





Archive for April 2011
Wizi uliotukuka Mlimani City...
DR. SHEIN AENDELEA NA ZIARA YAKE NCHINI UTURUKI
Faraja Kihongole na Projestus Rwegarulila wameremeta leo
Mwandishi mwandamizi wa kituo cha Televisheni cha Channel 10, Da' Faraja Kihongole akiwa na akiwa amepozi na mume wake, Projestus Rwegarulila baada ya kumeremeta leo Alasiri katika Kanisa la St. Peter Oysterbay jijini Dar es Salaam.msaada tutani
Mimi ninashida na anuani ya ubalozi wa Tanzania, Bangkok, Thailand. Nilijaribu kutafuta katika mtandao (Google) na nikapata anuani hii (Tanzania Honorary Consulate , Thailand, S.L.D. Condominium, 3rdFL., 501 Saladaeng 1, Rama IV Road,Bangkok10500,Thailand,
Nilipofuatilia ubalozi katika anuani hiyo hapo nilipewa maelezo kwamba walishahama miaka 10 iliyopita! Sikukata tamaa na niliamua kuwapigia simu. Simu ikapokelewa na nikajibiwa kwamba hiyo line kwasasa inatumiwa na ubalozi wa New Zealand.
Kaka Michuzi, nimeamua nije hapa kwenye kwenye blogu ya jamii kwani inatembelewa na watu mbalimbali labda kuna mmoja wa wapenzi wa blogu hii anawezakua anafahamu anuani ya ubalozi wa heshima wa Tanzania kule Bangkok, Thailand.
Ombi langu ni kwamba, wadau wa libeneke (blogu ya jamii) tafadhari kama kuna mtu anafahamu anuani au hata namba ya simu nitapenda kufahamishwa! Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Kwa yeyote mwenye anuani hiyo au namba ya simu ya mtu anaeshughurikia masuala ya kibalozi, Bangkok, tafadhari usisite kunifahamisha kwa kutumia barua pepe 52910601@st.kmutt.ac.th
Asanteni sana wadau wa blogu ya jamii.
Mdau wa blogu ya jamii.
JK awaapisha makatibu wakuu wa wizara leo
BOFYA HAPA
kuona picha zaidi.
VODACOM MISS TZ YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR



kwa picha zaidi
BOFYA HAPA

msaada tutani
Huyu jamaa tulikua tunamwita KC KABETA (Bahati mbaya sikumbuki jina lake kamili) huyu jamaa alikua maarufu saana pale sinza wazazi (iteba). Yeye kipindi hicho alikua anatokea Mburahati.
Uncle Michuzi mimi ni Mjasiria mali niliyepo huku Ughaibuni kwa sasa nataka nifungue kijimtego (Kitega uchumi) hapo Dar es salaam japo kiweze kunisaidia kujikwamua matatizo madogo madogo hapo nyumbani.
Kutokana na tabia za kijitega uchumi hiki kitafaa saaana na naamini kitaenda vyema kikiwa mikononi mwa huyu rafiki yangu KC KABETA, jamaa kwa jinsi alivyo nimependezewa niweke hiki kijitega uchumi mikononi mwake ingawa ni mda mrefu hatujawasiliana na sijui anaendelea vipi na yuko wapi naamini rafiki yangu KC KABETA atanisaidia saana kwani ana sifa zinazoendana na hiki kijitega uchumi.
KC KABETA popote ulipo usomapo ujumbe huu tafadhari tuwasiliane kaka, Ni muhimu saana.
Yeyote anaye mfahamu KC KABETA tafadhari naomba anisaidie ni vipi nitampata.
KC KABETA naomba tuwasiliane kwa email yangu hii
nimimi20@yahoo.com
Asante saana Uncle Michuzi,
Mjasiliamali wa Ughaibuni.
mji wa bukoba unavyoonekana leo
Soko kuu la Mji wa Bukoba linavyoonekana leo.
Mitaa ya katikati ya mji wa Bukoba.WAFANYAKAZI IDARA YA HABARI (MAELEZO) WAMUAGA RASMI MKURUGENZI CLEMENT MSHANA
Rais wa UNDER THE SAME SUN atembelea shule ya msingi Mugeza Mseto Wilayani Bukoba
TWANGA KUWASUGULUSHA KISIGINO VIMWANA WA TWANGA PEPETA MANGO GARDEN.
Sugua Kisigino ni mtindo unaotumiwa na Twanga Pepeta na ni moja ya staili zitakazotumika kwenye shindano hilo, hivyo washiriki watatumia fursa hiyo ili kufahamu jinsi ya kucheza staili hiyo.
Washiriki watatumia onyesho hilo ili kusalimu mashabiki wa Mango Garden ukumbi ambao una historia ndefu na Twanga Pepeta.
Onyesho rasmi la utambulisho wa Vimwana wa Twanga Pepeta 2011 unatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 06-05-2011 ndani ya Club ya Sun Cirro iliyoko Sinza na Fainali itakuwa Ijumaa tarehe 03-06-2011.
Burudani ya Utambulisho wa Shindano la Kimwana wa Twanga Pepeta 2011 itatolewa na Wakali wa Dansi Tanzania, African Stars Band “Twanga Pepeta” na Msanii Abbas Kinzasa maarufu kama 20 percent au asilimia ishirini, pamoja na shoo kali ya Nyonga teketeke ya Vimwana wa Twanga Pepeta.
MAIMARTHA JESSE
MRATIBU WA SHINDANO.
mwali wa zanzibar soccer bonanza afichuliwa rasmi

WASHIRIKI NI ZANZIBAR SERENA INN, THE RESIDENCE, ZANTEL, THE MONIVARO GROUP, FISHERMAN TOURS NA ZAMANI KEMPINSKI. BONANZA LIANZA SAA MBILI ASUBUHI MPAKA SAA TISA MCHANA.
TUNATARAJIA BONANZA LILATAKOLO KUWA NA HAMASA KUBWA NA KUACHA GUMZO ZANZIBAR, LIKISINDIKIZWA NA MUZIKI MKUBWA
KAMA WEWE MPENDA SOKA NJOO USHUHUDIE VIPAJI VILIVYOJIFICHA KWENYE HII SEKTA USIACHE KUMWAMBIA MWENZAKO KWANI HATAKUPENDA TENA AKIKOSA KUWEPO.
Charles Kisaka
Assistant Front Office Manager
Zanzibar Serena Inn
Zanzibar
NEWS ALERT: MDAU MWEMA AMNUNULIA WHEELCHAIR KIJANA MLEMAVU YOHANA BENJAMIN
Wheelchair mdau aliyojitolea kumnunulia kijana mlemavu Yohana Benjamin aliyeomba msaada tutani katika Globu ya Jamii majuzi (BOFYA HAPA). Mdau mwema huyu kaomba jina na bei ya wheelchair tuweke kapuni.Asante sana kwa kazi nzuri.
UFAFANUZI WA KAULI YA KATIBU WA BUNGE KUHUSU UELEWA WA KANUNI KWA WABUNGE WAPYA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tarehe 27 Aprili, 2011, Katibu wa Bunge, Dr. Thomas D. Kashililah alizunguza na vyombo vya habari kuhusu masuala makuu matatu:-
1. Utaratibu wa kutunga sheria Bungeni kwa mambo ya jumla
2. Mamlaka ya Spika katika Kazi za Bunge
3. Mwenendo wa Bunge la Kumi hasa Mkutano wa Tatu
Katika maelezo yake Katibu wa Bunge alitoa ufafanuzi wa kina juu ya namna mchakato wa Muswada wa Marekebisho ya Katiba na matumizi ya hati ya dharura (Certificate of Urgency).
Aidha, Katibu wa Bunge pia alifafanua mamlaka ya Spika katika Kazi za Bunge kwa kueleza kuwa katika kazi zake Spika anaongozwa na Kanuni za Bunge ambazo zinampa fursa ya kutoa adhabu kwa Wabunge ambao wanavunja Kanuni au kuonesha vitendo visivyostahili Bungeni na kusababisha uvunjifu wa amani na utulivu Bungeni.
Katika hilo na kuzungumza yaliyojiri katika Mkutano wa Tatu, Katibu wa Bunge alieleza kuwa Spika pia kwa kutambua kuwa wengi wa Waheshimiwa Wabunge ni wapya (asilimia 69 ya Wabunge wa sasa) ambao hawana uzoefu wa mambo ya Bunge, hutumia busara katika maamuzi yake kwa kuwa kutokana na ugeni wao, Wabunge hao bado hawajawa na uelewa mpana wa Kanuni na hivyo lililo muhimu sio kutoa adhabu bali kutoa elimu na kuwaelekeza wanapotenda/kutoa kauli sizo.
Aidha, ni kwa kuzingatia hilo, Ofisi ya Bunge iliandaa semina mbili elekezi zilizofanyika Jijini Dar es Salaam na pia kugharamia semina za vyama vikuu Bungeni – Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyofanyika Dar es Salaam na semina ya Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyofanyika Bagamoyo, mkoani Pwani.
Ofisi ya Bunge imesikitishwa na taarifa potofu zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Katibu wa Bunge amewaita Waheshimiwa Wabunge “mbumbumbu” neno ambalo halikutumika katika mazungumzo.
Ofisi ya Bunge inatambua na kuheshimu kwa kiasi kikubwa elimu na taaluma za Waheshimiwa Wabunge na hili halikuwa sehemu ya mazungumzo na waandishi wa habari.
Ofisi ya Bunge inaheshimu na kuzingatia uhuru wa vyombo vya habari katika kufanya kazi yao lakini inasisitiza kuwa uhuru huo usitafsiriwe kama ni fursa ya kuchonganisha pande mbalimbali katika jamii. Kupachika neno “mbumbumbu” kama kielelezo cha Wabunge kupewa muda wa kuzielewa Kanuni ni upotoshaji mkubwa wa maudhui ya aliyozungumza Katibu wa Bunge ambao hauna lengo jema.
Ofisi ya Bunge inatoa wito kwa waandishi kuzingatia maadili na miiko ya kazi zao wanapotekeleza kazi zao hasa habari za Bunge na Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi.
Imetolewa Ijumaa tarehe 29 Aprili, 2011 na:-
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma
na Ushirikiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge
S. L. P. 9133
DAR ES SALAAM.
TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA UWEKEZAJI
mdau timoth albert apata kipaimala
BUSTA RHYMES TO HEADLINE BIG BROTHER AMPLIFIED OPENING SHOW!

The news is official and it’s big!
Iconic hip hop superstar Busta Rhymes will headline the two-hour launch show for M-Net’s BIG BROTHER AMPLIFIED when it kicks off on DStv on Sunday May 1 at 20:00. The legendary performer is jetting into Johannesburg this weekend to perform on the Big Brother stage on a night when the continent will meet the new Big Brother housemates!
Busta Rhymes has been setting the standard as a rapper and hip-hop icon, having collaborated with stars such as Diddy, Pharrell, Janet Jackson, Chris Brown & Lil Wayne, including featuring on Tiësto and Diplo track "C'mon (Catch 'Em By Surprise). He has also made several appearances on the big screen including roles on Shaft, Finding Forrester and Halloween Resurrection. His 2006 album, The Big Bang, debuted at No. 1 on the Billboard Top 200 album chart. Seen by many as a living legend, the artist most recently formed his own record label, The Conglomerate, which he partnered with his artist , J Doe and Reek the Villain on the soon to be released movie soundtrack of the Fast & Furious 5 “This is How We Roll” (remix). Busta Rhymes continues to cement his position in the industry as one of the most undeniable performers of all time!
M-Net’s BIG BROTHER AMPLIFIED starts on DStv channel 198 on Sunday May 1. The series is available 24/7 to DStv Premium, Compact Plus and Compact subscribers. The series is headline sponsored by Coca-Cola and produced for M-Net by Endemol South Africa. BIG BROTHER AMPLIFIED will also be available on DStv Mobile in Ghana, Kenya, Namibia and Nigeria.
PLUS in other exciting news…last night (Thursday April 28), the official BIG BROTHER AMPLIFIED website (www.mnetafrica.com/bigbrother
BROTHER AMPLIFIED housemates
going into the house on Sunday. They are:
TV broadcaster Bhoke from Tanzania (26)
Nightclub manager Confidence from Ghana (37)
Singer and student Hanni from Ethiopia (22)
Rapper and Radio host Herminio from Mozambique (32)
Recording Artist and Marketing/Sales manager Jossy from Namibia (28)
Radio and Club DJ Lomwe from Malawi (27)
Actor and acting coach Luclay from South Africa (28)
Actress Millicent from Kenya (28)
Radio DJ Mumba from Zambia (24)
Artist and Musician Sharon O from Uganda (25)
Model Vimbai from Zimbabwe (24)
Radio Presenter Vina from Nigeria (26)
TV Presenter and Model Weza from Angola (26)
Entrepreneur, artist and marketer Zeus from Botswana (24)
So remember to tune in on Sunday May 1 at 20:00 ,
DStv channel 198!
balozi kallaghe akiwasili harusini
mnuso seattle jumamosi hii

================= NJOO TUSELEBUKE ==============
kumbukumbu

MAREHEMU MWALIMU MUNGUATOSHA KALEBI TEMU
(1923-2010)
Leo tarehe 29/04/2011 umetimia mwaka mmoja tangu Mungu alipomuita baba yetu katika makao ya milele. Japo hayupo pamoja nasi kimwili, lakini bado yuko nasi mioyoni mwetu. Tunakumbuka upendo, ukarimu na ucheshi wake, pamoja na mafundisho, maonyo na maelekezo aliyokuwa akitupa. Tunamshukuru Mungu kwa uvumilivu na ujasiri aliotupa tangu baba alipotutoka.
Unaendela kukumbukwa na mke wako Santa, watoto wako na wenzi wao, dada zako, mdogo wako, shemeji zako, wajukuu, vitukuu, marafiki na wanaukoo wote.
“BWANA ALITOA NA BWANA AMETWA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE”
Moshi wazindua mradi wa hifadhi mazingira
ratiba ya msiba wa leicester na tanzania

Assalaam Alaikum,
Inna lillahi wa inna ilaihi raajiuun. Jumuiya ya Watanzania Leicester, Uingereza inasikitika kutangaza kifo cha ndugu yao, Sheikh Ali Salmin Jaha, kilichotokea tarehe 27 Aprili 2011. Maiti itaswaliwa saa kumi na moja na nusu jioni (5.30 pm) Leicester Central Mosque, Conduit Street, LE2 OJN. Karibu na train station.
Mwili wa marehemu utasafirishwa siku ya jumamosi tarehe 30 Aprili 2011 kuelekea Dar es salaam inshaAllah na pia mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya jumaapili tarehe 1 may 2011
Kwa yeyote mwenye mchango wake wa hali na mali awasiliane nasi kwa namba zifuatazo:
Namba za simu : Suwedi Abdallah +447796080601
Salim Awadh +447949421087
Rashid Saadallah +447896916032
mama bishanga ameremeta



washiriki wa Big Brother amplified inayoanza jumapili
Watch Online from Anywhere
So whether you’re watching online or whether you are watching on DStv, make sure you don’t miss the start ofBig Brother Amplified.
























































