Kinyaunyau
Mwanamuziki mkongwe wa Kilimanjaro Band "Wana Njenje" Mabrouk Omar amepata mstuko katika enka ya mguu wake wa kushoto baada kuteleza na kuanguka kwenye ngazi za kupandia jukwaani usiku wa kuamkia leo kwenye kiota cho kipya cha maraha wanapotumbuiza siku hizi kila Jumamosi cha Salender Bridge Club maarufu siku hizi kama daraja la manyoya....Kiongozi wa bendi hiyo maarufu, Waziri Ally, kaiambia Globu ya Jamii sasa hivi kwamba Babu Njenje hivi sasa yuko nyumbani kwake akipumzika baada ya kuruhusiwa na madaktari ambao wamempima na kukuta hana madhara makubwa isipokuwa enka yake hiyo imepata mstuko katika ligamenti baada ya kuteleza na kuanguka.
"Babu Njenje hajambo na kwa kweli tunawashukuru mno wapenzi wetu kibao ambao wamekuwa wakifuatilia hali yake kwa njia ya simu ndani na nje ya nchi" amesema Waziri, akiongezea kuwa Babu Njenje hajambo na hamna haja ya kuwa na wasiwasi wote na kwamba Jumamosi ataonekana Jukwaani kama kawa hapo Salender Bridge club.
Zaidi






































































