In order to view this object you need Flash Player 9+ support!

Get Adobe Flash player
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.










  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com












Archive for October 2010

dr. slaa akipiga kura leo

Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa akipiga kura katika kituo cha Gongali kilichopo katika kata ya Qurus wialayani Karatu mkoani Arusha mapema leo asubuhi.
Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa akipata maelezo kutoka kwa wasimamizi wa kituo cha kupigia kura cha Gongali wilayani Karatu leo.
Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Wilbroad Slaa akiwa na Mkewe Josephine,wakati wakisalimiana na wanachi wa eneo hilo mara baada ya kumaliza kupiga kura leo asubuhi.


ratiba ya kuaga mwili wa marehemu Syllersaid Mziray "Super Coach"

Marehemu Syllesaid Mziray

Habari Ndg Michuzi,

Ratiba ya kuaga mwili wa marehemu Syllersaid Mziray, "Super Coach" kwa ajili ya mazishi yake yanayotarajiwa kufanyika kesho kwenye makaburi ya Kinondoni,jijini Dar.

Taratibu hizi zitaanzia Makao Makuu ya Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania, Kinondoni Biafra kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Tutashukuru sana.

4.00 – 05.00 Kuwasili Waombolezaji

05.00 – 5.30 Viongozi, Wageni Waalikwa wa CKHT kuchukua nafasi zao.

05.30 – 6.00 Nyimbo za Maombolezo.

06.00 – 07.00 Kuwasili Mwili na Ndugu wa Marehemu.

07.00 – 07.15 Wimbo wa CKHT kupigwa.

07.15 -08.15 Misa/Sala.

08.15 – 08.20 Maelezo ya Wizara ya Michezo, Mwakilishi wa Wizara.

08.20 – 08.25 Maelezo ya TFF, Mwakilishi wa TFF.

08.25 – 08.30 Maelezo ya Simba Sport Club , Mwakilishi wa Simba.

08.30 – 08.25 Wasifu wa Marehemu CKHT .

08.35 – 08.40 Maelezo ya mwisho ya MMC VC.

08.40 – 08.45 Shukrani ya Familia,Mhusika wa Familia,

08.45 – 09.45 Kuaga mwili wa Marehemu.

10.00 – 10.05 Wimbo wa Chuo.

10.05 Kuelekea Makaburini Kinondoni


kuahirishwa kwa uchaguzi katika baadhi ya majimbo

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

YAH: KUAHIRISHA BAADHI YA CHAGUZI MBALIMBALI

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwatangazia wananchi wote kuwa katika kikao chake cha tarehe 30/10/2010 imefanya maamuzi ya kuahirisha Uchaguzi katika baadhi ya Majimbo na Kata kutokana na upungufu uliojitokeza hususan katika karatasi za kura.

Kata na Majimbo ambayo Chaguzi zake zimeahirishwa ni kama ifuatavyo:-

1. Uchaguzi wa Wabunge katika majimbo ya Nkenge, Mpanda Mjini na Mpanda vijijini.Kwa upande wa Zanzibar (Unguja) Majimbo ya Mwanakwerekwe,Mtoni na Magogoni,na Wete (Pemba)
2. Uchaguzi wa Madiwani katika kata zifuatazo:-
Na.
HALMASHAURI KATA
1 Newala DC Mtonya
2 Mbulu DC Endegikot
3 Manyoni DC Kitaraka
4 Same DC Kisiwani
5 Kibaha DC Janga
6 Rufiji (a)Kibiti
(b) Chemchem
(c) Ngorongo
(d) Kipugira
(e) Mjawa
7 Uyui DC (a)KIgwa
(b)Ibelamilundi

8 Sikonge Kisanga
9 Njombe Mji Mwema
10 Ulanga DC Msogezi
11 Karagwe DC (a) Kimuli
(b) Kamuli
12 Kasulu Kitagata
13 Chato DC Buseresere
14 Mwanza (Jiji) (a) Mkuyuni
(b) Mirongo

Hata hivyo katika majimbo hayo matatu ambapo Uchaguzi wa Wabunge umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Madiwani utanaendelea kufanyika leo kama ilivyopangwa.

Vile vile, katika Kata ambazo Uchaguzi wa Madiwani umeahirishwa, Uchaguzi wa Rais na Wabunge utaendelea kufanyika kama ilivyopangwa.

Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuwajulisha wananchi wote kuwa tarehe za kufanyika kwa chaguzi hizo itatangazwa hapo baadaye.
(Rajabu R. Kiravu)
Mkurugenzi Tume ya Taifa ya Uchaguzi


Mh. Tsere akisubiri kupiga kura

Mheshimiwa Patrick Tsere Balozi wa Tanzania nchini Malawi (wa tatu shoto) akiwa kijijini kwao, Rhotia jimbo la Karatu akiwa katika foleni na wapiga kura wengine akisubiri zamu yake ili apige kura.


In the everlasting Memory of our beloved father

Mwl. Zephaniah E. R. N. Memba

It’s already five years since you departed from us to join our father in Heaven. Your sweet and fond memories are still so vivid in our hearts and minds. Although physically you are not with us, spiritually you are in our hearts daily. Indeed you were a special gift to us from GOD. We thank the Almighty GOD for the time you spent with us. We miss you great but we always take courage and hope in the verse you left with us from Romans 8: 31 “If GOD Be For US, Who Can Be against Us?”

You are deeply missed and remembered by your wife, Mama Ukende P Memba, Your children, Joyce, Albert, Rhoda, Imani, Flora and Peter, in-laws, Maria Makalla Memba, William Stephen Kotta, Johnson Nyingi, and grandchildren, Joshua, Milan David, Nkambujah Romeo, Rodney, Ukende Ronia, Rowan Tyalambula, Rondelle and Rochelle.


JK na Mama Salma wakipiga kura leo

JK akipiga kura yake katika kituo cha kupigia kura Shule ya Msingi Msoga, kata ya Msoga,Chalinze leo asubuhi.
JK akionyesha wino uliopo katika kidole chake ikiwa ni ishara ya kuonyesha kuwa keshapiga kura leo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipiga kura katika kituo cha shule ya msingi Msoga iliopo Chalinze leo asubuhi.


dr. shein na mh. warioba wakipiga kura leo

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Dr. Ali Mohamed Shein akipiga kura kwenye kituo cha Uchaguzi Shule ya Msingi Oyesterbay jijini Dar es salaam mapema leo asubuhi.
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Joseph Sinde Warioba akipiga kura kwenye kituo cha uchaguzi Shule ya Msingi Oyesterbay jijini Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dr. Ali Mohamed Shein akisalimiana na mmoja wa Waangalizi wa Uchaguzi kutoka Visiwa vya Ushelisheli walipokutana kwenye Kituo cha Uchaguzi Shule ya Msingi Oyesterbay wakati Makamu wa Rais alipokuja kupiga kura. wa tatu kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ndg. Jordan Rugimbana akisikiliza mazungumzo hayo jijini Dar es Salaam.


U.S. Ambassador visit polling stations

U.S. Ambassador Alfonso E. Lenhardt greets a voter at the Leaders Club polling station on Sunday, October 31, 2010.
U.S. Ambassador Alfonso E. Lenhardt greets a voter at the Police Post Mzimuni polling station on Sunday, October 31, 2010


dk. salim katika zoezi la kupiga kura mjini dar leo

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dr. Salim Ahmed Salim, akipiga kura leo jijini Dar es salaam ya kumchagua Rais , Mbunge na Diwani. Dkt Salim aliwasili katika Eneo la Soko la Samaki Msasani saa 12.50 Asubuhi na kufanikiwa kupiga kura katika Kituo B 3 cha Soko la Samaki Msasani saa 1.30 Asubuhi.
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dr. Salim Ahmed Salim akisubiri Kitambulisho chake kutoka kwa Karani wakati Karani huyo akiendelea na uhakiki ili kudhibitisha kama kweli jina lake limo katika daftari la wapiga kura ili aweze kwenda kupata katarasi za majina ya wagombea ili kushiriki zoezi la upigaji kura za kumchagua Rais, Mbunge na Diwani.
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Salim Ahmed Salim, (wa pili kutoka mwisho) akiwa katika mstari unaolekea katika Chumba cha upigaji kura leo jijini Dar es salaam kwa ajili ya kushiriki zoezi la kumchagua Rais, Mbunge na Diwani.Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO.


UCHAGUZI MWEMA

LEO NDIO SIKU MAMA YA DEMOKRASIA NCHINI TANZANIA AMBAPO WANANCHI WATAPIGA KURA KUCHAGUA MADIWANI, WABUNGE NA RAIS WA KUTUONGOZA KWA MIAKA MITANO IJAYO. GLOBU YA JAMII INAWATAKIA WATANZANIA WOTE UCHAGUZI MWEMA NA WA AMANI NA ATAYEIBUKA KIDEDEA TUNAMPA PONGEZI. SHIME SHIME KILA ALIYEJIANDIKISHA KUPIGA KURA ASITUPE NAFASI HII YA KUCHAGUA VIONGOZI ANAOWAPENDA BILA KUJALI DINI AMA KABILA LA MGOMBEA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA


lala unono ya Profesa Lipumba na CUF huko Morogoro leo

Staili ya kumaliza mkutano kwa mgombea wa urais kupitia CUF, Profesa Ibrahim Lipumba , kama alivyoonesha leo mjini Morogoro kwa kusema ' kwishaaa'.. Baadaye alirejea Dar na kumalizia kampeni katika viwanja vya Mwembe Yanga
Manjonjo ya mashabiki wa CUF Wilaya ya Morogoro Mjini , wakati wa ujio wao wa Mgombea Urais, Prof Ibrahim Lipumba

Viongozi wa wanawake wa CUF ngazi ya Wilaya ya Morogoro na Taifa wakimsikiliza mgombea urais, Profesa Ibrahimu Lipumba leo
Wanachama wa CUF Wilaya ya Morogoro mjini, wakiuza skafu za chama hicho kwa wanachama na wapenzi wa CUF Mjini Morogoro leo





lala unono ya JK na CCM leo jijini Dar

JK akipanda jukwaani kwa mbwembwe huku akicheza 'kiduku' kabla ya kuhutubia mkutano wake wa mwisho wa kampeni viwanja vya jangwani jijini Dar leo
JK akimpa mkono mai waifu wake Mama Salma Kikwete baada ya kuhutubia huku mgombea mwenza Dk. Mohamed Ghalib Bilal, Katibu Mkuu wa CCM Mh. Yusuf Makamba, Makamu wa CCM (Bara) Mh. Pius Msekwa na marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mh. Benjamin Mkapa pamoja na Waziri Mkuu mstaafu Mh. Joseph Sinde Warioba wakisubiri zamu zao
Meza kuu ikimpongeza rais Mstaafu Mh. Benjamin Mkapa kwa hotuba iliyotukuka
Rais Benjamin Mkapa akihutubia
Rais Mstaafu Mh. Benjamin Mkapa akiwa na mawaziri wakuu wastaafu Dk. Salim Ahmed Salim, Mh. Joseph Sinde Warioba na Mgombea mwenza wa JK , Dk. Mohamed Ghalib Bilal
waangalizi toka ofisi ya Kimataifa ya nchi za Maziwa Makuu (ICGLR)
JK akilakiwa kwa nderemo alipowasili Jangwani
Nyomi haikuwa ya kawaida Jangwani leo
Sehemu ya nyomi ya CCM Jangwano leo


lala unono ya dk. slaa na CHADEMA jijini mbeya leo

Mgombea urais wa CHADEMA Dk. Wilbroad Slaa akihitimisha mikutano yake ya kampeni jijini Mbeya leo. Chini ni wafuasi wa chama hicho na bango lao
Aliyekuwa kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Goodluck Haule, akimakabidhi moja ya mavazi ya chama hicho mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baada ya kukihama na kujiunga na Chadema.
wafuasi wa CHADEMA katika mkutano wa mwisho wa kampeni wa mgombea urais wa chama hicho Dk. Wilbroad Slaa huko Mbeya leo
Nyomi ya CHADEMA katika mkutano huo
Dk. Slaa akihutubia umati wa wafuasi wa CHADEMA
Dr. Slaa akiondoka eneo la mkutano baada ya kuhutubia huko mbeya leo


CCM yafunga mikutano yake ya kampeni katika viwanja vya jangwani leo

JK akisalimiana na mgombea mwenza wake Dk. Mohamed Gharib Bilal wakati akishuka jukwaani baada ya kumaliza kutoa salamu kwenye hafla ya kufunga mikutano ya kampeni kwa CCM, iliyofanyika kwenye viwanja wa Jangwani jioni hii.
Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na Rais Mstaaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin Mkapa na rais Mstaafu wa awamu ya pili,Mh. Ali Hassan Mwinyi wakati alipomaliza kutoa salamu zake kwa wapenzi na wanachama wa CCM waliofurika leo katika viweanja vya Jangwani jijini Dar wakati wa hafla ya kufunga mikutano ya kampeni.
JK akisalimiana na wananchi wakati alipowasili kwenye viwanja vya Jangwani leo kwa ajili ya kufunga mikutano ya kampeni kwa CCM.
JK akisalimiana na Mjumbe wa Halmashauri kuu kwa Mkoa wa Dar es Salaam, Asha Baraka, wakati akiingia kwenye viwanja vya Jangwani leo.
Sehemu ya wanachama na wapenzi wa CCM wakiwa wamefurika katika viwanja Jangwani kuhudhulia hafla hiyo ya kufunga mikutano ya kampeni kwa CCM iliyofanyika jioni hii.


SHUKRANI

Marehemu Mchungaji Matiku Thomas Nyitambe

Familia ya Marehemu Mchungaji Matiku Thomas Nyitambe iishio Uingereza na Tanzania, kwa moyo mkunjufu, tunapenda kuchukua nafasi hii kuishukuru Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Jumuiya ya watanzania Reading na Slough ,Kanisa La wasabato (Angaza SDA Church -Reading), Madhehebu yote ya kidini hapa UK ,vyama vyote vya kisiasa,Waganga wote kutoka Mkoa wa Mara ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na pia bila kusahau blog zote zilizo shiriki kutoa taarifa(Hakingowi,Issa Michuzi,Majid Mjengwa ,TZUK,Watanzaniaoslo,Musoma -tanzania ,wavuti n.k) , kwa kufanikisha shughuli zote za msiba wa Marehemu baba yetu Mchungaji Matiku Thomas Nyitambe ambaye alifariki Kutokana na ajali ya gari tarehe 3/October /2010 na hatimaye kuzikwa tarehe 9 /October/2010 kijijini kwake Kirongwe Tarime MkoaniMara.

Tunapenda pia kutoa shukrani nyingi kwa majirani,ndugu,jamaa na marafiki kwa misaada yenu ya hali na mali ambayo imewezesha familia ya marehemu walioko Uingereza kuweza kuwahi mazishi.

Kwa kuwa ni vigumu kumshukuru kila mtu kipekee, tunasema tu kwamba Asanteni sana kwa michango yenu ya hali na mali ambayo ilisaidia katika mipango na mikakati yote ya kuuhifadhi mwili wa Marehemu hadi kuzika.

Hatuna cha kuwalipa bali tunamwomba Mwenyezi Mungu awajalie na kuwazidishia mibaraka katika shughuli zenu za kila siku.Tumeambatanisha picha za ajali .

Sisi tulimpenda sana Marehemu Nyitambe lakini

Mwenyezi Mungu amempenda zaidi,

Jina la Bwana lihimidiwe.

Asanteni sana

Amen


prof. Lipumba katika mkutano wa kampeni za lala salama morogoro

Mgombea wa Urais kupitia chana cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiwahutubia wananchi wa Manispaa ya Morogoro kwenye mkutano wake wa kampeni za lala salama mchana wa leo kabla ya kurejea Dar es Saalam kufanya mkutano wa mwisho wa kufunga kampeni za chama hicho.
Mmoja wa shabiki wa Chama cha Wananchi CUF akiingia uwanjani kwa ajili ya kumpokea Mgombea wa Urais wa Chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba ( hayupo pichani) leo siku ya mwisho wa kampeni za uchaguzi mjini Morogoro kama alivyokutwa.
Baadhi ya waangaalizi wa uchaguzi mkuu wa hapa nchini kutoka Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja walifuatilia mkutano wa kampeni ya mgombea wa Urais wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ( hayupo pichani) leo mjini Morogoro ambao ulikuwa ni kati ya mikutano yake ya mwisho kabla ya uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka huu.


Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker