Ni Da'Devota akiwa na mai hazbendi wake siku walipomeremeta.
Taswira zaidi BOFYA HAPA
Nguo za Maharusi toka Virago Boutique Namanga, Dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 37 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 21, 2010

    We Devota mbona hukunialika,kumba una mipango kabambe ya kupata mwenzi!
    Mdau wa Mbezi Beach

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 21, 2010

    vigezo gani vimetuka kuifanya kuwa ni ya mwaka?

    ReplyDelete
  3. PETER NALITOLELAMay 21, 2010

    JAMANI DADA YANGU ANATAFUTA MCHUMBA MZUNGU. YEYE HACHAGUI AWE MNENE AU MWEMBAMBA. DADA YANGU YAANI HACHAGUI KABISA, HAWE NA MENO AU ASIWE NAYO,TAHIRA AU JINIAS YEYE YEYE HACHAGUI LAKINI ZE MUZUNGU IS NOT RICHEBO BASI HATA HIS HIGHNESSESS HASHEEM THABITI NA YOHANNA MASHAKA WANAFAA KABISA KWA SABABU WAO NI TWARISTI WA TANZANIA NA CELEBRITI WA USA. NBA NA WOLSTRITI. HAWA JAMAA WANATOKA CHUO CHA MUZUMBE CHA KULE MOLOGOLO AMBAKO WOTE TUMEKULA NONDOZZZ. KWANI HAWA JAMAA WAWILI PIA NI WAWEKEZAJI, LAKINI DADA YANGU ANAOGOPAGA KUFUNGA NDOA BILICANAS KWA SABABU T.I.D ATAWALOGA JAMANI. SASA DEVOTA, TUFANYEJE KWA SABABU DADA YANGU NAYE ANATAKA KUWA SELEBRITI NA KUWA JUU. ILA UMEPENDEZA SANA NA HUKO JUU SANA NA MAIEZIBENDI WAKO WA KUTOKA USA YA NBA. MIMI BWANA NIKITOKA TU KANADA KULA NONDOZZ, NITASHUKA NA MAIWAIFU WANGU WA KITASHA PALE EAPOTI YA KIPAWA NA KUPOKEWA NA GNOMA ZA TAMADUNI

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 21, 2010

    weee ankal Michu, una uhakika hili gauni lilitoka namanga ya Dar? Maana mtaa wa pili walisema eti alikuwa ameliagiza kutoka NY City Marekani jamani, msimuangushe mtoto wa watu, alipendeza!

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 21, 2010

    mzungu atakuwa anataka wa Tanzania.lakini wewe bint umeumbika. kila la heri ktk ndoa yako.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 21, 2010

    kwakweli sijawahi kuona harusi nzuri kama ya devota Tanzania,big up sis mlitoka kwa kweli.
    J

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 21, 2010

    Shemeji Chibonge!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 21, 2010

    Diva kuna wengine hukututendea haki tulichanga lakin kadi hatukupewa tukajaisikia kwenye bomba tu kuwa hakukuwa na sendoff only kitchen party na harusi tu..Poa sina jakamoyo nakutakia Kheri katika Maisha mapya ya Ndoa

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 21, 2010

    wamependeza sana jamani, dhu naona wadada wa Bongo kuoa wathungu ni fashion, but ni kweli kwani wanaume wa bongo wamezidi kucheat! hongera DEVO.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 21, 2010

    this is the wedding sijawai kuona bongo, OMG. wao wao wao! am speachless! ngoja nitafute mzungu wangu mie lo shida za nini! hope I will get one. am so so so jealous!

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 21, 2010

    kwakweli bora kajipatia mume wa ukweli,maana kucheat kwa wanaume wa kibongo kumezidi
    kutwa kucha twaambukizwa migonjwa na UKIMWI juu,asipite msichana mijicho gube gube jujuu tu.

    mzungu (% kubwa) mkichokana mnaambiana basi hakuna mitabia ya kishashi-shashi

    sikujui dada ila hongera zako!!

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 21, 2010

    Kama mlikuwa hamjui mzungu ha cheat lakini atakuulia mbali. Wewe una shida zako lakini na wao pia wanamahesabu yao na sio hivyo hivyo tu. Na nani aliyekuambia kwamba mzungu ha cheat?

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 21, 2010

    mimi pia nimeolewa na mzungu na tumebahatika kuwa na watoto wawili na number 3 on the way, before nilikuwa na mchumba wangu (M-TZ) mapenzi yake yalikuwa mara leo yuko na huyu mara kesho, so akawa anijali kabisa at the end, na tangu nimempata my hubby sasa ambaye ni mtungu, yaani life is so easy! they do care so much and they love the kids a lot! am very blessed and never date a mbongo again, magonjwa kibao!

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 21, 2010

    Devota umependeza sana wewe na mumeo. Yaani sina la kusema kwa jinsi ulivyonoga kuanzia kitchen party mpaka harusi. Mungu aibariki na ndoa yako inoge hivvyo hivyo...Nagira A Town.

    ReplyDelete
  15. Sister J.May 21, 2010

    Wadau hapo juu mnaodhani WANAUME wa BONGO wanaongoza KU-CHEAT nadhani hamjawahi kutoka nje ya nchi... LoL!!Poleni zenu nyingi sana!!

    Mume wangu ni Mzungu(American) na mara kadhaa nimekuta msg kwenye simu yake toka kwa girls achilia mbali HARUFU FULANI ninayoikuta kwenye nguo na mwili siku alizoni-CHEAT nikagundua.

    Well, sijali sana kwani alishaniomba msamaha nikasamehe, japo kuwa mwenendo bado unamashaka hadi leo.

    Nadhani nyinyi wadada mlio bongo mshafunguka macho hapo.. Men yeyote ana-cheat kwa hulka za mwili wake.

    Jessica, MD

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 21, 2010

    Mbona huyu dada yeye hamjashambulia kama mlivyomshambulia mzee wa nondozi...makulilo junior, wiki kadhaa alipofunga ndoa. nakumbuka hapa karibia commets zote zilikuwa ni khs makaratasi, lakini hapa hatujaona kuwa devota yeye naye ni makaratasi hahahahaa

    mpenda haki

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 21, 2010

    Dada umependaza kweli na harusi yako ilikua nzuri. Hongera kwa harusi nzuri sana.Wote pia mmependeza pamoja na shemu.

    ReplyDelete
  18. Hongera dada Harusi yako ilikua nzuri sana.Da yani mimi najiuliza huyu mme wako alikutoa pesa za harusi au mlichanga?Maana mimi wazungu nawajua kabisa Harusi zao hua si za garama.si kama hawana pesa la hasha.

    Mimi mwenzako ndoa yangu nimefungia Las vegas lakini ndungu yangu wagen waalikwa walikua 5 tu,hakuna kichen part wala nini.Kuhusu chakula baada ya kufunga ndoa ni hotelini.

    Kama kweli huyu mzungu wako alitoa pesa za gharama za harusi basi huyo mtu kweli kweli.Ila sasa kama mdau alivo sema hapa juu ndugu ndoa na mzungu mmmmmm.inataka moyo sana kwani yeye akichoka anakuacha kama vile hakuwahi kukujua.

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 21, 2010

    huo mchuchumao wa huyo bwana harusi!! tarumbeta lazima zihite!!

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 21, 2010

    Hii harusi ni kiboko. I think it deserves to be harusi ya mwaka coz sidhani kama kuna nyingine iliyowahi kuifikia hii hapa nchini. See for yourself kufuru waliyoifanya

    ReplyDelete
  21. AnonymousMay 21, 2010

    Michuzi we sema tu wamekulipa shilingi ngapi kufanya hiyo personal advertisement. Mbona harusi nyingi tu nzuri zimefanywa mwaka huu na haukuzitoa?

    ReplyDelete
  22. Bwana Makullilo ndoa yake wananchi mliishambulia sana mbona hakuna wapambe sjiunini ndoa ya makaratasi sasa hii ndoa ya nini kalamu.

    ReplyDelete
  23. AnonymousMay 21, 2010

    Kweli huyo dada alipendeza sana. Tunawatakia maisha mema na baraka tele tela

    Anayesema wanaume wakibongo hujui kitu. Kucheat ni kucheat tu. Na wanaume wa kitanzania wana roho ya kufeel guilty hawa hawana kabisa. I have been there I have done that. Akishaamua mambo yake ni ameamua. Hamna cha therapy wala nini kitakachombadilisha roho yake. Akisema I am not happy it's over. Kama mlikutana mkiwa mnatengeneza hela nzuri sasa situation yako imechange ni basi tena. Alikupenda kwa mwili wako mwembamba ukiengeza kg moja tu utakoma. Na kama alikupendea life insurance ndio hivyo tena shurti ulale jicho moja macho kila siku. La sivyo......

    Na kuhusu makulilo Jr na harusi yake juzi kwa vile hujui kitu. Lisemwalo lipo na ukiona the majority of the people wanaongelea the same thing jua kuna ukweli ndani yake. Huyu wengi hawamjui na hawajui huu urafiki wao waliuanza lini. Lakini makulilo nani asiyemjua na amekwenda lini USA na kumfahamu huyo mwanamke lini na kuamua kuoana naye? Think about it. Ya makulilo ilikua ya haraka sana ...Kulikua hakuna meet and greet...It was just I do I do....

    Note that ingawaje harusi nyingi zinaanzaga kwa lengo la papers na watu wengi wanasema lakini nyingi zina products nzuri tu. Watu wengi wanafall in love kikweli baada ya kuoana na wengi wana watoto sasa wazuri tu. It's all about ur destiny

    ReplyDelete
  24. AnonymousMay 22, 2010

    Mimi chichemi. Shemeji itabidi amfundishe dada yetu kidhungu sana. Kilapagraph kidogo vile cha introduction makesa yote yale...Mhhhhh

    ReplyDelete
  25. AnonymousMay 22, 2010

    kwanza kabisa hongera Da Devota kwa kuingia kwenye chama cha wanandoa.

    pili, hao wanaojidanganya kua wanaume wa kizungu hawacheat wanahitaji msaada wa kisaikolojia haraka sana.hiyo ni nature ya wanaume,kutafuta mwanamke mwingine baada ya kuwa na wewe kwa muda fulani. tena wazungu ni balaa, yaani akikuchoka anakupa black and white na kuanza mbele wakati wewe bado unampenda na pengine mna watoto pamoja. wanawake wa kibongo bora mtafute wabongo wenzenu kuliko kujiumiza roho kutafuta wazungu..

    na msije kuniita hater au nina wivu, kwa taarifa yenu mimi nimeolewa na mzungu lakini nawaona wanaume wote lao moja,awe mzungu,m-bongo au mhindi.kama wakwako hajacheat leo,ipo siku tu atacheat..take your time kumsoma or else learn from bill clinton and the rest..lol

    ReplyDelete
  26. AnonymousMay 22, 2010

    NIMEKUMBUKA HII HARUSI NDO ILIOKUWA INALETA UGOMVI KWENYE BLOG YA UTURN.JAMANI HARUSI YA MWENYE UTURN HAIFIKII HII HATA KWANINI DEVOTA APEWE SIFA ZAKE JAMANI.HIYO KITCHENI PARTY TU NDO KAMA RECEPTIONI.MH KAFUNIKA.

    ReplyDelete
  27. AnonymousMay 22, 2010

    wanaume ni wanaume tu, binafsi:

    nilipendana na mzungu mmoja huku north america akawa mhuni, yes they take care of you but they do cheat too. Haya nikamalizana nae huyo kupata mwingine ananiambia baada ya miaka 3 sorry baby im gay, hapo ndio nilichoka kabisa, nikaachana nae nikakaa muda bila mtu ila bwana desturi za kiafrica mtoto wa kike uolewe na nini nikaona naendea miaka 30 ngoja nitafute wa kukata nae ukapera... nikapata mbongo mwenzangu ambae huwezi kuamini, jamaa ni fiti sana, hana mambo ya wanawake, matatizo tunamaliza wote, nikimweleza bwana nyumbani matatizo natuma pesa hana neno basi ni raha tu tatizo ni moja tu, ndugu zake, mawifi ni nuksi haswa hata wakwe nao saa zingine si watu wazuri lakini i always try to stay away from the, i mean what the heck i am already married to him, so they can simply fall back, and let me do my thing. sasa hivi wanafikiria nimempa limbwata kumbe si hivyo ni basi tu wote tulikuwa tunatafuta mtu wa kuishi nae milele thanks god. Sala zimenisaidia sana.

    ReplyDelete
  28. AnonymousMay 22, 2010

    inaweza kuwa hata huyu jamaa yeye ndio anataka karatasi za kuishi africa si unajua wazungu kwa kututumia na wenyewe wamo sana. sasa devota kaa mbali na marafiki singo, watakuharibia nyumba. kaa elewana na mumeo. Majiko siku hizi ni tabu kupata watu hawaoi. wanataka tu kumtumia mtu weeeee bila ya kuoa so tulia binti

    ReplyDelete
  29. AnonymousMay 22, 2010

    Devota naomba unipe jina ya blog yako tafadhali nasikia ipo ila sijawahi iona., au wadau wenzangu ka mwaijua hiyo blog naomba mturushie hapa, picha zako nzuri sana. Shukrani

    ReplyDelete
  30. Nimerudi tena baada ya kusoma wadau wachache hapa juu yangu nakubaliana na baadhi yao.Devota sikujui wala nini,na tafadhali usiseme nina wivu na ndoa yako la hasha.

    mimi mme wangu ni mzungu wa Usa,na ngoja nikwambie mme wangu huyu alikuja kunichukua Tz na akanileta hapa usa,Na haraka haraka tukafunga ndoa.

    lakini Devota wangu,wazungu hawana dogo hata kidogo,ukivunja sahani kwao kubwa,yani namaanisha hawana dogo kwao kila jambo ni kubwa.

    mda si mrefu tuligombana na mme wangu,yani hakyanani nikusimulia sababu huwezi kuamini,basi jaa akanunua tiketi akaniambia.You know what .... i am done with you,this is tiket back home.

    mwenzangu nikashanga yani doaa imedum miezi 5 tu leo mzungu amesha done na mimi,yani akasema chukua guo zoka na nakupeleka uwanja wa ndege mda huu.

    ndege yangu ilikkua inaondoka asubuhi na mzungu alinipeleka uwanjani jioni yani alitaka nilale uwanjani mpaka asubuhi.uliza nilipewa shilingi ngapi sasa ya kula njiani.elifu idhirini tu.

    bahati nzuri nilipata msamaria mwema uwanjani hapo akanipeleka kwake.na baada ya kukaa siku kadhaa nikampigia sim mzungu na nikamwomba msamaha kwa kosa lisilo julikana,

    nimerudi sasa nipo nae,lakini navyo ishi nae hapa ni mguu ndani mguu nje,sasa na wewe kua muangalifu sana.nakwambia ukweli mzungu si mtu wa kumuamini kwa asilimia zote.

    mda wowote wanabadilika na akibadilika ni kama vile hajawahi kukuona katiaka maisha yake.mimi naona wa kaka zetu wa nyumabni ni wazuri ila tatizo wengi wao hawana uwezo.wanamatatizo lakini si kama hawa wazungu.

    mzungu mambo ya ndugu zako hataki kusikia hata kidogo.familia kwao ni wewe na yeye kwisha kazi,kama huamini subiri utaona mda si mrefu.

    mdau
    usa

    ReplyDelete
  31. AnonymousMay 22, 2010

    Hongera dada. Ila hao wanosema kuolewa na mzungu ni afadhali wanajidanganya, kwani migogoro ya ndoa ipo dunia nzima na wanaume wote ni watoto wa baba mmoja but mzungu akikuchoka anakubebesha viragO kwa uwazi kabisa anakutimua. IN SHORT NDOA ZA KIZUNGU HAZIDUMU ILA KAMA UMEFUATA KUONDOA UMASKINI AAA HAPO UTATAKATA KIASI KAMA SIO SAAANA.

    ReplyDelete
  32. AnonymousMay 22, 2010

    Mengi ya kujifunza kutoka kwa wachangiaji wengi kama Jessica na Fatuma. Mimi ni mwanaume nimekuwa Ulaya kwa zaidi ya miaka kumi na kama kuna linalonisumbua inapokuja suala la wazungu especially one to one inakuwa ni Culture differences. Waafrika nadhani tunaonekana kama sio humans na saa nyingine kama kiingereza hakipandi inakuwa taabu. Anyway kila mtu na bahati yake na ukichukulia vumbi la nyumbani saa nyingine inabidi kujaribu. Lakini usikandie wanaume wa kibongo wengine tuko tu poa hapa na uwezo tunao.

    ReplyDelete
  33. AnonymousMay 22, 2010

    Kila mtu na experience yake. Mimi ni dume. Nime-date rangi zote - Wahindi, Wajapan, Waafrika, Wazungu, Waaborgine.... Kweli neno kuu ni CULTURAL DIFFERENCE. Kwa kweli tuna tofauti kubwa sana. Fikiria una uwezo lakini unakatazwa kusaidia ndugu zako (kama alivyosema Fatuma hapo juu). Ndugu zako na marafiki hawatakiwi kukutembelea. Na kwangu mimi ndugu na marafiki ni bora kuliko mali. Hata nikiwa billionaire bila ndugu na marafiki ni bure tu.

    Kuna hao wa Kijapan sasa. Mnakwenda kula mgahawani, kila mtu analipa hela zake. Hataki umlipie, na hataki kukulipia. Ukilazimisha kulipa ni ugomvi mkubwa. Na kama huna hela yeye anazo basi utapelekwa polisi tu yeye anaangalia tu. Yaani mapenzi yenu ni tendo la ndoa tu. Wakati mwingine ukifikiria sana mwanaume hata unashindwa kulifanya. Hakuna kabisa mazingira ya kimapenzi kati yenu. Unahisi ni mkataba tu.

    Haya ukirudi kwa hawa wa nyumbani, mapenzi unapata safi. Lakini akienda semina anawavulia wengine pia chupi. Akiwa masomoni nje ya nchi ndiyo basi kabisa..... Mpaka atashika mimba huko na kutoa au atarudi Bongo ili kukupakazia hiyo mimba.

    ReplyDelete
  34. AnonymousMay 22, 2010

    ndo ni ndoa tuu hata iwe ya mkeka,mambo meeengi heti mzungu,nae si bwana harusi tuu?hongera dada ila kaza moyo usije mmiss mwafrik.si tunajua hapo furahisha baraza tuu

    ReplyDelete
  35. AnonymousMay 23, 2010

    hongera dada

    ReplyDelete
  36. AnonymousMay 23, 2010

    Hongera dada!Mmmh Fatuma mdau USA pole sana kwa yaliokukuta,yan just 5months mzungu ameshadone with u??sooo bad!Ila mm nawapenda na ninatafuta wazungu coz nataka niwe na watoto half cast!

    ReplyDelete
  37. AnonymousMay 23, 2010

    Anonymousa May 22: 09:22 (S?
    / 1) enh?

    Hembu usitake kuchekesha SIDELINES hapa. Yaani inamaana kuwa kwako wewe utawapa kipaumbele marafiki na ndugu kuliko mtu anyekupa nanihii? IDIOT! Halafu watu msiwe wepesi kulaumu kama ambavyo nimeona watu wanamlaumu Da Sherry kuwa kwa nini kakata mawasiliano na mama yake mzazi na ndugu zake (sababu unazijua weye 1? Usingilie bifu usizozielewa!), Kwa mtindo huo watu watakula kona > 2. Lol!

    Fatuma, pole sana, ndoa inatakiwa mapenzi toka pande zote, na sio mtu kuwa kama care giver ama kumfanyia shughuli za ndani huyo mumeo. Mtaishia kutuma vi-iphone Bongo weee, but wapi!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...