Habari zilizoingia sasa hivi kutoka eneo la Mbwewe mkoani Pwani muda mfupi uliopita ni kwamba kuna ajali ya ndege ndogo ya Jeshi yenye namba 9119 ambayo imegongana na gari la watalii la kampuni ya african tours, baada ya kutua kwa dharura katika barabara kuu ya Dar-Arusha.
Habari zinasema rubani aliamua kuishusha barabarani baada ya kupata matatizo ya kiufundi wajkati ikiwa katika mruko wa kawaida wa mazoezi. Hivyo baada ya kutua barabarani ndege iliivaa gari hiyo ya watalii ambalo lilipinduka.
Inasemekana rubani ameshaondolewa ndegeni wakati juhudi zinafanywa kuondoa abiria wawili walionasa kwenye ndege hiyo hivi sasa. Hali ya rubani inasemekena ni ya kukatisha tamaa. Hakuna aliyekufa kwenye gari ya watalii.
Vikosi vya dharura vya Jeshi la Ulinzi na polisi viko eneo la tukio hivi sasa, na kipaumbele ni juhudi za kuisogeza pembeni ndege hiyo ambayo kwa sasa imeziba kabisa barabara na kusababisha foleni ndefu kila upande wa barabara hasa wa mabasi ya abiria na malori ya mizigo yanayohudumia barabara ya Dar-Arusha
Duh Bongo noma. Ajali kila sehemu, barabarani, majini, sasa ni "colabo" ndege zinaanza kugonga magari!
ReplyDeletemdau umeniacha hoi,colabo sio,duh,michuzi yani comment za humu
ReplyDeleteyep!!!that's africa anything its possible falling plane from the sky like rain kweliiii God's must be crazy in africa......waiting for falling snow..no worry in africa....edwin urasa
ReplyDeletetuleteeni picture mkiweza...
ReplyDeletemdau,
USA
Ajali za ndege kugonga magari sio kitu kipya, kwa sababu huku U.S. hutokea pilot aki lose engine, anatua kwenye highway kwa sababu airport iko mbali. Ni tukio jipya kwa huko Tanzania. Imeshatokea Texas, na hata Illinois, actually Chicago Midway Airport ambapo jet ya Southwestern ili over shoot ni kugonga fence na kusimama barabarani baada ya kugonga gari. Ni ajali, lakini sio kitu kipya.
ReplyDeleteColabo.
ReplyDeletemani umeniacha hoi
kwaa kwaaa eeh mdau umechizi ati collabo
ReplyDeleteWe Anony ndege kutua barabarani wala sio kitu kipya hapa Tanzania.
ReplyDeleteMiaka michache iliyopita ndege ndogo ilishawahi kutua barabarani Dodoma njia Kuu ya Dodoma/Dar, kilomita chache kabla ya kufika Kiwanja cha ndege cha eapot ya dodoma, lakini haikuleta madhara.
colabo!
ReplyDeleteduh!