In order to view this object you need Flash Player 9+ support!

Get Adobe Flash player
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.










  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com












Archive for August 2011

JK atembelea majeruhi wa ajali, ahutubia baraza la Iddi Dodoma

 Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Bi. Ashura Kassala, mkazi wa Manzese jijini Dar es Salaam aliyelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma kufuatia kupata majeraha makubwa kutokana na ajali ya basi La Champion lililopata ajali juzi mkoani Dodoma.Rais Kikwete alikwenda kuwapa pole majeruhi hao baada ya kulihutubia baraza la Iddi lililofanyika  katika msikiti wa Gaddafi mkoani Dodoma.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Bwana Winston Chinduge mkazi wa Gairo,mkoani Morogoro ambaye ni mmoja wa majeruhi wa Basi la Champion lililopata ajali juzi mkoani Dodoma.Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia baraza la Iddi lililofanyika katika msikiti wa Gadaffi mjini Dodoma leo jioni
Sheikh Mkuu  na mufti wa Tanzania Issa bin Shabaan Simba akipeana mikono na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa Baraza la Iddi lililofanyika katika msikiti wa Gaddafi Mkoani Dodoma. Picha zote na mdau Freddy Maro wa Ikulu


MAKAMU WA RAIS KATIKA SWALA YA EID EL FITR VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum, wajumuika pamoja na waumini wa dini ya kiislamu kuswali swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
Immam Mkuu wa Msikiti wa Manyema jijini Dar es Salaam, Masoud Mohamed Jongo, akitoa mawaidha baada ya swala ya Eid El-Fitr iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Ibrahim Lipumba (kushoto), wakiwa katika swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El- Fitr, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo .
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Ibrahim Lipumba, baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El-Fitr leo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR


Salamu za Iddi toka kwa kijasti bikozi




heri ya idd wadau.
haya, watu wa man u furahini.ofkozi mimi 
pia ni arsenal lakini kwa sasa nipo kwa mkopo man city


Mdau Kijasti


SALAM ZA EID MUBARAK TOKA SWEDEN

TUNAMSHUKURU MWENYEZI MUNGU KWA KUMALIZA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI SALAMA.

SASA NI WAKATI WA KUSHEREHEKEA EID PAMOJA.JUMAMOSI TAREHE 3.9.2011 SAA TISA MCHANA (15.00 HRS) T-ALVIK(ALVIK MEDBORGAHUS)-GUSTAVSLUNSVÄGN 168 A 2TR,UKUMBI ;NOCKEBYSALEN.

TAFADHALI WATAARIFU NA WENGINE.


Swala ya Iddi Zanzibar leo

 Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohd Shein akiwahutubia viongozi na wananchi mbalimbali hawapo pichani katika ukumbi wa salama Holl Bwawani zanzibar baada ya kumalizika kwa mfungo wa Ramadhani.
 Naibu mufti wa Zanzibar Sheikh Swaleh Omar Kaabi akimkaribisha Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kuhutubia katika Baraza la Idi ambalo lilifanyika  katika ukumbi wa Salama Holl Bwawani mjini Zanzibar.
 Umati katika Swala ya Iddi uwanja wa Maisara
 Baadhi ya kinamama waliohudhuria katika swala ya Idi Elfitri huko katika kiwanja cha Maisara mjini Zanzibar
 Rais wa Zanzibar Alhaji Dr,Ali Mohd Shein pamoja na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali  na wananchi,wakiwa katika swala ya iddi ambayo imeswaliwa kitaifa katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar Alhaji Dr,Ali Mohd Shein pamoja na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali  na wananchi,wakiwa katika swala ya iddi ambayo imeswaliwa kitaifa katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar.
 Rais wa zanziba Dr Ali Mohd Shein akisalimiana na Rais Mstaafu Mh. Amani Abeid Karume  katika kiwanja cha Maisara mjini zanzibar kwa ajili ya kuswali swala ya Idi Elfitri.
 Makamo wa kwanza wa Rais Seif Sharif Hamadi akisalimiana na Waziri wa katiba  na Sheria wa Zanzibar Abubakari Khamis Bakari baada ya kuingia katika kiwanja cha maisara mjini zanzibar kwa ajili ya kuswali swala ya Idi Elfitri.
Rais mtaafu wa Zanzibar Amani Abeid Karume akisalimiana na Waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar Abubakari khamis Bakari baada ya kuingia katika kiwanja cha maisara mjini zanzibar kwa ajili ya kuswali swala ya Idi Elfitri.
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI MAELEZO ZANZIBAR

Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi M, Al Hajj Dk Ali Mohamed Shein amesema Serikali imeandaa mipango kuhakikisha inaongeza fursa zaidi za ajira rasmi na zisizo rasmi Visiwani Zanzibar.

Akihutubia Baraza la Eid-El-Fitri Mjini hapa jana, Dk Shein alisema katika mwaka wa Fedha 2011/2012 Serikali inatarajia kuajiri watu 2,476 kulingana na mahitaji na uwezo uliopo.

“Tunaelewa kuwa mahitaji ya fursa hizo ni makubwa zaidi…katika kukabiliana na uhaba wa fursa za ajira, Serikali inashajiisha wananchi kujiunga katika vikundi vya Ushirika ili waweze kunufaika” Alisema Rais Dk Shein.

Dk Shein alisema kuwa mkazo umewekwa katika kuvisaidia vikundi vya uzalishaji mali vinavyoanzishwa na vijana na wanawake ili waweze kujiajiri wenyewe wajiongezee kipato na kupambana na umaskini.

Akizungumzia mwezi mtukufu wa Ramadhan, Rais Dk Shein aliwakumbusha waumini wa Dini ya Kiislamu na wananchi wote nchini kuitumia elimu waliyoipata katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani kuimarisha mwenendo mwema na kujenga maisha bora ya duniani na akhera.

Dk Shein alisema suala la kudumisha amani, umoja na kuheshimiana miongoni mwa waislamu na wale wa dini nyengine kumewezesha kuendesha ibada hiyo katika hali ya amani na utulivu.

Alisema kwamba kuendeleza mwenendo mwema na kujiepusha na vishawishi vinavyoweza kuleta matatizo na kusisitiza suala la kujenga uadilifu hasa katika sehemu za kazi kwa wafanyakazi kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Sherehe hizo zilitanguliwa na swala ya Iddi iliyofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja na kuhudhuriwa na Makamu wa kwanza wa Rais, Seif Shariff Hamad, Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Idd na viongozi wengine wa Serikali, Dini na Vyama vya siasa.


JK na Dkt Bilal katika swala ya Iddi el Fitr jijini Dar es salaam leo

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimu waumini waliohudhuria swala ya Iddi katika msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wakiswali swala ya Iddi katika msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni mapipa jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwapa mkono wa Iddi baadhi ya waumini waliohudhuria swala ya Iddi katika msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni Mapipa jijini Dar es Salaam leo asubuhi(picha na Freddy Maro)



:- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Ibrahim Lipumba, baada ya kumalizika kwa Swala ya Eid El-Fitr leo viwanja vya |Bustani ya Mnazi Moja jijini Dar es salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa Swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo

Imamu Mkuu wa Msikiti wa Manyema jijini Dar es Salaam, Sheikh  Masoud Mohamed Jongo,  akiswalisha jamaa katika  swala ya Eid El-Fitr iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa pili kulia) Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (kulia), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Alhad Salum, wajumuika pamoja na waumini wa dini ya kiislamu kuswali swala ya Eid El-Fitr, iliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo


REMINDER: 1 Day left .....2011 DICOTA....


YOU have only 1 day left to take advantage of $99.00 early registration fee for this year's DICOTA Convention!!!!! It will be $190 from Sept 1st to Sept 20th when doors will be closed.

Few Highlights for this Year's Convention includes (but not limited to):
  • Investments Opportunities and Role of the Diaspora: Learn what role does National Social Security Fund (NSSF), Tanzania Investment Center (TIC), Z'Bar Investment Promotion Agency (ZIPA), Tanzania Revenue Authority (TRA) plays to facilitate engagement and participation in development in Tanzania. Learn how you can utilize Diaspora Desk in our Foreign Affairs & International Cooperation Office.
  • Have a clear understanding on the Role of Central Bank (BOT) and other Commercial Banks in facilitating effective Diaspora Remittances and Providing Capital for Investments. Key figures from BOT, Stanbic Bank Tanzania, CRDB Bank and National Housing Corporation (NHC) to name a few will engage in panel discussion and presentations.
  • USA vs Tanzania Bilateral relations: Familiarize yourself with Millennium Challenge Corporation (MCC) grant and what it has achieved in building Tanzania's infrastructure. 
  • Loan Financing Small and Medium Scale Economic Projects Opportunities for Diaspora?: International Finance Corporation (IFC) World Bank Group will be sending their Country Lead on the subject.
  • Diaspora Access to Land?: The Who Is Who panelist: Mr. Kyando Mchechu-NHC Director General, Dr. Ramadhani Dau-NSSF Director General, Nyumba Poa Ltd Director Mr Peter Malika, to name a few will quest our thirst on the subject. Permanent Secretary Ministry of Land and Housing Development (Ardhi) will present Government plans to assist Diaspora in accessing land in Tanzania.
  • Ever wonder about Employment Opportunities and Challenges for Diaspora Skills Engagement? Radar Recruit CEO will do a presentation on this...and Yes please, BRING YOUR RESUMES!!
  • Do YOU: DICOTA has set aside half a day on Sept 25th for Networking and Job Interviews !
  • Long weekend? How about Maasai BBQ @ the Park, Soccer Bonanza featuring sharp skills from H-Town, TX; Twin Cities, MN; Seattle, WA; City of Angles, CA; the host Washington DC and off course Wichita, KS
  • Stay Sharp for that 50 Years Uhuru Gala Dinner featuring Kilimanjaro Band-Wananjenje,Maestro King Kiki himself; Jahazi Modern Taarab and the talented Asia Idarius and her Tanzania Mitindo House.
To take advantage of early registration,  please visit www.dicotaus.org while there, we encourage you to access different links to familiarize yourself about DICOTA.

See you in Washington DC, this Sept 22nd-25th.


ARSENAL YASAJILI MSHAMBULIAJI MPYA

Ankal,

Pole kwa mashabiki wa Arsenal. Habari zilizopo kwenye libeneke la klabu hiyo ya Uingereza zinasema uongozi wa klabu umepanga kuwapoza mashabiki wake waliosafiri kuenda kuipa sapoti timu yao uwanja wa Old Traffod, mpango wa kuwapooza utajumuisha kuwalipa gharama za tiketi walizokata siku hiyo timu yao iliponyukwa mabao 8 kwa 2.

Habari njema ni kuwa Mzee Wenger, anajipanga kurekebisha makosa na tayari amekwisha msajili mshambuliaji, kepteni wa timu ya Taifa ya Korea Kusini, CHU YOUNG PARK anayetokea AS MONACO ya Ufaransa. Chu Young Park, mwenye umri wa miaka 26, atakuwa akivaa jezi namba 9 akiwa na washika bunduki hao wa London.

Mdau John.


salamu za Iddi Mubarak toka sauzi

Ankal, nakutakia sikukuu njema ya Idd wewe, 
familia yako na wadau wote wa blogu ya jamii.
Ni kuwajuza tuu kuwa hapa Sauzi sikukuu za kiislamu kama Idd El Fitr, Idd El Haj na Maulid hazijajumuishwa kwenye sikukuu za kitaifa. Ni kama leo, tupo kwa job tunawajabika.Yaani kwa kifupi, shule na ofisi zote za serikali na binafsi shughuli zinaendelea kama kawaida.
Ila kwa wale waislamu, wanaruhusiwa kutokufika kwa ofisi na wakaendelea kusherehekea kwa namna zao, mfano hapa job kwangu waislamu hawajafika kazini leo.

Mdau, John
Eastern Cape, Sauzi.


Mdau Kahwa ashiriki semina ya kuangalia mustakabali wa mkataba wa amani kati ya Paua New Guinea na Visiwa vya Bougainville

Mdau ambaye ni mkuu wa ofisi ya United Nations Office for Coordination for Humanitarian Affairs nchini Papua New Guinea,Ndg Ruger Kahwa (Kati) akiwa na Rais wa Autonomous Government of Bougainville Mr John Momis (Kulia) na Mtaalam wa masuala ya katiba na usuluhushi (Kushoto), Mara baada ya semina ya kuangalia mustakabali wa mkataba wa amani kati ya Paua New Guinea na Visiwa vya Bougainville baada ya miaka kumi. Semina iliyofanyika kisiwani Bougainville.


TTCL yakabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa watoto yatima na wazee wasiojiweza mkoani Kilimanjaro

Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya simu Tanzania(TTCL) Said Amir Said akizungumza na wanahabari (hawako pichani)muda mchache baada ya kukabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa watoto yatima na wazee wasiojiweza wa mjini Moshi.
Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya simu Tanzania(TTCL) Said Amir Said(katikati)akikabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Alhuda Bw Yahaya Karebile.(kulia).
Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya simu Tanzania(TTCL) Said Amir Said akikabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa watoto Mustapher Robert na Suleiman wa kituo cha watoto yatima cha Mkombozi.
Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya simu Tanzania(TTCL) Said Amir Saidakikabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa mlezi wa kituo cha wazee wasiojiweza cha Njoro Bi Ndeta Tenga.
Wafanyakazi wa TTCL mkoa wa Kilimanjaro wakiwa na wageni mbalimbali katika hafla fupi ya kukabidhi zawadi za siku kuu ya Eid kwa watoto yatima na wazee wasiojiweza.

Na Dixon Busagaga,Moshi.

KAMPUNI ya simu Tanzania (TTCL), imetoa zawadi ya vyakula kwa ajili ya watoto yatima, walemavu na wazee wasiojiweza, ikiwa ni moja ya utekelezaji wa mipango ya kampuni hiyo, yenye lengo la kusaidia makundi maalum ya kijamii.

Msaada huo ikiwemo sukari, mchele, mafuta ya kupikia, unga na sabuni vyenye thamani ya shilingi milioni 1.6, ulitolewa juzi kwa walengwa hao wanaolelewa kwenye vituo vya Mkombozi, Alhuda Fund Centre na kikundi cha wazee wasiojiweza kilichopo kata ya Njoro mjini Moshi.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo, afisa mtendaji mkuu wa TTCL Said Amir Said, alisema kampuni hiyo inatambua mahitaji muhimu ya kijamii kwa makundi maalum, na kuongeza kuwa msaada huo ni moja ya utekelezaji wa mpango wa kuyasaidia makundi hayo.

Said aliongeza kuwa licha ya msaada huo kuwa sehemu ya kuungana na makundi hayo ya kijamii katika kusherehekea sikukuu ya Eid el Fitr,pia kampuni hiyo imeelekeza nguvu katika kujali matatizo ya watu kwenye makundi hayo na kutafuta njia za kuwasaidia.

“Sisi TTCL kama kampuni ya umma na ya kizalendo, tunajali sana jamii inayotuzunguka pamoja na matatizo yake, ndio maana leo tunatoa msaada huu wa vyakula kwa makundi haya ya wahitaji, tukijua kuwa ni jukumu letu kama kampuni ya Kitanzania kusaidia”, alisema afisa huyo.

Pia alisema kampuni yake itaendelea kuihudumia jamii, ambapo sehemu ya mapato yake itaelekezwa kutoa huduma za kijamii, kama hatua mojawapo ya kuonyesha kuwa sehemu ya mapato hayo inarejeshwa kwa jamii.

Msaada huo wa chakula ni sehemu ya misaada mingine iliyotolewa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, visiwani Zanzibar ukiwemo mkoa wa Kilimanjaro, yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10, katika kusherehekea sikukuu ya Eid.


Mwalimu Nyerere & J.F Kenneddy at the White House 1963



ALIZALIWA SEPTEMBA 7th, 2008
SEPTEMBA 2011 BADO ANADUNDA...
FundiWaKombo
ChampagnePOP.jpg


Idd Mubarak!

UONGOZI WA GLOBU YA JAMII PAMOJA NA KIKOSI KAZI CHAKE INAWATAKIA WADAU WOTE POPOTE MLIPO DUNIANI IDD MUBARAKA NJEMA


Antigone crew ( Parapanda Theatre Lab and Gothenburgh City Theatre Sweden) in Dar!


Antigone crew ( Parapanda Theatre Lab and Gothenburgh City Theatre Sweden) now in Dar! set for a world class production of Greek play Antigone . Performances on 21st September  Water front , 22nd and 23rd Russian Culture centre , 25th Chuo cha Sanaa Bagamoyo . A production not to be missed .For more information visit www.trinitypromotionstz.blogspot.com 


MARIAN SCHOOLS BAGAMOYO FUNDRAISING GALA DINNER INVITATION- 4TH SEPT

Uongozi wa Shule za Marian Bagamoyo unawakaribisha wote kwenye Fundraising hii
ya Kujenga na kuendeleza Shule hizi.

Mgeni Rasmi atakuwa Mhe. Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba

Wazazi,wanafunzi wa zamani,wenyeji wa Bagamoyo na wote wale wenye Mapenzi mema mnakaribishwa sana sana SEPTEMBA 4, 2011 ukumbi wa Diamond Jubilee Hall  jijini Dar es salaam saa Moja jioni.

Asanteni!


aluta kontinyua na mambo yale yaleeeeeee.....safari hii Zenji


Baraza la mji wa Zanzibar limeanzisha zoezi la kuzifunga kwa kofuli gari zote zinazoegeshwa katika maeneo yasiyoruhusiwa na baada yake hutozwa fidia kwa anaetenda kosa hilo Ankal usiweke gari lako hapo yatakukuta yaliyomkuta dereva wa gari hilo la Suzuki Escudo katika eneo la mji mkongwe.
PICHA NA MDAU WAKO:ZANZIBARCARHIRE.COM


the first Dallas Eid el Fitri Experience

 Kwa  niaba ya WaTanzania wote wa Dallas Tx nawatakia sikukuu njema ya Eid el Fitri…Pia napenda kuchukua nafasi hii kuwakaribisha Watanzania wote mnaoishi Marekani to the first Dallas Eid el Fitri Experience kuanzia ijumaa sept 2 mpaka sept 4 2011… Ratiba kamili ni kama ifuatayo.....

Ijumaa Sept 2 “KARIBU NITE” at AGGIES LOUNGE 
(9205 Skillman rd ste 134 Dallas Tx 75243)
Party itaanza saa nne usiku mpaka chee, wanawake bure mpaka saa sita usiku… Kingilio kwa wanaume ni $10. Mazingira mazuri, mziki wa nguvu plus a surprise artist ataperform usikose…  Houston finest Dj Kaycee atakuwepo kuhakikisha unacheza usiku wote…Karibu
Jumamosi Sept 3 “WHITE PARTY” The Main Event at CLAYPIT (4460 Belt line rd Addison Tx 75001)
This is a strictly all white party (Viatu tuu unaruhusiwa kuvaa rangi tofauti) Party itaanza saa nne usiku… kiingilio dola 5 kila mtu before saa sita usiku dola 10 after saa sita usiku so tafadhali fika mapema… A FREE CHAMPAGNE BOTTLE TO THE BEST DRESSED PARTY PATRON  so pliz dress to impress… A special surprise artist to perform… (u do not wanna miss this).8 VIP TABLES available  Kwa wale wanaopenda VIP na BOTTLE service…Dj Kaycee on the 1 n 2 party till 5am…
Jumapili  Sept 4 “KWAHERI NITE” at OTARU LOUNGE (5100 Belt line rd ste 796 Addison Tx 75254)
Kwaheri nite kuanzia saa nne usiku mpaka saa nane usiku… kila mtu bure b4 saa sita usiku… dress code strictly enforced… Sehemu ya nguvu, mziki wa nguvu watu wa nguvu…Usikose!!!!!!!!
Ukitaka VIP ama Bottle service tafadhali piga namba zifuatazo             469-464-8031       //             469 254 0897      
ASANTENI  NA KARIBUNI SANA DALLAS!!!!!!!!!!!!!!!!!


hepi besdei ya kuzaliwa Enid Mollel

Mtoto Michelle Raymond akimlisha keki rafiki yake,Enid Mollel ambaye alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa nyumbani kwao Kaloleni jijini Arusha juzi(picha na moses mashalla
 Mtoto,Enid Mollel akimlisha keki mama yake,Magreth Olotu wakati akisheherekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza umri wa miaka 11 iliyofanyika nyumbani kwao eneo la Kaloleni jijini Arusha.
 Ndugu,jamaa na marafiki wakimpongeza mtoto,Enid Mollel(aliyevalia nguo nyeusi(baada ya kutimiza umri wa miaka 11 wakati akisheherekea  siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika nyumbani kwao juzi eneo la Kaloleni jijini Arusha.
Mtoto Enid Mollel akikata keki wakati akisheherekea  siku yake ya kuzaliwa 


hepi besdei ya kuzaliwa Iman Juma Pinto

 Mtoto wa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto, Iman Pinto, akikata keki wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka minne ya kuzaliwa kwake, mwishoni mwa wiki, Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto akikata keki tayari kumlisha mwanawe Iman.
 Imani akimlisha keki Bibi mzaa baba
 Iman akimlisha keki mamake mzazi Queen Komanya


Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker