Shirika la Dhahabu la Barrick (NYSE:ABX) (TSX:ABX) leo limeelezea msimamo
wake kuhusu muswada wa wanachama binafsi (C-300) ambao kwa sasa uko mbele ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nchi za Nje na Maendeleo ya Kimataifa ya Kanada, kwa kusisitiza kwamba, Muswada hauna umuhimu na kwamba huleta athari mbaya kwa biashara za Kanada. Vile vile Barrick imeeleza ukweli kuhusu madai yasiyothibitishwa ambayo yamekuwa yakitolewa na watu kwenye Kamati hiyo.
Katika taarifa yao ya pamoja na Kampuni ya Goldcorp Inc. na Shirika la Kinross Gold, makampuni hayo yamedokeza kwamba Muswada nambari C-300 utaathiri vibaya sana sekta ya uchimbaji madini ya Kanada kwa vipengele vikuu vitano:
1. Kuihatarisha nafasi ya ushindani ya makampuni ya Kikanada;
2. Kusababisha kushuka kwa heshima ya makampuni ya Kikanada;
3. Kudhoofisha ushirikiano na ubia katika Wajibu wa Mashirika kwa Jamii (CSR);
4. Kuchagiza makampuni kuhamia sehemu nyingine; na
5. Kudharau taratibu za sasa za kisheria za Wajibu wa Mashirika kwa Jamii.
(ili kupata nakala ya mawasilisho, tafadhali ingia kwenye tovuti hii:
www.barrick.com
“Leo hii tunawapa wanakamati maelezo ya kina, ukweli na uhakika ili kujibu
shutuma mbalimbali kwa ajili ya kuweka kumbukumbu sahihi. Masuala ya uchunguzi makini na hata ukosoaji ni sehemu ya ufanyaji biashara, lakini yanapaswa kuwa ya haki na ukweli,” alisema Bwana Vincent Borg, Makamu Mtendaji wa Rais, Mawasiliano Ngazi ya Shirika.
“Kitu kimoja kimeonekana dhahiri wakati vikao vya mashauriano vikiendelea: baadhi ya watu hawakuletwa hata kuthibitisha shutuma zao kali juu ya sekta ya uchimbaji madini ya Kanada pamoja na Barrick Gold - leo hii nyingi kati ya hizo zimebainika bayana kuwa ni za uwongo. Hawakuipatia Kamati hii
taarifa za ukweli na uhakika wala ushahidi kwa ajili ya kusimamia madai yao wakati wakitoa chokochoko za hapa na pale za kupaka matope kampuni.”
“ Vikao vya kusikiliza kesi hiyo vimetoa nafasi kubwa ya kudhihirisha ni
namna gani Muswada nambari C-300 ulivyogeuka kuwa sumaku ya kuvutia madai ya uwongo na yasiyothibitishwa yatokayo kwa watu mbalimbali kutoka sehemu yoyote ile duniani na hakuna kinachofanyika zaidi ya kuiathiri sekta ya uchimbaji madini ya Kanada,” aliongeza Bw. Borg.
Katika kila nchi huru ambamo Barrick huendesha shughuli zake, kuna taasisi
za serikali, mifumo ya sheria, mamlaka zinazohusika na sera, taratibu za kisheria pamoja na mahakama. Barrick inaamini kwamba katika nchi hizi shutuma za namna hiyo hutolewa inavyostahiki zikiambatana na maelezo yote ya ukweli na yanayohusiana na madai hayo na si kamati ya bunge ya Kanada ambayo haikutoa uhakiki wala maelezo. Zaidi ya mataifa hayo huru, makampuni huwa yanawajibika katika ngazi ya kimataifa na kwa kufuata miongozo inayohusu uwajibikaji.
“Chombo husika kwa ajili ya urekebishi na utatuzi ni mahakama au mamlaka
huria zinazohusika ambapo masuala yanaweza kuchunguzwa ipasavyo kwa wakati muafaka - na si majukwaa ya kisiasa,” aliongeza Bw. Borg.
Dhamira ya Shirika la Dhahabu la Barrick ni kuwa kampuni bora zaidi ya
dhahabu ulimwenguni kwa kutafuta, kutwaa, kuendeleza na kuzalisha rizavu zenye kiwango bora kwa usalama, kwa faida na kwa kuwajibika kwa jamii.
MAWASILIANO NA WAWEKEZAJI:
Deni Nicoski
Makamu wa Rais,
Mahusiano na Wawekezaji
Simu: (416) 307-7410
Barua-pepe:
dnicoski@barrick.com
MAWASILIANO NA VYOMBO VYA HABARI:
Vincent Borg
Makamu Mtendaji wa Rais,
Mawasiliano Ngazi ya Shirika
Simu: (416) 307-7477
Barua-pepe: vborg@barrick.com