Mshambuliaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 Ngorongoro Heroes , Thomas Ulimwengu (kulia) akimtoka beki wa timu ya vijana ya Malawi, Lucky Malata (5) katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Ngorongoro ilishinda 3-1. Mshambuliaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 Ngorongoro Heroes , Thomas Ulimwengu (kulia) akiwania mpira sambamba na beki wa timu ya vijana ya Malawi, Limbikani Mzava katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Ngorongoro ilishinda 3-1. Golikipa wa timu ya taifa ya Malawi ya vijana chini ya miaka 20, Alex Makina akiuangalia mpira ukitinga wavuni na kuhesabu bao la pili kwa timu ya taifa ya Ngorongoro Heroes. kocha wa timu ya taifa ya vijana ya Malawi akiwa ameeduwaa baada ya mchezo kumalizika
Kocha wa timu ya vijana chini ya 20, Rodrigo Stockler akimpongeza mfungaji wa bao la pili la timu hiyo, Omega Seme wakati mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Ngorongoro ilishinda 3-1. Kwa matokeo hayo timu ya ngorongoro itakutana na timu ya vijana ya Ivory Coast wiki ya tatu ya mwezi mei ambapo mchezo wa kwanza utafanyika katika nchini Ivory Coast na baada ya wiki mbili timu hizo zitarudiana katika dimba uwanja wa taifa, Dar es Salaam.
Is Ngorongoro Heroes any different from Serengeti Boys? Kindly Explain!
ReplyDeleteIt's a good thing that they did, beating Malawi that is. Facilitations!
Kama sijakosea Serengeti ni U-17 na Ngorongoro ni U-20.
ReplyDeleteHEKO!
Ngorongoro Heroes is the Youth national team whose players are aging under-20
ReplyDeleteWHILE
the Serengeti Boys is the youth national team whose players are aging under-17.
NDUGU WAHUSIKA MIMI NAPENDA KUTOA ONYO KUHUSU UZIO (fence) HAPO JUU ZIMEKA KINOMA SANA.HII NI HATARI SANA IKITOKEA FUJO ISIJE IKATOKEA KAMA HILLSBOROGH soma hapa .
ReplyDeleteHongera vijana wetu, kazeni buti kwa safari bado ni ndefu sana.
ReplyDeleteAnkal tunashukuru kwa hizi habari za picha ambazo kwa kawaida huleta kutoka katika viwanja vyetu. Ni more reliable kuliko kurasa na michezo za magazeti yetu.
picha ya kwanza hilo bango la biashara or whatever lilitakiwa liwe nje ya uwanja. Wabongo akili zipo wapi?
ReplyDeletembona uwanjani mashabiki ni wachache?
ReplyDeletewatanzania lazima tujifunze kusupport wachezaji. sioni haja ya watu kuingia bure uwanjani, kwa nini hata kama hamna pesa ya kutosha walipe kiasi fulani nafuu japo kuchangia gharama za kuutunza uwanja? hiyo tabia ya BURE...bure inanikela. pay something. and anything makes a difference. fikra za kutaka vya bure haziishii hapo kesho mkiwa viongozi mnaishia kuomba hata vitu ambavyo mnaweza kufanya wenyewe.