In order to view this object you need Flash Player 9+ support!

Get Adobe Flash player
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.








  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com










uzee

Uzee kitu adhimu, huo ninauingia
Ujana sasa adimu, Shabani aliusia
Maungoni mwangu humu, uzee unanijia,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Mbali ninamuachia, rafiki yangu ujana,
Miaka inakimbia, ya leo siyo ya jana,
Nabaki nakumbukia, nilipokuwa kijana
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Shabani aliandika, kaulilia ujana,
Ni vipi unamtoka, kashindwa kuung’ang’ana,
Meno yalimdondoka, na nguvu tena hamna,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Taratibu waingia, uzee wabisha hodi,
Siwezi kuukimbia, hata niwe mkaidi
Hata nikitukania, ndivyo napigwa baridi,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee

Mvi sasa zanijia, nimejaribu kung’oa
Kidevu zasalimia, na miye nazichomoa,
Nikitoa zazidia, nami nazidi kutoa!
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Mapensi nayaachia, na macheni ya shingoni,
Hereni nilivalia, kwenye sikio jamani,
Mwendo nilibadilia, nilivyonesa njiani,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Niliwapata mademu, tena wengine kwa zamu,
Nikaitwa mtaalamu, wa mambo yale matamu
Sasa yanitoka hamu, nanyimwa hata salamu!
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Nilenda nilipotaka, wasiponitaka nilenda,
Sikuwa na hata shaka, ati mtu kunidunda,
Leo naogopa paka, ninavutwa kama punda,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Mwendo wa kudemadema, nikishika natetema,
Uso umenikunjama, natembea nikihema,
Magoti nayo yauma, uzee si lele mama!
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Kumbe maisha ni hivi, uzee haukwepeki,
Ninazikubali mvi, hata kama sizitaki,
Uzee siyo ugomvi, ujana haushikiki,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Kweli nilifurahia, enzi zile za ujana,
Kamwe sintoyarudia, yalopita naagana,
Uzee nakumbatia, kwani lingine hakuna,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Nasubiri wajukuu, nione na vitukuu,
Nakunja miguu juu, na mshukuru Mkuu
Kuona umri huu, enzi hizi ni nafuu,
Na miye nakusalimu, mgeni wangu uzee!

Na. M. M. Mwanakijiji
(Sauti ya Kijiji a.k.a Vuvuzela Matata)


Kuna Maoni 8 mpaka sasa.

  1. Anonymous Anasema:

    Mwanakijiji
    Bonge la shairi, nicheka kweli maana
    hizi mvi basi tena. Lakni wengine wanazipenda a little gray you know! U Remember BillyJean? Enzi za DarHot!!

    Vuvuzela Oyee!!

    Mdau N. America

  2. Anonymous Anasema:

    swadakta mtunzi! umeongea kweli tupu! ujana haushikiki! binafsi kila nikiufikiria uzee nahisi kuchanganyikiwa! uzee kuukubali c kazi rahisi! lkn hatuna budi kwani haubishi hodi! nilazima ukuingie upende usipende!

  3. Anonymous Anasema:

    Shair zuri tena limetulia mhh jamani uzee kila mtu anauogopa.ankal jamaa anapatikana wapi huyumwambie atutungie shairi la libeneke.vuvuzela oyee

    Yabinty

  4. Anonymous Anasema:

    Ni shairi zuri linalotukumbusha tunakotoka na tunakokwenda. Ukiweza kufikia uzee ni kweli mshukuru Mungu. Ni kweli usemavyo Mwanakijiji uzee ni kitu adimu. Nami nakusalimu kwa miaka 58 niliyofikisha karibu mgeni wangu uzee.

  5. Anonymous Anasema:

    Superb! - Bonge la shairi.

  6. Anonymous Anasema:

    Haya mashairi ndio wasanii wetu wanatakiwa waimbe kuwahamasisha watu wakubaliane na uzee, maana siku hizi bana watu hawataki kabisa uzee, hadi kwenye mavazi utakuta mmama mtu mzima kabisa lakini anapiga kimini nywele sijui zimepakwa rangi nyekundu kama yondo sister lol! ukiangalia uso unachungulia mboga iliyochacha hivyo vipedo vyake na vibukta hakuvivaa ujana wake huko, mambo ya kuiga wazungu tu sisi hatuna utamaduni huo heshimu watoto wako na vibabu kwenda disco na vibinti vidogo kama watoto wao lol! mtu mzima hovyoooooooooooo!! Mithupu rusha hiyo.

    Mdau wa Vuvuzela

  7. Anonymous Anasema:

    Wee Anon unaekandia WAZEE-FULL-KUJIACHIA.....KOMA KABISA......kila mtu ana hiari ya kuvaa anachokipenda.....KOMA KABISA....tena naona umesindilia kashwa zako zaidi kwa wakina mama.....BABA TUACHE TUZEEKE KWA RAHA ZETU.....nani avae gauni usawa huu.....kama mifweza ipo kwanini nijizeeshe bwana....I AM A PRETY YOUNG LADY IN MY LOVELY 50 YEARS OF AGE........HABARI NDIYO HII....................

  8. Anonymous Anasema:

    I agree with ano:3:15PM. Age is just a number dear. if you can handle it show it. uzee hauna maana kujiachia na kujionea huruma. Kama vitu vinatinga then viweke!!! these days 40s is the new 20s and 50s new 25s. Hey
    Go GIRL. I am in my 30s but trust me come see me in my 70s if GOD WILLING! NITAVIWEKA AS USUAL!

Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker