In order to view this object you need Flash Player 9+ support!

Get Adobe Flash player
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.










  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com












Archive for May 2009

dogo wa uswazi leo


dse


nizar khalfani kufanya majaribio canada, sio UK

Nizar Khalfani (shoto mbele) akiwa na kikosi cha Taifa Stars


HIVI karibuni uongozi wa timu ya soka ya Moro United ulitoa taarifajuu ya kiungo wake wa kimataifa, Nizar Khalfan kutakiwa England kwamajaribio ya kucheza soka ya kulipwa katika timu ya Ligi Kuu ya huko,Tottenham Hotspur `Spurs’.

Baada ya Bodi ya Wakurugenzi kujadili ombi hilo na baadayekumshirikisha mchezaji husika, ilionekana kuwa ni heshima ya pekee,lakini kutokana na mazingira ya soka yetu, mchezaji huyo anahitajimaandalizi ya dhati kuweza kuingia katika ushindani wa kuwania nafasikatika klabu kubwa kama Spurs.

Hili lilikwenda sambamba na ujio wa mwaliko mwingine kutoka klabu yaVANCOUVER WHITECAPS FOOTBALL CLUB ya Canada iliyozuru nchini mapemamwaka huu na kuvutiwa na uwezo wa Nizar baada ya kumuona akiichezeatimu ya taifa `Taifa Stars’.

Kwa kuona Vancouver inaweza kuwa mahali pazuri pa kuanzia kucheza sokaya kisasa, Nizar ameridhia kwenda Canada kwa majaribio ya wiki mbilikuanzia Juni 8, mwaka huu. Vancouver itabeba gharama zote za Nizarwakati wa majaribio ngazi.

Mkurugenzi Mkuu, Azim Dewji ameuzungumzia uamuzi huo kwa kusema: “Kwakuangalia hali halisi, Nizar anaweza kupata nafasi kwa urahisiVancouver kuliko Tottenham, hivyo tumekubaliana akaanzie Canada ambakoatapata mwanga zaidi wa soka.

“Na kwa kuwa umri wake bado ni mdogo (miaka 21), bado atakuwa nanafasi ya kujaribiwa katika klabu nyingine kubwa za Ulaya, lakinibaada ya kuwa ameshaivishwa Vancouver. Bado tuna mawasiliano na Spursna Moro United itaendelea kushirikiana nao.

“Kwa kuwa hii ni changamoto kwetu, tunarudia kusema sasa ni wakati waMoro United kuzama katika soka ya vijana. Mtazamo wetu utaanzia katikakikosi cha msimu ujao wa Ligi Kuu.”


Naye Nizar, alikiri kuwapo kwa makubaliano hayo, huku akisisitizakuwa, anaamini njia itakuwa nyeupe kwake kama ataanzia Vancouverkuliko Spurs.

“Hata mimi mwenyewe nadhani Vancouver nitafanikiwa. Waliniona hapanami nimeona uwezo wao, napata faraja kwamba inawezekana. Lakiniieleweke nako nitapita, kiu yangu ni kufika mbali kisoka, hasa kuchezakatika moja ya ligi kubwa za Ulaya.”

Nizar anatarajiwa kuondoka wakati wowote wiki hii, baada ya kupataviza ya kuingia Canada tayari kwa majaribio kuanzia Juni 8.

Uongozi wa Moro United unamtakia kila la kheri Nizar, kwani mafanikiohayatakuwa ya klabu pekee, bali hata kwa Taifa Stars.


siku ya kutotumia tumbaku duniani yaadhimishwa rombo

wananchi wakiwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali kuunga juhuhudi za kupiga vita matumizi ya tumbaku duniani katika sherehe zilizofanyika jana kitaifa eneo la Horiri – Rombo mkoani Kilimanjaro mpakani mwa Kenya na Tanzania.
wanafunzi wa shule mbalimbali wakiwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali kuunga juhuhudi za kupiga vita matumizi ya tumbaku duniani katika sherehe zilizofanyika jana kitaifa eneo la Horiri – Rombo mkoani Kilimanjaro mpakani mwa Kenya na Tanzania.

Mwanafunzi wa shule ya msingi Gunule ambayo iko Horiri wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro Twaha Bakari akiwa amebeba bango lenye ujumbe wa kupiga vita matumizi ya tumbaku katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kuttotumia tumbaku duniani

wahudhuriaji kwenye sherehe hizo
Baadhi ya wananchi waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kutotumia tumbaku duniani wakifuatilia kwa makini ngoma na michezo mbalimbali iliyokuwa ikionyeshwa katika viwanja vya Horiri wilayani Rombo –Kilimanjaro.






update ya ajali ya meli zenji

Meli ya MV Fatih ikiwa imezama katika eneo la Bandari ya Malindi ndani yake ikiwa na abiria wanaokisiwa kuwa zaidi ya 100. Abiria 27 walikuwa wameokolewa na maiti watatu tu ndio waliopatikana. Meli hiyo iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam ilikuwa imebeba abiria pamoja na shehena ya mizigo mbalimbali. Picha na mdau Mwajuma Juma - Zanzibar.
Na Mwajuma Juma, Zanzibar
WATU watatu wamekufa maji na wengine zaidi wanahofiwa kufa katika ajali ya meli ya abiria na Mizigo ya MV Fatih Zanzibar iliyopinduka na kuzama baharini, muda mfupi baada ya kuwasili katika Bandari ya Malindi ikitokea jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Mgharibi Unguja Bw. Bakar Khatib Shaaban, alisema jana kwamba ajali hiyo ilitokea saa 3:00 usiku na tayari baadhi ya maiti zimeanza kuopolewa.
Alisema kwamba meli hiyo ilikuwa na abiria 25 na mabaharia 13 lakini alisema takwimu hizo zinaonekana ni za uongo kwa vile inadaiwa kuwa meli hiyo imebeba watu kupita kiwango chake.
Kamanda huyo alisema kwamba hadi jana mchana maiti za watu watatu tu ndizo zilizoopolewa ikiwemo ya mtoto na mwanamke mmoja na kwamba watu 27 waliokolewa.
Aliwataja baadhi ya watu waliokolewa akiwemo Nahodha wa chombo hicho Ussi Ali, Maulid Abdallah, Zaidba Ali Khatib, Omar Ramadhan Mohammed, Haruna Omar, Kitiba Mussa, Halima Mussa, Hawa Juma Saleh, Sharif Hamad, Omar Khamis na Machano Mkui.
Hata hivyo alisema kuwa watu wengine majina yao bado hayajapatikana lakini walikimbizwa Hospitali matibabu.
Alieleza kuwa chanzo cha tukio hilo bado kinaendelea kufanyiwa uchunguzi lakini wanawasiwasi kwamba meli hiyo ilipinduka, baada ya kuzidiwa na mzigo upande mmoja, kwa vile ilikuwa imebeba shehena za mbao, gari moja trekta na vyakula.
Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Mustafa Aboud Jume alisema kwamba waokoaji 30 wakiwemo wazamiaji kutoka Kikosi cha KMKM walianza zoezi hilo saa 9:00 usiku juzi kwa kushirikiana na wazamiaji mbali mbali.
Hata hivyo alisema kwamba meli hiyo italazimika kujaza upepo ili iweze kuelea juu na kutoa mizigo na watu wanaosadikiwa kuwemo.
“Mashine ya kujaza upepo tunayo, na tunatarajia kujaza upepo ili iweze kuja juu, lakini zoezi hili litategemea na kina cha maji kitakavyokuwa na kama kitapungua italazimika tusubiri hadi usiku”, alisema Mkurugenzi huyo wakati akizungumza na Waziri Kiongozi Bw. Shamsi Vuai Nahodha.
Hata hivyo Waziri Kiongozi aliutaka uongozi wa Shirika la Bandari kufanya kila linalowezekana meli hiyo iweze kutolewa pamoja na watu wanaodaiwa kuzama katika melihiyo.
“Naomba munipe taarifa kila hatua mtakayokuwa mnafikia na pale mtakapokwama nitafurahi sana kama mtaiarifu Serikali”, alisema Waziri Kiongozi.
Nae Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Shariff Hamad, alisema kuwa watendaji katika Shirika la Bandari wanpaswa kuwajibishwa kwa vile chombo hicho kinajulikana siku nyingi kuwa hakina sifa za kubeba abiria, na hivi karibunikikitokea Pemba kilipotea na kuibukia Tanga wakati kilikuwa kikielekea Unguja.
“Hili jambo ni la kusikitisha sana kwani tangu awali chombo hiki kinajuulikana kuwa hakifai kwa vile hivi karibuni kiliweza kupotelea Tanga na badala yake abiria kulazimika kushushwa katika bandari ya Mkokotoni, naiomba Serikali iwachukulie hatuawahusika”, alisema Maalim Seif.



Top in Dar alonga

video

msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya TID alonga na globu ya jamii


kombe la mbuzi oye! hahahaaaaaa....

sherehe na bosi pamoja na tajiri
Mkuu wa wilaya ya nanihino,
hebu tubandikie ushindi wetu huu (Chelsea) wa kombe la mbuzi, lakini kumbuka nyinyi hata la kuku hamjaambulia mwaka huu! kudadadadadadeki..
Mdau Helsinki.


torres yupo yupo hadi 2013!!!

El Nino Fernando Torres

Assalam alaikhum Alhaji.

Habari ni kuwa kijana wetu FERNANDO TORRES juzi amemwaga wino wa kuwa liverpool hadi 2013 kwa miaka mitano zaidi. alikuwa na mkataba toka mwanzo ila wa juzi umeboreshwa kwa kuongezewa kitita chake toka £ 90,000 pound elfu tisini kwa wiki hadi zaidi ya laki moja na kumi kwa wiki£110,000.

wakati hilo likifanyika.jamaa zetu Manchester bado matumbo yao yako juu kwani kuna uvumi mkubwa kijana wao anaweza kutimkia Real Madrid. na hajasema kama atajicommit tena MAN U.pia amekuwa akimvunjia heshima kocha wake inaonekana hana nia ya kubaki man u.
Nakuwekea link ya habari ya mkataba wa Torres hapa.
homepage/sport/football/2454362
/Torres-agrees-30m-Kop-contract.html
mkuu naomba usitoe jina langu iandike kivyako.
mdau meya wa uk.


swali la kizushi

Bro Misupu,
pole na mihangaiko pamoja na jitihada za kututumikia sisi Wadau'z kwa moyo mkunjufu tena bila chembe ya Ufisadi kama wao (usiniulize akina nani).
Sasa Bro nitashukuru kama utanisaidia kunipatia jibu mujarabu manake Wanawake wanaotembea na waume za watu huitwa Vimada au Nyumba ndogo. Sasa Bro pamoja na wadau'z, mwanaume anayetembea na mke wa mtu anaitwaje?
Nitashkuru sana nikipatiwa ufumbuzi wa swali langu toka kwa wadau wa blogu ya jamii...
Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Kimdau cha Moscow.
P'se Jina na E-mail kapuni kama haitakuwia ngumu!


ray na kanumba walonga

video

nyota wa filamu bongo ray na kanumba walonga na globu ya jamii


iluminata james ndiye miss universe tz 2009

ukumbi mpya a mlimani city conference center kwa nje. hapa ndipo miss universe tz 2009 imefanyikia
iluminata james miss universe tz 2009
tano bora
iluminata james akiwa na majaji baada ya mchuano. toka shoto ni rosie motene mtangazaji wa tv ya channel 53 ya sauzi, masudi kipanya na mbunge wa viti maalumu mh. al sharyamaa kwegyabir.
wadau wa kenya airways na mrembo iluminata
meza ya mabosi wa sumsung tanzania, wafadhili wakuu wa miss universe tz
gwaride la warembo
kumi bora
mwandaaji maria sarungi-tsehai akielekeza jambo kwa majaji

maria akieleza jambo majaji. kulia ni mzee mzima john kitime ambaye naye alikuwa jaji. cheki alivyotoka pina!
msanii wahuu toka kenya akitumbuiza

ambwene yesaya a.k.a ay alikuwepo kuwapa watu raha
kikundi cha ngoma cha albino kilitia fora katika shoo hiyo
sindimba toka mang'aka lilimwaga na wasanii albino

sebene lilimwagwa na diamon musica
mwandaaji wa miss universe tz maria sarungi-tsehai akimzawadia tuzo mshindi wa miss universe tz 2009 iluminata james baada ya kuibuka kidedea usiku huu kwenye mchuano uliofanyika ukumbi mpya wa mlimani city conference centre hapa dar. iluminata ana umri wa miaka 23 na anatokea mwanza
miss universe tz 2009 iluminata james (kati) akipozi na mshindi wa pili evelyn almasi (kulia) na hidaya maeda ambaye ni mshindi wa tatu

iluminata akiwa na mshindi wa pili evelyn (kulia) na mshindi wa tatu hidaya baada ya matokeo
wadau wa precision air ambao ni moja ya wadhamini wakipozi na miss universe 2009 iluminata james baada ya kutangwanza matokeo usiku huu.
Habari Kamili
Mlimbwende Iluminata James kutoka mkoani Mwanza leo usiku ametwaa taji la Miss Universe Tanzania kwa mwaka 2009 na kujikatia tiketi ya kuliwakilisha taifa katika michuano ya dunia itakayofanyika baadaye mwaka huu katika visiwa vya Bahamas.
Iluminata ambaye anampokea taji hiyo mwanadada nyota katika fani ya mitindo nchini Miriam Odemba alifanikiwa kutwaa taji hilo baada ya kuwashinda walimbwende wenzake 19 ambao nao walikuwa wakichuana vikali kuwania taji hilo.
Shindano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Mlimani city jijini Dar es Salaam , mbali ya mashabiki wa masuala ya ulimbwende kupata burudani ya kuonyeshwa mavazi na miondoko ya ‘catwalk’ kutoka kwa washiriki 20 pia walikongwa nyoyo zao na burudani safi ya muziki kutoka kwa msanii nyota wa Bongofleva , Ambwene Yesaya ‘Mzee wa Comercial’ , mwanadada Wahuu kutoka Kenya anayetamba na wimbo wa ‘Sweet love’.
K abla ya hapo bendi ya Diamond Musica chini ya Allaine Mulumba ilikuja na wimbo wao maarufu wa ‘Mapenzi kitu gani’ na kufuatiwa na sebene la uhakika na burudani hiyo ilihitimishwa na ngoma za utamaduni kutoka kikundi cha Albino Revolution Cultural Troope.
Mbali na Iluminata washindi wengine katika fainali hizo za Miss Universe Tanzania ambazo zilihusisha warembo kutoka mikoa mitano ya Tanzania , Arusha , Mwanza , Dodoma , Morogoro na Dar es Salaam walikuwa ni Evelyne Almasi ambaye alichukua nafasi ya pili na hivyo kujipatia nafasi ya kushiriki kwenye shindano la Miss Earth.
Mwanadada Hidaya Maeda ambaye alishinda nafasi ya tatu katika kinyang’anyiro hicho, yeye ataliwakilisha taifa katika shindano la Miss International baadaye mwaka huu, na nafasi ya nne ilikwenda kwenye Zeinab Kianda na Gisela Tarimo alinyakua nafasi ya tano.
Miss Universe Tanzania 2009 mbali ya kujipatia tiketi ya kushiriki kwenye shindano la dunia pia alizawadiwa Sh milioni tatu , nafasi ya kusoma kozi ya lugha ya kifaransa kwa mwaka mmoja katika kituo cha Alliance Francaise pamoja na kupatiwa vipodozi vyenye thamani ya Sh 500,000 na duka la Shear Illusion .
Majaji wa shindano hilo walikuwa ni pamoja na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Al Sharyamaa Kwegyabir , mwanamuziki John Kitime,Masoud Kipanya , Mbunifu wa mavazi Ally Rhemtullah, Maria Sarungi Tsehai , Amit Patel kutoka kwa wadhamini wa shindano hilo kampuni ya Samsung ambao waliongozwa na jaji mkuu Rosie Motene kutoka Afrika Kusini ambaye ni Muigizaji nyota na Mtangazaji wa kituo cha Studio 53.


AJALI YA MELI ZENJI KATIKA PICHA NA HABARI KAMILIFU

MABAHARIA WA BOTI YA RUBANI YA SHIRIKA LA BANDARI ZANZIBAR WAKISHUSHA MIILI YA MAREHEMU WATATU WA AJALIM YA MELI HIYO AKIWEMO MTOTO WA KIUME NA WATU WAZIMA MMOJA WA KIUME NA WA KIKE
HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA KATIKA AJALI YA MELI YA FATIH IKIWA IMEBIRUKA KATIKA BANDARI YA ZANZIBAR IKITOKEA DAR-ES-SALAAM IKIWA NA ABIRIA NA MIZIGO MPAKA SASA TAYARI MAITI TATU ZIMESHAPATIKANA WAFANYAKAZI WA MSARABA MWEKUNDU WAKIONDOA MWILI WA MMOJA WA MATI WA AJALI YA MELI YA FATIH WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI WA KAMATI YA UJENZI NA MAWASILIANO WAKIFUATILIA UTARATIBU WA UOKOAJI WA ABIRIA WA MELI YA MV FATIH USIKU WA 29-5-2009, KUTOKA KULIA ZAKIA OMAR JUMA CUF, MZEE ALI USSI CCM,MAKAMO MWENYEKITI HAMADI MASUOD HAMADI CUF, RAMADHANI NYONGE CCM NA MWENYEKITI WA KAMATI HIYO KAMAL BASHA CCM.
WANANCHI WALIOFIKA LEO ASUBUHI KUSHUHUDIA AJALI YA MELI YA FATIH WAKIWA NJE YA BANDARI YA MALINDI KUTAKA KUJUWA WATU WALIOPATA AJALI HIYO YA MELI
WANUSURIKA KATILA AJALI YA MELI YA FATIH WAKIJIPATIA MSOSI KATIKA KITUO CHA POLISI
HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA KWA VIJANA WA MSALABA MWEKUNDU KUTOA HUDUMA KWA MAITI WA AJALI YA MELI
BAADHI YA MALI ZILIZOOKOLEWA KATIKA MELI ILIOZAMA KATIKA BANDARI YA ZANZIBAR IKITOKEA DAR-ES-SALAAM YAKIWA KATIKA BANDARI HIYO BAADA YA KUOKOLEWA. MAJINA YA WALIOPOTEZA MAISHA BADO KUPATIKANA NA IDADI KAMILI BADO KUJULIKANA KWANI LAZIMA NDUGU WA MAREHEMU WAJULISHWE MWANZO, NA JUHUDI ZA KUOPOA MAITI ZINAENDELEA.
Picha zote na mdau Othman Maulid Mapara
HABARI KAMILIFU

MELI ya mizigo ya inayomilikiwa na Kampuni ya Seagul, Mv Fatih, imepinduka na kuzama katika Bandari ya Malindi Zanzibar usiku wa kuamkia jana huku maiti za watu watatu zikiwa zimepatikana zikielea na watu wengine 27 wamejiokoa katika ajali hiyo ambapo mamilioni ya mali yanasadikiwa kupotea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Bakari Khatib Shaaban amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo, na kusema kwamba Meli hiyo ilikuwa tayari imeshafunga gati katika Bandari ya Malindi majira ya saa 4.00 kamili uski juzi usiku na abiria waliokuwemo walikuwa wanataka kushuka lakini ghafla ilipinduka na kuzama baharini.
Kamanda Shaaban alisema hadi jana mchana ni maiti za watu watatu tu ndizo zilizoonekana ikiwemo ya mtoto mdogo wa kiume, na watu wazima mwanamke na mwanaume ambao hawakuweza kufahamika majina yao kamili kutokana na hakna jamaa waliozitambua maiti hizo.
Waliookolewa katika ajali hiyo ni pamoja na Machano Mkinai Mkaazi wa Mkwajuni na Kitiba Mussa Kitiba, wa Gamba Mkoa wa Kaskazini 'A' Unguja, Halima Mussa wa Arusha, Hassan
Omar, Maulid Abdalla, wote wa Kisiju Mkoa wa Pwani.

Wengine ni Fatma Ali Salum, wa Kinyasini Wete kisiwani Pemba, Hawa Juma Saleh wa Rukwa Tanzania Bara, Zainab Ali Kitiba, Tandale Dar es Salaam, Sharifa Hamad wa
Wingwi Pemba, Ramadhan Juma Mohammed Tandale na Omar Khamis Mohammed wa Vinguguti Dar es Salaam.
Amesema baada ya kutokea tukio hilo polisi walitaka maelezo ya Nahodha wa Meli hiyo, Ussi Ali ambaye wanamshikilia kwa maelezo zaidi lakini lakini maelezo yake yanaonesha wasi wasi kwa jeshi la polisi kutokana na kuwepo utatanishi mwingi katika maelezo ya Nahodha huyo.
Kamanda Shaaban alisema kwamba awali Nahodha alisema katika meli yake
kulikuwa na abiria 25 na wafanyakazi 13, lakini Polisi inatilia shaka taarifa hizo kwani yawezekana Meli hiyo ilibeba abiria wengi na mizigo hivyo wanaendelea kumhoji
Nahodha huyo hadi hapo maelezo jeshi la polisi litakapopata maelezo ya kuridhisha kutoka kwa Nahodha huo.
"Jeshi la polisi halijaridhishwa na maelezo ya Nahodha bado hasa katika idadi za abiria alizozitoa lakini bado tunaendelea kumuhoji kwani hatujaridhika na taarifa yake" Alisema Kamanda huyo.
Kamanda Shaaban alisema jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi wa kina ili kujua chanzo cha ajali hiyo na haitosita kuwachukulia hatua wanaohusika na kuwataka wananchi kutulia na kuacha vyombo vya sheria kufanya kazi zao kwa wazi.
Hali katika Bandari ya Zanzibar baada ya ajali hiyo kutokea ilikuwa kitahanani kwa wananchi wakiwemo wafanyabiashara waliokuwa eneo hilo wakisubiri mizigo yao na jamaa zao jambo ambalo lilisababisha msongomano mkubwa kiasi cha kuwafanya Polisi kuwatawamya kwa kurusha risasi hewani.

Kutokana na hali hiyo Jeshi la Polisi lililazimika kuweka doria kali katika maeneo yote huku
wakishirikiana na baadhi ya askari wa vikosi vyengine kutokana na baadhi ya vibaka kujipenyeza na kuanza kuvuna mali zilizokuwemo katika Meli hiyo.

Kazi za utafutaji wa maiti nyengine iliendelea kwa siku nzima ya jana baada ya
wazamiaji zaidi ya 30 wa KMKM kuifanya kazi hiyo baada ya kuwasili saa 8.00 za usiku wa juzi.

Kazi hiyo, baada ya kupatikana kwa maiti tatu ilisita kwa usiku huo, iliendelea tena jana asubuhi kuanzia saa nne ambapo waokoaji hao waliamua kutumia mbinu mbalimbali za kuwawezesha kuingia ndani ya meli hiyo lakini hadi saa saba mchana walikuwa bado hawajafanikiwa kuingia ndani ya meli hiyo

Akisimulia mkasa wa ajali hiyo kepteni aliyekuwa akiendesha meli hiyo Ussi Ali Ussi, alisema wakati akiingia Bandarini ghafla aliona meli hiyo ikijaa maji na kulala upande wa
kushoto.
Alisema alianza safari yake saa 10.00 jioni kutoka Dar es Salaam na kuja Unguja ambapo aliwasili saa 3.30 usiku lakini akiwa njiani alipata tatizo la usukuni kutoenda vizuri akiwa karibu na kufika Bandarini hapo.
Akiendelea alifahamisha ndani ya meli hiyo alibeba mizigo yenye uzito watani 40, abiria 25 na wafanyakazi wake walikuwa ni 13 ambapo watatu aliwaona baada ya meli hiyo kuzama lakini kwa wakati huo wa usiku hakujua wapi walipo.
Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ni miongoni mwa viongozi waliofika katika eneo la bandari na Zanzibar kuonana na abiria waliookolewa na kushuhudia ajali hiyo.

Rais Karume aliwataka mafundi wanafanyakazi ya uokozi kuona kuwa wanajitahidi kuhakikisha kuitafuta miili zaidi kama bado imo ndani ya meli hiyo.
Katika bandari hiyo umati kubwa ulikuwa umesheheni huku mamia ya watu wakiwa wamekaa nje ya geti la gati wakitaka kuingia ndani kushuhudia jamaa zao na ajali hiyo ambayo jambo ambalo limesababisha msongamano mkubwa bandarni hapo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar, Mustafa Aboud Jumbe alimweleza Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha, kwamba juhudi za uokoaji inaendelea kwa kushirikiana na Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM), Polisi na wadau wengine wanaojitolea kusaidia uokozi huo.
Jumbe alisema bado ni mapema kuielezea serikali juu ya hatua za kuweza kuchukuliwa zaidi kwa vile wameanza kuifanya kazi hiyo ambapo imekuwa ngumu kutokanana na meli hiyo kuwa na mzigo mkubwa kiasi ambacho kimekuwa kikiwapa usumbufu waokowaji.
Kutokana na kuwepo kwa umma wa wananchi katika eneo la bandari Shirika la Bandari liliamua kufunga milango yake yote ya Bandari hiyo kwa usalama wa watu huku waandishi wa habari wakipata kazi kubwa katika ufanyaji kazi zake kutokana na vikwazo walivyokuwa wakiwekewa katika eneo hilo.
Jumbe alisema kwamba baadae watajaza upepo Meli hiyo iliyozama kwa kutumia kifaa maalum ili mizigo na watu waliokuwepo waweze kuja juu ambapo kazi hiyo itafanywa baada ya maji kujaa kwani kwa wakati huo maji yalikuwa yanakupwa na kazi hiyo ingeshindikana kufanyika.
Waziri Kiongozi aliwataka Viongozi wa Bandari kuieleza Serikali ni msaada gani wanaohitaji ili kuweza kufanikisha uokoaji wa mizigo, watu na meli hiyo ambapo Shirika la Bandari lilisema limejipanga vyema kukabiliana na janga hilo.
Wakati shirika la bandari likitoa ahadi hiyo hadi sasa hakuna msaada uliopatikana wa kutoa maiti zilizokuwa ndani ya meli hiyo huku Rais wa Zanzibar akilitaka shirika hilo kuomba msaada shirika la bandari la dare s salaam kuja kusaidia kuwaokoa watu waliomo ndani ya meli hiyo.
Habari zaidi kutoka kwa abiria walionusurika katika ajali hiyo wamedai kuwa ndani kulikuwa na watu wengi wanaokisiwa kufikia 100, lakini Nahodha wa Meli hiyo anapingana na idadi hiyo na kusisitiza kwamba meli yake ilikuwa na idadi ndogo ya abiria.
Halima Mussa mkazi wa Arusha ambaye amenusurika katika ajali hiyo alisema kwamba wakati tukio hilo linatokea alikuwa tayati ameanza kushuka ndani ya Meli hiyo, lakini ghafla aliona ikipinduka wakati ikiwa imefunga gati na baadae akiwa katika maji alijikuta ameshikilia kitu.
"Mimi namshukuru Mungu kwa sababu nilikuwa nashuka lakini ghafla nikajikuta nimo katika maji lakini baadae nikakamata kitu bila kukijua ni kitu gani nilichoshikilia na nikaaza kupiga
mayowe ya kutaka msaada na huku nyuma yangu nasikia sauti nyengine watu wakiomba msaada.
"Kuna watu waliokuwepo katika maji ndio wakanisaidia kwa kunambia shikilia hivyo hivyo hicho kitu na kunitaka ninyooshe mikono ndio waliponiokoa na kunileta juu" alisema Halima Mussa huku akihema.
Watu waliofika katika bandari ya Malindi yameilaumu serikali kwa kushindwa kuchukua hatua za dharura za kuweza kukabiliana na shughuli hiyo ambapo ajali imetokea majira ya saa 4 usiku lakini hadi saa tisa ndipo waokoaji waliopofika huku wakiwa hawana vifaa vya uokoaji.
"Ni dharau za hali ya mwisho hii maana ajali tokea saa 4 usiku lakini hawa watu wa KMKM wanakuja sa 9 hawana chochote cha kuweza kuwasaidia kuokoa abiria matokeo yake wamekuja na kuondoka kwa kisingizio cha kuongojea maji yakupwe" amesema Ali Haji Mkaazi wa Jangombe ambaye ana jamaa yake katika meli hiyo.
Naye Kepteni Juma wa meli ya Sea Bus amesema ipo haja ya kuwa na timu nzuri ya waokoaji na diver ili waeze kuwaokoa watu pindipo inapotokea ajali kama hiyo kwani.
"Lazima tuwe na timu nzuri ya divers wasaidie kuokoa lakini pia tax force ni muhimu kuwepo kwa ajili ya maafa kama haya na kufuata madili ya kazi ni kitu cha lazima kwa sisi manahodha ili kunusuru maisha ya watu" alisema Kepteni huyo.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad aliwaambia waandishi kwamba
wakati umefika hivi sasa kuhakikisha serikali inalifanyia kazi tatizo hilo ambalo linaweza kuathiri wananchi wengi kwa kuziwajibisha taasisi husika kwa vile meli hiyo tayari hapo
awali ilipata hitilafu na kulazimika kushusha abiria katika Bandari ya Mkokotoni baada kupata maharibiko ikitokea Pemba.

Maalim Seif alisema ipo haja kwa serikali hivi sasa kuvifanyia ukaguzi vyombo vya usafiri kwa kuona inatenganisha huduma kati ya vile vinavyotoa huduma baharini.
Meli hiyo ambayo inamilikiwa na Said Mbuzi imeelezwa kuwa ilibeba mizigo mbali mbali ikiwemo Trekta, gari mbili, magunia ya unga wa ngano, sukari, mchele, magunia ya viazi, ya nyanya, mifuko ya saruji, magodoro na bidhaa nyengine ambazo zote zimezama huku wajanja wakitumia nafasi hiyo kuopoa bagodoro na bidhaa nyengine na kukimbia nazo nchi kavu.
Tukio za kuzama kwa Meli hiyo ambayo uzamaji wake unafanana sana na ule wa
MV Bukoba linatokea wiki moja tu katika kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba mwezi Mei mwaka 1999 ambapo watu kadhaa walifariki dunia na kweka historia ya Tanzania katika ajali mbaya za meli zilizowahi kutokea nchini.


KUMBUKUMBU YA MAREHEMU ADELINA MAPANGO

ILIKUWA SIKU,WIKI,MIEZI NA SASA UMETIMIA MWAKA TANGU BWANA ALIPOKUCHUKUA MPENDWA WETU MAMA ADELINA MAPANGO (Mama CHAHALI).
PENGO ULILOTUACHIA HALITOZIBIKA MILELE.KINACHOTULIWAZA NI MAPENZI YA BWANA.JAPO SIE TULIKUPENDA,LAKINI YEYE ALIKUPENDA ZAIDI,NA NDIO MAANA AKAKUCHUKUA SAA4.30 USIKU WA TAREHE 29/05/2008.JAPO HAUKO NASI KIMWILI,LAKINI TUKO SOTE KIROHO.
KWA NIABA YA FAMILIA YA MZEE PHILEMON CHAHALI,NACHUKUA FURSA HII KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA WOTE WALIOSHIRIKIANA NASI KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE KATIKA SALA/DUA WAKATI TUNAMUUGUZA MAREHEMU ADELINA,NA SAPOTI MLIYOTUPATIA KUTUFARIJI BAADA YA MSIBA.BWANA AWABARIKI SANA.
BWANA ALITOA,BWANA ALITWAA.JINA LAKE LIHIMIDIWE MILELE,AMEN. PUMZIKO LA MILELE UMPE EE BWANA,NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE.APUMZIKE KWA AMANI.
AMEEN


miss tz kanda ya mashariki yanukia



kp leo



queen suzy wa ngwasuma apata mchumba malaysia

Mnenguaji wa FM Academia Queen Suzy ambaye kwa sasa yuko Malaysia ziarani na Bendi ya The Kilimanjaro Connections amepata mchumba ambaye anatarajia kufunga naye ndoa baadaye mwaka huu.

Suzy amevalishwa pete ya uchumba na mchumba wake ambaye ni raia wa Uingereza anayeishi na kufanya kazi nchini Malaysia.

Kwa picha zaidi na habari bofya hapo chini:


JK katika CNN

Habari za kazi mkuu wa wilaya.
Naomba uwarushie wadau linki ya mahojiano kati ya Mhe. Rais Kikwete na CNN.
http://edition.cnn.com/video/#/video/
international/2009/05/29/av.1.jakaya.kikwete.cnn


Dr. Tajudeen Abdul Raheem Remebered today at UDSM

The late Dr. Tajudeen Abdul Raheem

THE MWALIMU NYERERE FOUNDATION
{In collaboration with UDASA who booked the Venue}
INVITES ALL TO
A “DAY” VIGIL IN MEMORY OF
Dr. Tajudeen Abdul Raheem
AT
THE COUNCIL CHAMBER,
THE UNIVERSITY OF
DAR ES SALAAM
MAIN CAMPUS
THIS SATURDAY 30TH MAY 2009
FROM 9AM TO 12NOON
A book of condolences will also be open for signature


AJALI YA KUZAMA KWA MELI ZENJI

HABARI TOKA VISIWANI ASUBUHI HII ZIMETHIBITISHA KWAMBA MELI IITAYO MV FATHI IMEZAMA KATIKA BANDARI YA ZENJI NA JUHUDI ZINAENDELEA KUOPOA MAITI TOKA KATIKA MELI HIYO AMBAYO ILIKUWA INAJIANDAA NA SAFARI YA KUELEKEA DAR IKIWA NA SHEHENA YA MIZIGO MBALIMBALI NA ABIRIA.
HABARI ZINASEMA HADI SASA MAITI WATATU (MWANAUME MMOJA NA MWANAMKE NA KIJANA WA KIUME WA UMRI WA MIAKA KATI YA 14-17) WAMEOPOLEWA HADI SASA, ILA MAJINA YAO BADO KUPATIKANA.
SABABU YA KUZAMA KWA MELI HIYO BADO HAIJAJULIKANA NA IDADI KAMILI YA ABIRIA WALIOKUWAMO NA WALIOPOTEZA MAISHA AMA KUOKOKA PIA BADO KUJULIKANA KWANI KAZI YA KUOPOA MAITI BADO ZINAENDELEA. INASADIKIWA KUNA WATU ZAIDI MAJINI.
HABARI ZAIDI NA PICHA TUTAPATA BAADAYE WAKATI GLOBU YA JAMII IKIENDELEA KUFUATILIA KWA UKARIBU AJALI HII


aquarius web designing and development

Hello all,
We are now undertaking website designing and development.
PRICE $350 USD,
VAT EXCLUSIVE
Web designing of up to 8-10 pages can be delivered in 48 hours for your approval. We believe to have the most reasonable in prices than town.
3D "gif animations","avi video files", "mp3 audio files", slide shows can be inserted also. We require all datas typed in word files eg. company profile, services etc.
Photography & video is also our passion and use professional Nikon 8 mega pixel camera.( little extra cost for photography if required for your site )
Domain registration and web hosting can also be taken care by us at a reasonable price.
THANKS
SUJIT BHOJAK
AQUARIUS ADVERTISING LTD.
SEWA STREET,
0754 373733


usiku wa wana masoko afrika mashariki wafana dar

mgeni rasmi mkurugenzi mkuu wa kenya breweries ltd Baker Magunda akitoa darasa wakati wa sherehe ya usiku wa masoko kwa wana afrika mashariki uliofanyika hoteli ya kempinski kilimanjaro jijini dar usiku wa kuamkia leo ambapo wafanyakazi katika vitengo vya masoko toka makampuni mbalimbali walikusanyika pamoja katika mnuso huo uliodhaminiwa na vodacom, tbl na mwananchi
bosi wa masoko wa vodacom ephraim mafuru akiongea wakati wa mnuso huo
meneja wa kilaji cha ndovu wa tbl george kavishe akimwaga sera
mashindano yaliyoshirikisha wadau mbalimbali yalikuwepo. hapo ni kabla ya kuanza kwa shindano la kusakata rhumba
bosi wa masoko wa vodacom tanzania ephraim mafuru akishuhudia mai waifu wake akikata keki aliyomwandalia ikiwa ni sapraizi kwani siku hii iliangukia siku ya mnuso wa wana masoko
wasanii wakali wa afrika mashariki kwa sasa amani toka kenya (shoto) akila pozi na marlaw kabla hawajatumbuiza
amani akitumbuiza
bebe cool toka uganda alikuwepo kutia radha mnuso huu
marlaw akipagawisha kwa kibao chake cha 'pi pi pi'

meneja wa kilaji cha ndovu george kavishe (kulia) akiwa na bosi wa masoko wa stanbic bank abdallah singano (pili kulia), kelvin twissa wa masoko zain (shoto) na mdau papa kooll wakila pozi mnusoni
ilikuwa furaha na vifijo usiku mzima
kipindi cha maswali na majibu kilinoga hasa watu kama mama saada mufuruki walipomuuliza mtoa mada kuhusu maswala mbalimbali ya masoko

wadau wakishindana kukata mayenu. nanihii ndani ila alitolewa raundi ya kwanza...

















Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker