Mmoja wa Viongozi wa Tume ya Taifa ya Unesco, ( wapili kushoto aliyesimama) akitoa maelezo juu ya matumizi ya vifaa vya kufundishia somo la sayansi kwa wanafunzi wa shule mbili za  Msingi  katika Manispaa ya Morogoro, zilizoingizwa kwenye mpango wa kuhamasisha wanafunzi hao kuvutiwa na masomo ya sayansi,( wapili kushoto walioketi) ni Katibu Mtendaji wa UNESCO , Profesa Elizabeth Kiondo.

 Wanafunzi wa shule mbili za  Msingi  katika Manispaa ya Morogoro, Solomoni Mahlangu na Kigurunyembe ,ambazo zimeingizwa kwenye mpango wa mradi wa kuhamasisha  wanafunzi hao kuvutiwa na masomo ya sayansi,wakiwa katika picha ya pamoja na nje ya ukumbi baada ya kuzinduliwa kwa mpango wa mradi wa kuhamasisha wanafunzi katika shule za Msingi kuvutiwa na masomo ya Sayansi , Mradi huo unasimamiwa na UNESCO na kuendeshwa katika Mikoa sita ya Tanzania, ambayo ni Zanzibar, Arusha, Kilimanjaaro, Pwani, Dar es Salaam na Morogoro

Baadhi ya wanafunzi wa shule mbili za  Msingi  katika Manispaa ya Morogoro, ambazo ni Solomoni Mahlangu na Kigurunyembe , zilizoingizwa kwenye mpango wa kuhamasisha wanafunzi hao kuvutiwa na masomo ya sayansi,wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi baada ya kuzinduliwa kwa mpango wa kuhamasisha wanafunzi katika shule za Msingi kuvutiwa na masomo ya Sayansi , Mradi huo unasimamiwa na UNESCO na kuendeshwa katika Mikoa sita ya Tanzania. Picha na John Nditi


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Haya ndio mawazo mazuri ya kujitoa kwenye shida na umaskini ktk nyanja za teknologia,ila tuwaendeleze hawa vijana kwenye nafasi za kitaifa ili angalau waje kutusaidia baadaye.
    Wapewe kipaumbele na serikali kuu kwa gharama zozote.Tuige mifano ya nchi zilizoendelea,kwa mfano NASA wanawaandaa watoto from low level mpaka wanamaliza elimu ya juu.
    Tuache kuwashirikisha wasomi na siasa, tunapoteza wataalamu wengi(vichwa).

    ReplyDelete
  2. Sasa nimeelewa kwa nini watu wanajazana mijini. Lini tutapeleka huduma vijijini?. Na hayo mashangingi ya DFP ni ya kutelezea taun tuu?. Tukumbuke wenzetu swekeni(!) tafadhali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...