Bi Sabina Nambalamoka (kulia) akimuuguma mama yake,Bi Kilala Magala alielazwa katika hospitali ya wilaya ya Ulanga baada ya kujeruhiwa kwenye ajari ya moto.Na Sekela Mwasubila - Ulanga
Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia na bibi yao kuungua vibaya kutokana na moto ulioteketeza nyumba yao majira ya saa nne usiku katika kijiji cha Isyaga wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro.
Akiongea na mwandishi Bi Sabina Nambamoka (35) ambaye ni mtoto wa majeruhi amewataja waliofariki kuwa ni John Makamo (9) na Edwini Kologero (5) na Bi Kilala Mgala (60) ambaye ni mama yake mzazi.
Amesema yeye anaishi kijiji cha jirani na eneo la tukio hivyo alikuja kuitwa usiku kuwa na nyumba ya mama yake inateketea kwa moto na alifika eneo la tukio alikuta moto umetanda na juhudi za kumuokoa zikiendelea, baba yake alikuwa amekwisha okolewa na alijeruhiwa kichwani na mkononi.
Aliongeza kuwa baada ya mama yake kuokolewa moto ulizidi na kupelekea watoto kupoteza maisha yao kwa kuungua vibaya na kumfikisha mama yake hospitali ya Wilaya mnamo saa tisa za usiku.
Akiongea Dkt. Malekano toka hospitali ya Wilaya ambaye ndiye anayemhudumia mgonjwa aliyejuruhiwa kwa moto huo amesema kuwa baada ya kupata matibabu hali ya mgonjwa inaendelea vizuri japokuwa ameungua asilimia sabini na tano ya mwili wake.
Mkuu wa upelelezi wa Wilaya L.N Buya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha moto ni moto uliokuwa umeachwa nje kutokana na upepo ukashika nyasi zilizoezekewa nyumba na kupelekea kuungua kwa nyumba hiyo.













































Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Bilal akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Nanyumbu baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Masasi leo
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab akimvisha skafu Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala leo mchana
Mgobea Mwenza wa urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Masasi, baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Newala, leo
Baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Newala Mkoa wa Mtwara, wakiwa katika magari kwenye msafara wa kumsindikiza Mgombea Mwenza wa nafsi ya urais, Dk Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akitoka Wilaya hiyo kuelekea Wilaya ya Masasi leo asubuhi
wananchi wa Kijiji cha Lukuledi Wilaya ya Masasi Mkoa wa Mtwara, waliojitokeza kumsikiliza mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akiwahutubia na kuwanadi wagombea Ubunge wa Jimbo la Lulindi,Bwanausi Dismas na Mariam Kasembe wa Jimbo la Masasi leo













