WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
Kwa kushirikiana na
TAASISI YA BENJAMIN WILLIAM MKAPA HIV/AIDS

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS inatekeleza Mradi wa kuimarisha mifumo ya huduma za afya ( Health Systems Strengthening) kupitia ufadhili wa Mfuko wa Duniawa kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria - Mzunguko wa 9 ( Global Fund Round 9).  Baadhi ya malengo ya mradi  ni pamoja na; kuongeza wataalam wa afya, ili kuimarisha huduma za UKIMWI, Kifua Kikuu, Malaria na huduma nyinginezo, katika Halmashauri zilizopo maeneo yenye uhaba mkubwa wa watumishi kutokana na changamoto ya mazingira yake.

Baadhi ya malengo ya mradi  ni pamoja na kuimarisha uwezo wa vyuo vya mafunzo ya afya, kwa kuvipatia wakufunzi zaidi, ili kuhakikisha kuwa uzalishaji wa wataalam wa afya unaongezeka zaidi nchini. Katika kutekeleza azma hii, BMAF wanatoa tangazo la nafasi za kazi kwa waalimu 137 wa vyuo vya Afya,  kama ifuatavyo:

    1. KANDA YA KATI (CENTRAL ZONE)
CHUO KADA IDADI
  1. MIREMBE School of  Nursing 
Nurse Tutors 4
  1. ST. GASPAR School of  Nursing 
Nurse Tutors 5
  1. KANDA YA MASHARIKI (EASTERN ZONE)
  1. KIBAHA Clinical Officers Training Centre (COTC)
Medical Doctors Assistant Medical Officers (AMO) 4 3
  1. KILOSA Clinical Officers Training Centre
Medical Doctors Asst Medical Officer (AMO) 4 2
  1. KANDA YA ZIWA ( LAKE ZONE )
  1. Bugando Asst Medical Officers Training Institute (AMOTIC)
Medical Doctors Medical Specialist 4 1
  1. KOLANDOTO School of  Nursing 
Nurse Tutors 6
  1. MUSOMA Clinical Assistants Training Centre (CATC)
Medical Doctors Asst Medical Officers (AMO)
2 3
  1. NDOLAGE School of  Nursing 
Nurse Tutors 5
  1. RUBYA School of  Nursing 
Nurse Tutors 3
  1. SENGEREMA School of Nursing 
Nurse Tutors 6
  1. KANDA YA KASKAZINI (NORTHERN ZONE)
  1. HAYDOM School of  Nursing 
Nurse Tutors 4
  1. HURUMA School of  Nursing 
Nurse Tutors 5
  1. KCMC Asst. Medical Officer Training Centre
Medical Doctors Specialists 4 2
  1. KCMC School of  Nursing 
Nurse Tutors 5
  1. KIBOSHO School of  Nursing 
Nurse Tutors 3
  1. MUHEZA School of  Nursing 
Nurse Tutors 4
  1. TANGA Dental Therapist School
Dental Surgeons 2
  1. TANGA Asst. Medical Officer Training Centre
Medical Doctors 3
  1. TANGA School of  Nursing 
Nurse Tutors 3
  1. KANDA YA KUSINI (SOUTHERN ZONE)
  1. LINDI Clinical Officer Training Centre
Medical Doctors 6
  1. MASASI Clinical Asst Training Centre
Medical Doctors 1
  1. MASASI Clinical Asst Training Centre
Asst Medical Officers 2
  1. MTWARA Clinical Asst Training Centre
Medical Doctors 6
  1. NDANDA School of  Nursing 
Nurse Tutors 2
  1. NEWALA School of  Nursing 
Nurse Tutors 3
  1. NYANDA ZA JUU KUSINI (SOUTHERN HIGHLANDS )
  1. ILEMBULA School of  Nursing 
Nurse Tutors 2
  1. MAFINGA Clinical Officer Training Centre
Medical Doctors 4
  1. PERAMIHO School of Nursing 
Nurse Tutors 6
  1. NYANDA ZA JUU KUSINI MAGHARIBI (SOUTHERN WESTERN HIGHLAND)
  1. Mbeya Asst Medical Officer Training Centre
Medical Doctors 3
  1. SONGEA Clinical Asst. Training Centre
Medical Doctor 1
  1. SUMBAWANGA Clinical Asst. Training Centre
Medical Doctor Asst. Medical Officers 2 3
  1. KANDA YA MAGHARIBI (WESTERN ZONE)
  1. KABANGA School of  Nursing 
Nurse Tutors  3
  1. KIGOMA Clinical Asst Training Centre
Medical Doctors 2
  1. NKINGA School of  Nursing 
Nurse Tutors 4
                                                Jumla     137
Izingatiwe kwamba:
  • Ajira ndani ya mradi huu itatolewa kwa mkataba wa miaka miwili. Kwa wale wote watakaofanikiwa kumaliza vipindi vyao vya mikataba, wataajiriwa katika utumishi wa umma.
  • Watumishi waliopo katika ajira ya utumishi wa umma au katika Taasisi/Vyuo vya mashirika ya dini (FBOs) hawaruhusiwi kuomba nafasi hizi.
  • Mishahara itatolewa kwa mujibu wa Waraka wa Maendeleo ya Utumishi Na. 1 wa mwaka 2009 kulingana na sifa na ujuzi wa mtumishi husika pamoja na maslahi mengineyo yaliyobainishwa katika mradi.
  • Kwa taratibu za Serikali, wataalamu wenye umri chini ya miaka 45 wanashauriwa kuomba zaidi, na watakuwa na fursa kubwa ya ajira yao kuingia serikalini kwa masharti ya kudumu na pensheni. Kwa wataalamu wenye umri zaidi ya miaka 45 au waliostaafu, maombi yao pia yatashughulikiwa na ajira ya serikali itakuwa kwa mkataba.
  Maombi yote yaambatanishwe na:
  1. Barua ya maombi ya kazi, ikipendekeza Halmashauri 3 mwombaji anayopendelea kupangwa kazi, na pia aonyesha  ridhaa ya kujiunga na utumishi wa umma, baada ya mkataba wa miaka miwili kumalizika.
  2. Nakala ya cheti cha Taaluma na cheti cha kidato cha 4 pamoja na cha 6 (iwapo anacho), na viwe vimethibitishwa na Hakimu au Wakili.
  1. Picha mbili (2) – saizi ya Pasipoti  na maelezo binafsi (CV), ikionyesha umri, anuani kamili na namba ya simu ya kiganjani, pamoja na  anuani/ namba ya kiganjani ya wadhamini wako.
Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe 15 Juni 2011 
Maombi yote   yatumwe kwa:
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, S.L.P. 9083, DAR ES SALAAM. 
Tangazo hili linapatikana pia katika tovuti za:



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...