana alifanya maombi, na mtuhumiwa huyo akaanza kutambaa kama nyoka wodini hapo.

Polisi waliitwa na kumpeleka Rehema kituo kidogo kilichopo karibu na hospitali hiyo ambako alikiri kwamba yeye ni mtu wa juju, na kudai kwamba shughuli hiyo kafundishwa na bibi yake kwa jina la Salome Nganame.
Aliwaambia askari kwamba hakuwa peke yake katika skuli hiyo, kwani mafunzo hayo ya undondocha kafunzwa yeye na kinadada wengine aliowataja kama Asha Said(29), Fatuma Saleh(23) na Khadija Mpogolo.
Alisema yeye na hao aliowataja ilikuwa waibe pamoja mtoto pele hospitali na kwenda kumnyonya damu.
aliwaambia askari kwamba walipomkamata bibi huyo na wenzie walikuwa wanawacheki tu kwenye 'TV' yao huko waliko.
Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Kiongozi wa Chama cha Upinzani nchini Zimbabwe ,The Movement for Democratic Change(MDC)Bwana Morgan Tsvangirai jana jijini Addis Ababa wakati viongozi hao walipokutana kwa mazungumzo ya faragha katika hoteli ya Sheraton.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete awali alikutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe Bwana Stanley Shimbalasha. Pichani Rais Kikwete akisisitiza jambo wakati akizungumza na waziri huyo wa mambo ya nje wa Zimbabwe katika hoteli ya Sheraton jijini Addis Ababa jana jioni

Mzee anayetuhumiwa kumfungia kwenye chumba bintiye na kisha kuzaa naye watoto saba anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo huko Austria.

Mzee huyo Josef Fritz mwenye umri wa miaka 73 hapo jana alikiri kuwa alimfungia mwanaye huyo wa kike aitwaye Elizabeth kwa kipindi cha miaka 24 ambapo alizaa naye watoto saba.

Mkuu wa upepelezi wa makosa ya Jinai nchini Austria Franz Polzer alisema mmoja wa watoto hao saba aliyozaa na mwanaye alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa na kwamba aliutelekeza mwili wa kichanga hicho kwenye tanuri la nyumba yao.

Mdau Malumbo.

KAKA MICHUZI,


NACHUKUA FURSA HII KUWAWAKILISHA WATU WA UBUNGO WENZANGU KUELEZA KILIO CHETU JUU YA HILI BONDE UNALOLIONA.


HILO BONDE KABLA HALIJAFIKIA HALI HIYO LIMESHAWEKEWA VIKAO SI CHINI YA KUMI KUWACHANGISHA WANA UBUNGO WOTE, NA SISI RAIA KWA KUPENDA MAENDELEO TUKAITIKIA WITO WA SERIKALI YETU YA KIJIJI TUKACHANGA'TENA NA TENA. 'LAKINI KAKA MICHUZI, AMINI USIAMINI, TANGU TUCHANGE ZAIDI YA MARA 7 HAKUNA HATA KIPANDE CHA KOKOTO KILICHOWEKWA KWA BONDE HILO MPAKA LIMEFIKA HATUA HIYO.


SASA WATU WA KUKAMATA MAFISADI WASIKAMATE HUKO JUU TU WAJE NA HUKU VICHOCHORONI. WAPO' MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA UBUNGO KIBANGU NA DIWANI WAKE WAHOJIWE KUHUSU FEDHA ZA MICHANGO ZA HAPA.


MDAU
UBUNGO KIBANGU

mdau ughaibuni anaomba msaada kwenye tuta. anaomba kujua jina halisi ya ala hii ya muziki. yeye anafanya biashara ya vitu vya kitamaduni toka bongo, na anatumia tovuti yake kutangaza. nayo ni http://www.simplytanzanian.com/
leo nimepata heshima sio tu kutembelewa ofisini hapa dar na mzee wa busara, yusuf mahmoud a.k.a dj yusuf, bali pia kukabidhiwa kitabu cha picha kinachoelezea mambo yote ya tamasha la sauti za busara lifanyikalo kila mwezi februari ya kila mwaka kwa mwaka wa tano sasa. kitabu hiki ambacho kimeandikwa kistadi na kusheheni picha kibao za sauti za busara ni mkusanyiko wa matukio yote muhimu ya tamasha hilo ambalo limejipatia umaarufu mkubwa duniani kama 'the friendliest festival on earth'. asante sana dj yusuf na peter bennet kwa tunu hii.
kwa habari zaidi na picha za sauti za busara bofya hapa
mama mzazi wa mtoto salome yohana aliyechinjwa majuzi akiwa amepagawa kwa uchungu wakati akisaidiwa kuweka udongo kwenye kaburi la binti yake wakati wa mazishi tabata segerea jioni hii. globu hii inatoa rambirambi kwa wafiwa na kuomba haki itendeke ili kila aliyehusika na kitendo hiki cha kinyama ahukumiwe ipaswavyo.
Mola Ilaze pema Roho ya Salome Peponi - Amin
Baadhi ya watumishi wanaofanya kazi katika Kamisheni ya Umoja wa Afrika AU iliyopo jijini Addis Ababa Ethiopia wakimsikiliza kwa Makini Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipokuwa anaongea nao leo asubuhi katika Makao makuu ya umoja huo
JIEPUSHENI NA AJIRA ZA UPENDELEO - JK
Na Salva Rweyemamu, Addis Ababa
Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Kikwete leo ameuelezea uongozi mpya wa Kamisheni ya AU majukumu yake, ikiwa ni pamoja na kuepukana na kishawishi cha makamishna hao kuajiri ndugu zao katika Umoja huo.
Akizungumza na makamishna wapya ambao walichukua madaraka ya kuongoza Kamisheni hiyo jana, Mwenyekiti huyo wa AU amesema kuwa tatizo la ajira za upendeleo ni la muda mrefu katika AU, na hata kabla ya hapo katika OAU (Organisation of African Unity) uliotangulia AU.
“Afrika ni kubwa na ina watu wengi wenye uwezo. Chukueni bongo kali zaidi kutoka miongoni mwa vijana wa Afrika, na siyo kuajiri watu kwa sababu ni ndugu zenu ama jamaa zenu hata kama hawanazo sifa za kuajiriwa katika taasisi muhimu kama hii,” amesema kiongozi huyo wa AU katika mkutano uliofanyika kwenye Makao Makuu ya AU mjini Addis Ababa, Ethiopia.
AU inatakiwa kuwa na wafanyakazi 939 na mpaka sasa imeajiri 634.
JK pia ameutaka uongozi huo mpya chini ya Jean Ping wa Gabon kusimamia vizuri fedha za AU na kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika ipasavyo. Amesema kuwa raslimali zenyewe za AU ni kidogo na chache na kama zinatumika vibaya, umoja huo utashindwa kutekeleza mipango yake na kujiimarisha kama inavyotakiwa.
“Tujiepushe na matumizi mabaya ya fedha kidogo ambazo tunazipata. Hili nalo limekuwa linazungumzwa kwa chini chini na kwa muda mrefu katika umoja wetu.”
Na ili kuhakikisha kuwa fedha za AU zinatumika vizuri na ipasavyo, JK ameutaka uongozi huo mpya kuhakikisha kuwa mahesabu ya AU yanakaguliwa kila mwaka mwaka, na hata kila mara inapokuwa lazima kufanya hivyo.
Juu ya majukumu mengine ya makamishna hao, JK ametaka juhudi kubwa kufanywa katika kuendelea kuijenga AU.
“Hii ni taasisi changa mno. Ni kweli kuwa viungo vyake vingi vimeundwa na kukamilika, lakini ukweli ni kwamba bado taasisi yenyewe ni changa na hivyo inahitajika juhudi kubwa zaidi kuweza kuiimarisha.”
AU ilianzishwa rasmi Julai 2002 kuchukua nafasi ya OAU. Amewaambia makamishna hao kuwa wao ndiyo bongo za Afrika na kuwa kwa pamoja wanaunda kundi la watu wanaofikiria kwa niaba ya Afrika (think tank), na hivyo lazima watumie uwezo wao katika kulisaidia Bara la Afrika kupiga hatua.
“Nyie ndiyo think tank wa Bara letu. Mmechaguliwa kwa sababu ya uwezo wetu mkubwa na kwa sababu ya nguvu yenu ya kuweza kupanga na kuleta maendeleo ya Bara letu hili. Lisaidieni,” amesema JK.
Amehimiza ufanisi, uadilifu na ushirikiano katika utendaji kazi na kusisitiza, “kama mnavyojua AU ni taasisi ya kisiasa, na kimsingi, siasa ni kazi ya ushirikiano na hivyo lazima mfanye kazi kwa ushirikiano, miongoni mwenu nyie, kati yenu na mwenyekiti wetu, na kati yenu na wafanyakazi wengine wa AU.”
Amewataka kujenga mahusiano mazuri na pia kujiheshimu katika utendaji kazi, akisema kuwa wao ni viongozi na moja ya wajibu wa kiongozi ni kujiheshimu. “Najua hili mnalijua fika, lakini kwa kuwakumbusha tu ni kwamba baada ya kuingia katika shughuli hii, baadhi ya mambo yenu yalikuwa mambo binafsi, sasa yanaweza wazi, hadharani.”
Baada ya kuwa amemaliza kukutana na makamishna, Mwenyekiti huyo wa AU amekutana na wafanyakazi wote wa AU kwenye Ukumbi wa Congo kwenye makao Makuu ya AU.
JK amewataka wafanyakazi hao kuunga mkono uongozi mpya wa Jean Ping kama walivyounga mkono uongozi uliopita wa Alpha Omar Konare wa Mali ambaye jana alikabidhi uongozi kwa Ping.
Amewashukuru wafanyakazi hao kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya katika kuijenga AU na kusisitiza kuwa mafanikio yote ambayo yamepatikana mpaka sasa yametokana na bidii, juhudi na jasho lao.
“Tusingeweza kuwa tumepata mafaniko tuliyopakata mpaka sasa, yaani tokea Julai 2002 tulipoanza hadi sasa. Mmefanya kazi nzuri kama watumishi wa kimataifa ndani ya Bara lenu wenyewe. Tafadhali endeleeni na moyo huo wa kuijenga Afrika.”
Akiwahimiza kuongeza bidii, JK amemalizia kwa kuwatolea kauli mbinu maarufu ambayo aliianzisha kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania wakati akiwa waziri wa wizara hiyo ya “Better than yesterday, less than tomorrow.”

Connecticut center Hasheem Thabeet plans to return to school for his junior season instead of entering the NBA draft.


The 7-foot-3 native of Dar es Salaam, Tanzania, was projected as a first-round pick in the draft.
Thabeet averaged more than 10 points and almost eight rebounds a game as a sophomore, and ranked third in the nation with 147 blocked shots. He was the Big East's defensive player of the year, helping UConn to a 24-9 record.


"As a team, we took a step in the right direction this year, but I look forward to us working together to win a Big East Championship and making a run at a national championship," Thabeet said in a statement released Sunday by UConn. "I really enjoy being here, getting a great education and spending time with my friends and teammates."


Thabeet, 21, has been playing organized basketball for fewer than six years.


"Hasheem has made as much progress as any player I have coached in my 36 years and if he continues that incredible progress, he will help us take the next step as a team and help himself become one of the best players in college basketball," UConn coach Jim Calhoun said.


full story click here

Mtoto Ramadhani, siku alipokutwa na kichwa, alimpa onyo mwandishi wetu kuwa naye hana muda mrefu wa kuishi)


“Wakati mwanangu anaendelea kucheza nje niliamua kuweka neti kitandani ili aje alale na kabla sijamaliza kutandika akaja baba yake akaniuliza alipo mtoto nilimfahamisha kuwa anacheza nje ambapo alikwenda kumuangalia, baada ya muda alirudi ndani akaniambia hajamuona.


“Hata hivyo, shangazi yangu aitwae Furaha Majani ambaye tulikua naye ndani alitoka nje kumtafuta bila mafanikio hali hiyo ilinipa wasiwasi na kunifanya nitoke nje kumuangalia lakini nami sikumuona.

soma zaidi kwa kubofya hapa





samweli
mdau meshack mfugale (kulia) akikabidhi dola 500 kwa emmanuel nkya kama mchango wake kwa mtoto samwel nkya (pichani juu) anayehitaji kwenda india kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji na matibabu katika uso wake ambao umeharibika. wanaoshuhudia ni wajumbe wa kamati ya kumsaidia mtoto samweli akatibiwe.


mdau mfugale anayefanya kazi darfur, sudan, ni mmoja ya wadau wengi waliojitokeza kumchaangia mtoto huyu kiasi sasa mchango umetimia dola 9,500 na zimebakia dola 2,500 tu kukamilisha matakwa yote ikiwa ni pamoja na tiketi ya ndege mtoto samwel na baba yake, matibabu na malazi hospitali mwezi mmoja.


Baba wa mtoto huyo, emmanuel nkya, ametoa shukrani sana kwa wasamaria wema wote waliochangia kwa hali na mali. safari ya kwenda india inatarajiwa kufanyika wakati wowote kuanzia sasa.
Kwa habari kamili bofya hapa


no image

CHAMA CHA MAPINDUZI

Shina la Reading

MKUTANO WA PILI WA SHINA LA READING

Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Wanachama Wote - C C M - Reading
Wakereketwa Wote - C C M - Reading
Wapenzi Na Wana-Mapinduzi Wote wa Reading
Tarehe: 04/05/2008 Saa: 08:00 Mchana - Saa 12:00 Jioni

WAPI:
UKUMBI WA: 79 (Kijiweni)
79 LONDON ROAD
READING
RG1 5BY

Watanzania ambao wangependa kujiandikisha, mnaombwa kuleta picha zenu za passport size mbili na paundi kumi na tano (paundi tatu kwa kadi, halafu paundi kumi na mbili kwa ada ya uanachama ya mwaka mzima).

Kwa ufafanuzi zaidi, tafadhali wasiliana na:

MAIRA MIGIRE – 07799212095
Katibu wa CCM Shina la Reading

Wote Mnakaribishwa – Kutakuwa na Vinywaji, Nyama choma na Muziki Baada ya Shughuli Zote.
Kiingilio – BURE!!!-- Best RegardsSoames PharesReadingUnited Kingdom

MDAU,

ENDAPO KAMA UNA GARI AINA YA MERCEDES BENZ , RANGI NYEUSI AMA NAVY BLUE MUUNDO WA E200, E250, E300 NA E500 NA IKO KWENYE HALI NZURI WASILIANA NA KITENGO CHA SULLIVAN WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA AMBACHO KINAKUSUDIA KUKODISHA MAGARI AINA YA MERCEDES BENZ SALOON KWA MUDA WA SIKU 10 KUANZIA MEI 28, 2008 HAD JUNI 6, 2008 KWA AJILI YA MKUTANO WA SULLIVAN UTAOFANYIKA ARUSHA KATI YA JUNI 2 HADI 6. 2008.

PELEKA GARI LAKO KWA UKAGUZI GOVERNMENT TRANSPORT AGENCY (GTA) PALE BOHARI KUU BARABARA YA NYERERE KUANZIA MEI 3, 2008 KATI YA SAA MBILI UNUSU ASUBUHI NA SAA TISA UNUSU ALASIRI.

KITENGO CHA SULLIVAN TANZANIA KITAKODISHA GARI LAKO KWA GHARAMA ISIYOZIDI SHILINGI 150,000/- KWA SIKU.

KWA TAARIFA ZAIDI WASILIANA NA KITENGO CHA SULLIVAN SIMU NAMBA

022 2111906/11,

2110185,

2128336,

AMA

0787 245424,

0715 599 299

KWA HABARI ZAIDI JUU YA MKUTANO WA SULLIVAN

http://www.thesullivansummit.go.tz/


BENDI YA MUZIKI WA DANSI YA AFRICAN STARS “TWANGA PEPETA INTERNATIONAL” INATARAJIWA KUONDOKA MJINI DAR ES SALAAM LEO JUMANNE USIKU KWA “ SHUTTLE” KWENDA MJINI NAIROBI, KENYA KWA AJILI YA KUTUMBUIZA MAONYESHO MANNE NCHINI HUMO.

MAANDALIZI YOTE KWA AJILI YA SAFARI HIYO YAMEKWISHA KAMILIKA NA BENDI IPO KAMILIFU KWA AJILI YA KUKONGA NYOYO ZA MASHABIKI WA HUKO.

ZIARA YA TWANGA PEPETA NCHINI KENYA IMETOKANA NA MWALIKO MAALUM KUTOKA KWA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA KITAIFA CHA WAFANYAKAZI NCHINI KENYA(COTU) MR FRANSIS ATWOLI NA PIA ROTAMU PROMOTIONS YA NCHINI HUMO NA ZIARA HIYO ITAFAHAMIKA KWA JINA LA “AMANI TOUR” LENGO L IKIWA NI KUSAMBAZA UJUMBE WA AMANI NCHINI KENYA KWA NJIA YA MUZIKI KUFUATIA MACHAFUKO NA VURUGU KUBWA ZA KISIASA ZILIZOKUWA ZIMEIKUMBA NCHI HIYO HIVI KARIBUNI MARA BAADA YA UCHAGUZI MKUU.

BENDI INATARAJIWA KUONDOKA NA WANAMUZIKI WAKE WOTE NYOTA WAKIONGOZWA NA KIONGOZI MKUU KHAMIS AMIGOLAS NA KIONGOZI MSAIDIZI LUIZER MBUTU CHINI YA MENEJA WAO ABOU SEMHANDO.

BENDI INATARAJIWA KUREJEA NCHINI WIKI IJAYO JUMATATU YA TAREHE 5-05-08 ILI KUENDELEA NA RATIBA YAKE YA KILA WIKIENDI JIJINI DAR ES SALAAM.

ITAPOKUWA HUKO ONYESHO LA KWANZA LITAFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA UHURU PARK KATIKA KILELE CHA SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI (MEI MOSI) KUANZIA SAA NNE ASUBUHI AMBAPO MGENI RASMI ANATARAJIWA KUWA RAIS WA JAMUHURI YA KENYA MHESHIMIWA MWAI KIBAKI.

ONYESHO LA PILI LITAFANYIKA SIKU YA IJUMAA TAREHE 02-05-08 KUANZIA SAA TATU USIKU KATIKA KLABU YA USIKU YA NEW DEEP WEST RESORT ILIYOPO JIJINI NAIROBI, ONYESHO LA TATU LITAFANYIKA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 03-05-08 KUANZIA SAA MBILI USIKU KATIKA KLABU YA CASAURINA (ZAMANI ILIKUWA IKIJULIKANA KAMA COCO BEACH), NA ONYESHO LA NNE NA LA MWISHO AMBALO NI MAALUM KWA AJILI YA FAMILIA LITAFANYIKA KATIKA UKUMBI WA NEW DEEP WEST RESORT JUMAPILI, MEI 4 KUANZIA SAA KUMI JIONI HAPO HAPO MJINI NAIROBI.

HII ITAKUWA NI MARA YA PILI KWA BENDI YA AFRICAN STARS “ TWANGA PEPETA” KUZURU NCHINI KENYA KWA MUALIKO BAADA YA MWAKA JANA MNAMO MWEZI WA SITA KUZURU CHINI HUMO KWA MAONYESHO KATIKA MIJI YA NAIROBI NA MOMBASA.

BARAKA MSIILWA
MWENYEKITI
AFRICAN STARS ENTERTAINMENT (ASET)
Mdau John Kitime leo anatuamsha na 'Fimbo lugoda' Orchestra Tancut Almasi: Toka kushoto Buhero Bakari (Trumpet),Kyanga Songa, Kasaloo Kyanga, Kabeya Badu, Kalala Mbwebwe,Abdul Mngatwa,Akuliake Salehe (King Maluu)

Ndugu Wadau,
Chuo cha LONDON SCHOOL OF COMMERCE (associate college of university of wales) kinatangaza usajili maalumu wa wanafunzi wapya wa mwaka huu wa masomo 2008/9 unaoanza mwezi wa sita (June) 2008.
Kwa taarifa zaidi na kozi mbalimbali wanazotoa tembelea tovuti yake www.lsclondon.co.uk .Kuna punguzo maalumu la Ada kutoka £6450 mpaka £3950 kwa mwaka wa masomo huu kwa wanafunzi wa kitanzania watakaopitia kwangu kuomba na kukubaliwa masomo yao hapa chuoni, punguzo hili maalumu utalipata kwa kuwasiliana nami ili nikuwakilishe hapo chuoni.
Naomba wanafunzi wenye interest na kusoma chuoni hapa kwa kozi zilizotangazwa kwenye tovuti ya chuo tuwasiliane kwa namba yangu hii hapa +447506458289.... au email hii
ally.abdallah@lsclondon.co.uk
Natoa tahadhari kwamba Mimi ni wakala wa wanafunzi wa kitanzania ninayehusika na punguzo la bei tu.. Sihusiki kabisa na upatikanaji wa kibali cha kuingilia Nchini (visa), kwahiyo naomba nisiulizwe maswali kuhusu swala hilo,chuo kitakamilisha kila taratibu za mwanafunzi aliyekubaliwa masomo na kupata nafasi chuoni ili eweze kupata visa..
kwa maelezo zaidi kuhusu upatikanaji wa visa za uingereza bofya hapa http://www.ukvisas.gov.uk/en/
Ni matarajio yangu, kila mwenye kutaka kupata habari zaidi za kusoma chuoni hapa na punguzo hili la bei atapitia tovuti ya chuo (www.lsclondon.co.uk) kwanza na kumaliza mushkeli aliokuwa nao, kisha kuwasiliana na mimi ili kupata punguzo hilo la ada.
NB: unapowasiliana nami tafadhali nukuu jina la chuo kwanza LSC na wai umeona tangazo hili halaf endelea na ujumbe, maswali yako nk.
TAHADHARI: Sitopokea malipo kutoka kwa mwanafunzi yeyote yule,ada na malipo mengine yanafanyika katika kitengo husika chuoni, ili upate punguzo ni kuwasiliana na mimi nikupe taratibu husika (Bure).
Asanteni

,


TUMIA VASELINE kwa kuwa Ngozi yako ni Mali


Ngozi inatakiwa tuitunze na kuikinga na madhara ya mazingira kama vile TUSIACHE NGOZI KUWA KAVU, KUWA NA MADOA YANAYOSABABISHWA NA JUA AU UMRI, CHUNUSI AU VYAKULA MBALIMBALI.


Tuna mafuta mbalimbali ORIGINAL ya kulainisha ngozi na mojawapo ikiwa ni Vaseline.


Angalia site hii http://www.vaseline.com/index.aspx kuhusu Vaseline na umuhimu wake


VASELINE inatumika kwa NGOZI za kila RANGI.


Fika dukani ujipatie mojawapo kulingana na mahitaji ya ngozi yako


Angalia video hii kuhusu Vaseline



Vaseline na mafuta mengine yanapatikana Sinza hapa Dar.


Kwa maelezo zaidi wasiliana na

Rose
0784-521171

au tuma maswali yako
no image
Wanafunzi wote ambao walisoma Ljs Morogoro Mnaalikwa kuudhuria katika kikao muhimu cha kujadili changamoto mbalimbali juu ya umoja wetu.
MAHARI: ROSE GARDEN
DAR ES SALAAM
MUDA:SAA TISA MCHANA
TAREHE: 1 MAY 2008
Watakaofika watapata kuonana na marafiki ambao hawakutegemea kuwaona tena na kukumbushana maisha ya Seminary

-- MR.Godwill Philip Matayi
Kamati ya maandalizi

NAPENDA KUCHUKUA NAFASI HII KUWATOA HOFU WADAU NILIOWATUMIA LINK INAYOELEZA UWEZEKANO WA MDAU KUWA NA JINA LAKE KAMA HIVYO HAPO JUU KWENYE UKURASA WAKE WA WAVUTI.
HAYA NI MANJOMBWENJOMBWE KAMA YA GOOGLE AMBAO KATIKA KUENDELEZA LIBENEKE LAO WAMEAMUA KUFANYA HIVYO. KWA HIYO MDAU ULIYEPATA MWALIKO WANGU WALA USIKONDE. NI VIJIMAMBO VYA PIMPYMAIL TU NA SIO VIRUSI. KUNRADHI KWA YEYOTE NILIYEMKWAZA
MICHUZI

The African-American celebrity community came out in full support of Africa Saturday, April 19.


Actress Vivica A. Fox along with the Leon H. Sullivan Foundation hosted the Girlfriends Brunch for Africa, at her Los Angeles home to join the conversation on Africa.


The brunch was geared to garner celebrity support and encourage participation in the upcoming Leon Sullivan Summit being held in Arusha, Tanzania June 2-6th.


Attendees included Essence Atkins (Deliver us from Eva, Half & Half), producer Tracey Edmonds, Jill Marie Jones (Girlfriends),Tamala Jones (Daddy Day Camp), Regina King (24, Enemy of the State, Miss Congeniality 2, Ray, Legally Blonde 2, Jerry Maguire), Lela Rochon (Waiting to Exhale), Raven Symone (That’s So Raven), Terri Vaughn (Steve Harvey Show) and Kim Whitley (College Road Trip) among others.


Following the brunch, a presentation was given by Hope Masters, President & CEO of the Leon H. Sullivan Foundation and Summit convener, which included a personal invitation for each guest to attend the Summit.


In addition, several important issues were discussed, including organizing a celebrity contingency to visit Africa to participate in some of the projects established by the Foundation.


“The support and warmth we received from the African American Hollywood community was overwhelming,” stated Hope Masters.


“Everyone came out in support of Vivica and to support our cause. This brunch was just the beginning of what’s to come in getting our community to play an active role in Africa. I look forward to working with these beautiful women during this year’s Summit and in the future.”


The Leon H. Sullivan Foundation is an organization dedicated to leveraging the commitments and resources of the United States and the African Diaspora to promote positive change on the continent of Africa.


Their 2008 Summit will be held in Arusha, Tanzania June 2-8, 2008.


With a focus on issues such as the environment, infrastructure, tourism, education, health and investment, this year’s Summit also includes humanitarian missions such as a mosquito netting project as well as donating books and medical supplies to Africa.


Nichet Smith

Director, Public Relations

Leon H. Sullivan Foundation

1800 K. Street

NW Suite 1021

Washington, DC

20006202.

736.2239

phone202.

736.2226 fax


Sullivan Summit VIII


"The Summit of A Lifetime"

June 2-6,2008

Arusha,

Tanzania


REGISTER NOW ONLINE!!


www.thesullivanfoundation.org/summit http://www.youtube.com/sullivanfoundation

KUNDI la mwanamuziki Bozi Boziana kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo linatarajia kusindikiza uzinduzi wa albamu ya Impact ya bendi ya Akudo Impact.


Msemaji wa Akudo amesema leo kuwa kundi la Bozi Boziana linatarajia kuwasili Mei 13 likiwa na wasanii takribani 17.


Uzinduzi wa albamu hiyo umepangwa kufanyika Mei 16 kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee ambao utafanyika kwa ushirikiano wa Kampuni za Qssp Group Ltd na NY Production.


Mratibu wa tamasha hilo Bahati Singh alisema : " Akudo wao wako kwa ajili ya vijana, lakini tukaona ni heri tuwape burudani ya watu wa aina mbalimbali na ndio maana tukaamua kuwaleta Bozi Boziana kwa ajili ya watu wazima na Jahazi Modern Taarabu kwa wapenzi wa muziki wa mwambao," alisema.


Habari zaidi na picha nenda: lukwangule.blogspot.com
no image
KAKA MICHUZI,
TWAREJEA KATIKA SWALI LAKO KWA WATU WAISHIO UGHAIBUNI.TUNASHINDWA KUJIANDIKISHA KTK BALOZI ZETU KWA MAMBO MENGI NA MENGINEYO NI KAMA IFUATAYO;-
1)KATIKA SHEREHE ZA MUUNGANO 26/04/08,TUMEALIKWA KWA KISHINDO KATIKA KUSHEREHEKEA SIKUKUU HIYO NAKUJULISHWA KWAMBA MGENI RASMI ATAKUWA BALOZI WETU KUTOKA SWEDEN.
KWA SISI TUISHIO MBALI NA OSLO,TULISAFIRI TOKA MAKWETU KWENDA JAPO KUMUONA HUYO BALOZI WETU AMBAYE ANGETUPA MACHACHE KUHUSU NCHI YETU,LAKINI KILICHOTOKEA HUKO NI KWAMBA BALOZI HAJAONEKANA VIONGOZI WA CHAMA CHA WATANZANIA WAMESHINDWA KUTUPA JIBU KAMILI KUHUSU KUTOKUONEKANA KWA BALOZI WETU AMBAYE NDIYE ALIYEKUWA MGENI RASMI.WALA MTU YOYOTE KUTOKA UBALOZINI HAKUONEKANA.
KWA HAYO MACHACHE KAKA MICHUZI TUNAKUOMBA UWAFIKISHIE UJUMBE HUU HAO WAHUSIKA WA UBALOZI.
NA MPAKA HAPO UTATAMBUA NI KWANINI WATANZANIA WAISHIO UGAIBUNI HAWAJISIKII KWENDA KUJIANDIKISHA KWA MAUDHI KAMA HAYA AMBAYO YANATUKOSTI MUDA WETU NA FEZA ZETU.
2)SHUKRANI KWA CHAMA CHA WATANZANIA OSLO KWA PART NZURI NA CHAKULA KIZURI.NI MATUMAINI YETU UJUMBE HUU UTAUWEKA HEWANI KWANI MJUMBE HAUWAWI.
WAKEREKETWA NORWAY,
Ã…LESUND



Habari za leo wadau,
Ule wakati tulio usubiria sasa umefika, Website ya pekee itakayo jishughulishaktk kuutangaza muziki wa Tanzania ipo jikoni na ina karibia kuiva.

Unataka kusikiliza muziki wa nyumbani? Basi watembelee wajuzi wa fani hiikupitia
www.mkmusicgalaxy.com kwa miziki mipya na ya kizamani uburudike na roho yako.

Kumbuka, hawa ndio walewale wakiokupaga raha siku za nyuma na mambo ya mahusiano.com. sasa wamekuja upya!!

Nawatakia siku njema.


Kind Regards,

Support Department

MK MUSIC GALAXY - Exploring the Tanzanian Music.

Part of MK GROUP OF COMPANIES (T) LTD - http://www.mkgroupltd.com
Tel: +44 - 752 - 792 - 9234
Kijana Ramadhani Mussa (12) ambaye jana alikamatwa na kichwa cha mtoto mwenzie na kuanza kukinyoya damu hadharani pale kwenye lango la Hosptali ya Taifa Muhimbili, alishawahi kukutwa kwenye makanisa kadhaa ya jijini Dar es salaam akidai kudondoka na ungo na kisha kuombewa na wachungaji wa makanisa hayo, lakini mara ya mwisho alionekana ni kijana tapeli tu au wachungaji waliokuwa wakimuombea walikuwa wanafanya usanii kuvutia 'wauimini'!

Awali mtoto huyu inadaiwa alikutwa usiku wa manane kwenye Kanisa la Kilutheran pale Manzese na kuombewa na Mchungaji Jonathan wa Kanisa hilo baada ya kudai kuwa amedondoshwa na wachawi wakiwa kwenye ungo, ingawa waumini wengine walimuona kijana huyo kama mchawi na kutaka kumpiga.


Baadae inadaiwa alipelekwa Hospitali ya Mwananyamala ambako nako alitoweka kimiujiza, kabla ya kukutwa kwenye kanisa lingine Tabata na hatimaye Mikocheni kwa Mchungaji Rwakatare ambako ndiko alipoombewa akiwa na mwenzake kwa muda kabla ya kuambiwa kuwa ni 'matapeli' kwani hizo ndizo zao kujifanya wamedondoka kwenye ungo na kuibukia Makanisani ili kujipatia pesa!


Akiongea na kituo cha ITV jana, Mchungaji Rwakatare, ambaye pia ni Mbunge wa CCM wa kuteuliwa, alisema "Mungu amejitetea mwenyewe" kwa kuonesha kuwa walichokuwa wanakisema kuwa watoto hao walikuwa na mapepo hawakuwa wanaongopa.


"Laiti kama wangewaachia wawaombee, yule mtoto asingekufa wala yasingetokea yaliyotokea, lakini kwa sababu kuna watu wanajaribu kuwa kama Mungu, ndiyo maana haya yote yanatokea!
"Wamuache Mungu awe Mungu", alisema Mchungaji Rwakatare na katika hili inaoenekana mtumishi huyu wa Bwana amejipatia 'tano' zingine!
Mwenyekiti wa AU Jk akimpa tano mwenyekiti wa kamisheni ya umoja wa afrika (AU) aliyemaliza muda wake profesa alpha oumar konare ambaye leo kakabidhi madaraka hayo kwa mh. jean ping huko addis ababa ethiopia
JK: Bei hizi za mafuta zinatuua
*Aitaka Afrika kuongeza sauti yake kuhusu bei za mafuta na chakula
Na Freddy Maro
Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Mrisho Kikwete amelionya Bara la Afrika kuamka na kuanza kutafuta njia za kukabiliana na tatizo la bei kubwa za chakula na mafuta duniani.
Akizungumza leo katika sherehe ya makabidhiano ya uongozi wa Kamisheni ya AU kwenye makao makuu ya AU mjini Addis Ababa, Ethiopia, JK amesema kuwa bei hizo ndiyo changamoto mpya na kubwa zaidi kwa wakati huu ya Afrika na uongozi mpya wa Kamisheni ya AU.
Katika makabidhiano hayo, Mwenyekiti wa Kamisheni iliyomaliza muda wake, Alpha Omar Konare wa Mali amekabidhi madaraka kwa Mwenyekiti mpya, Jean Ping wa Gabon.
Kabla ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kamisheni ya AU, Konare alikuwa Rais wa Mali wakati Ping alikuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Gabon.
Rais Kikwete ambaye alikuwa Mwenyekiti na msimamizi mkuu wa sherehe hiyo, amewaambia mamia ya watu waliohudhuria sherehe hizo: “Kamisheni mpya inaingia katika madaraka wakati Afrika inakabiliwa na changamoto mbili kubwa sana na mpya. Changamoto hizo ni bei kubwa vya chakula na bei kubwa ya mafuta.”
Ameongeza: “ Kama changamoto hizo hazikukabiliwa haraka na ipasavyo zitamaliza kabisa chumi nyingi za Afrika, ambazo kwa bahati nzuri zimekua zinakua vizuri katika miaka michache iliyopita.”
JK amesema kuwa iko hatari kubwa kweli kweli kuwa mafanikio yote ya kiuchumi ambayo yamepatikana katika Afrika yatamezwa na bei hizo kubwa za chakula na mafuta.
“Katika hili, sauti ya Afrika inatakiwa kusikika na uongozi katika jambo hili unatakiwa kuonekana dhahiri,” amesema JK.
Mbali na changamoto hiyo ya bei za chakula na mafuta, Rais Kikwete pia aliorodhesha changamoto nyingine zinazolikabili Bara hili kwa kadri uongozi wa Kamisheni unavyotoka mikononi mwa kundi moja kuingia kwa kundi jingine, kwa amani.
Changamoto nyingine ambazo zitaukabili uongozi huo mpya, kwa mujibu wa JK, ni migogoro katika Darfur, Chad, Jamhuri ya Afrika ya Kati, na Somalia.
“Pia hali za DRC, Burundi na Zimbabwe zinahitaji uangalizi wa karibu wa AU.”
JK pia ameutaka uongozi huyo mpya kuongoza mjadala kuhusu utekelezaji wa Azimio la Accra kuhusu mwelekeo wa baadaye wa AU na mapendekezo ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja ya Afrika na pia kuongoza mjadala kuhusu tathmini ambayo imefanywa kuhusu AU yenyewe.
Hata hivyo, JK ameongeza: “Pamoja na kwamba changamoto ni kubwa na ni nyingi, lakini sina shaka kwamba taasisi yetu iko katika mikono yenye uwezo na yenye uzoefu ya Jean Ping, Makamu wake Erastus Mweche na makamishna wengine wapya.”
Ameongeza kuwaambia viongozi hao wapya“ Hili linanifanya niwe na imani. Kwa niaba ya Serikali na Watu wa Afrika nawaombeni kusimama kupambana na changamoto hizi.
"Najua mtaifanya kazi hiyo, kwa ufanisi.” Rais Kikwete pia ameelezea baadhi ya mafanikio ya AU katika kipindi kifupi tokea kuanzishwa kwake kutoka taasisi ya zamani ya Organisation of African Unity (OAU).
“AU sasa imejijenga kama taasisi ya kikanda inayoaminika na inayotegemewa kwenye uwanja wa kimataifa. Matokeo yake ni kwamba AU imejenga ushirikiano wa nguvu na Umoja wa Ulaya, Japan, China, Korea Kusini, Nchi za Marekani Kusini na hivi majuzi na India. Tunatarajia kuwa uongozi mpya utaimarisha mahusiano hayo na kujenga mpya.”
JK pia amemwagia sifa kemkem Konare kwa uongozi wake wa AU. “Profesa Alpha Omar Konare ni mtu wa mawazo mengi na makubwa. Visheni ya AU ya mwaka 2015, kimsingi, ni matunda ya ubongo wake; matokeo ya bongo yake inayochemka na visheni.
"Ndani ya moyo wa Afrika, kuna sehemu maalum ya Afrika, na watu wake. Ni Mwafrika kweli kweli kwenye sifa ambazo ni ngumu kuzielezea kwa ufasaha wa kweli kweli.”
Ameongeza JK: “Profesa Alpha Konare ni mtoto wa kweli kweli wa udongo wa Afrika ambaye ameitumia taasisi yetu vizuri sana na kwa ari, moyo mkubwa wa kujitolea na imani kubwa. Profesa Konare siku hizo amekuwa chanzo cha ari kwetu sote.”


vifaa vilivyoagizwa kwa bei mbaya na serikali kwa ajili ya mazoezi ya viungo hasa kwa maafisa wa taasisi mbalimbali zinakula vumbi uwanja wa ndani wa neshno na haonekani mtu akila tizi hata siku moja mahali hapo...

Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akisalimiana na wauguzi wanafunzi wakati alipotembelea hospiali ya Mvumi wilayani Chamwino na kuzungumza na waganga na wauguzi na kutoa msaada kwa wagonjwa. Shoto ni askofu wa Dayosisi ya Kati (DCT), Godfrey Mhogola.

Hamadi Billali wa Dar es salaam akipokea zawadi ya shilingi milioni tano alizojishindia kwenye wiki ya pili ya shindano la ‘Kili Time of Your Life’ kutoka kwa Meneja wa Mauzo wa TBL Kanda ya Dar es salaam, Consolata Adam mwishoni mwa wiki
no image
KAKA MICHUZI POLE NA KAZI YA KUTUELIMISHA SISI JAMII, NAOMBA KUWEKA HII MADA YA USAFIRI HEWANI ILI IWEZE KUJADILIWA NA WADAU KAMA INAWEZEKANA, HAPA MJINI MOSHI KUNA MATANGAZO YAMETAPAKAA KILA MAHALI KUWA IFIKAPO TAREHE MOJA MWEZI MEI NAULI YA DALADALA ITAPANDA KUTOKA SHILINGI 300/= YA SASA HADI KUFIKIA SHILINGI 450/= KITUO HADI KITUO.
JE ITAKUWAJE KWA WALE WAFANYAKAZI WA SERIKALI WANAOLIPWA KIMA CHA CHINI CHA SHILINGI 84,000/= BILA MAKATO (KODI NA KADHALIKA), NA ANA FAMILIA INAYOMTEGEMEA (CHAKULA,MALAZI, SHULE N.K),MWENYE NYUMBA ANASUBIRI KODI YAKE, KUFIKA KIBARUANI KWAKE INABIDI APANDE DALADALA MBILI, KWENDA NA KURUDI NI NNE, JE KWA MWENENDO HUU SERIKALI INAWAJALI RAIA WAKE MASKINI KWELI? HII KUPANDA KWA NAULI NI UAMUZI WA WAMILIKI WA DALADALA AU NI SERIKALI NA MAMLAKA HUSIKA? NINI KIFANYIKE ILI ANGALAU WANANCHI WAONE FAIDA YA SERIKALI YAO?

MDAU KCMC


no image
Tangazo la Msiba kwa wanafunzi wote wa Kazima Secondary school toka 1997 mpaka 2000
Kwa niaba ya familia ya marehemu ndugu yetu, kaka yetu, mwanafunzi mwenzetu enzi hizo za mwishoni mwa miaka ya 90 mpaka mwanzoni mwa mwaka 2000.
Nasikitika kutangaza kifo cha kaka yetu mpendwa HUSSEIN JUMA MATOVOLWA kilichotokea kwa ajali ya pikipiki.
Mazishi yamekwisha fanyika tarehe 27.04.2008.
Habari ziwafikie wanafunzi wote wa Kazima Secondary School na wale wote walio soma nae katika shule ya Msingi Itetemia Tabora, Na ndugu na jamaa wote walio kuwa wakimfahamu kaka Hussein mahali popote pale walipo watakaposoma Ujumbe huu!!
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!!
Ipyana Ambele
no image
Ero Mishuzi!
Saidia tasafali. Hii kitu nachengua mimi sana... iko hiine watu nyingeni nasema "anatikisa kibiriti" then ingine nasema "anatingisa kibiriti" wengine iko nasema " anatikisha kiberiti" na ingine "anatingisha kiberiti".
Naomba elekesa mimi ipi iko mahala yake
* Natangulisa sanks sangu
mdau Endulen

car for Sale


*2000 Blue Volkswagen


Only 50 miles. Only first gear and reverse ever used.


*Never driven hard.


*Original tyres.

*Original brakes.

*Original fuel and oil.

*Only 1 driver.


Owner wishing to sell due to employment lay-off.
Interested parties pse contact Mdau
no image
LEO WATANI WA JADI SIMBA NA YANGA WAMETOKA DROO YA 0-0 NESHNO KWENYE MMOJA WA MICHEZO SITA YA KUHITIMISHA LIGI KUU MWAKA HUU AMBAPO YANGA IMETWAA UBINGWA NA PRISONS YA MBEYA IMETWAA NAFASI YA PILI. WATOTO WA MJINI ASHANTI NA COASTAL UNION WAMESHUKA DARAJA.
no image
CLASS RE-UNION MOSHI TECHNICAL (1987)

Wengi wameomba kila mtu aliyekuwepo Moshi Tech mwaka 1987 ahusishwe, hata kama alikuwa kidato cha kwanza mwaka huo. Wengi wanaelekea kukubaliana na pendekezo hilo pia.

Naomba hata wale waliokua vidato vya chini (kidato cha 1 mpaka cha 3) watume majina yao kupitia:
betapromotions@gmail.com ili wapate taarifa zingine muhimu.
Tuendelee kuwajulisha pia wasiopitia mtandao mara kwa mara. Tunaendelea kupata majina na mapendekezo ya wale wanaotarajia kushiriki.

Ahsanteni sana!
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akichanganya michanga ya ardhi ya Zanzibar na Tanganyika wakati wa Muungano 1964 huku (kulia) aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Rashid Mfaume Kawawa akiangalia tukio hilo na nyuma (kushoto) aliyekuwa Rais wa Zanzibar Abeid Amani Karume akishuhudia tukio hilo.

Zaidi ya karne tunayoijua sisi nchi yetu ya Tanganyika ilipewa jina hilo, ambalo kwa lafdhi ya baadhi ya wazungumzao lugha ya Kiswahili Afrika Mashariki, maana yake ni "Changanyika". Je, aliyeipa jina hili la Kuchanganyika kabla ya tukio la hapo juu halijatokea, alikuwa na HIKMA yoyote?
Ahsante Kaka


Mhariri - Zenjydar Community Association

-- Zenjydar Community Association
Wachezaji wa Man u jana wliafanya bonge la vagi baada ya kukataa kutoka uwanjani mpira ulipoisha jana. Inaonyesha iliwauma vibaya sana kipigo cha jana mpaka wakashindwa kujibihev. kwa maelezo zaidi bofya hapa http://www.thesun.co.uk/sol/homepage/
sport/football/article1013041.ece
jfk akiwa na vijana jazz enzi hizo za miaka ya 80
jfk leo hii akiwa na njenje akiimba 'jojina'. huyu ndiye mdau anayetuletea zile za enzi hizo. pamoja na vijana jazz pia alikuwa na tancut almasi 'fimbo lugoda' ya iringa na hadi leo anaendeleza libeneke. pia alikuwa jaji wa bongo star search na pia ni mwenyekiti wa kamati ya hakimiliki. hivi karibuni anatarajia kuanzisha globu ya mambo ya muziki wa bongo. kaeni mkao wa kula...
no image
Kaka Michuzi,
Habari za kazi tunakushukuru kwa kutupa habari za nyumbani sisi tulio mbali na nyumbani. Naomba uiweke hii hewani.
Namtafuta rafiki yangu anaitwa JOYCE KIBOMA nilisoma nae kiluvya secondary tumepotezana tangu tulipomaliza shule.
Pia kwa wote waliosoma kiluvya secondary mail yangu ni jannetjj@yahoo.com
asante
Mdau Texas