Ndugu zangu
TAARIFA YA MSIBA WA SAID TAMIMU ALLY
Ningependa kuwajulisha kuwa Tamimu amefariki dunia Usiku wa kuamkia Jumapili na mazishi yalifanyika jana saa kumi jioni makaburi ya Tabata Segerea.
Natoa shukrani zangu za dhati na kwa niaba ya familia ya ndugu Said Tamimu Ally.
Nashukuru sana kwa wote waliotoa michango yao ya mali na hali kwa ajili ya kuokoa maisha ya ndugu yetu Tamimu.Shukrani pekee ziwaendee ndugu walioko UK, USA Norway, Canada Muscat, Dar es salaam,Tabora, Arusha na sehemu nyinge nyingi kwa msaada wao wa hali na mali ikiwemo ushauri na kutoa pole.
Asante sana.Soma Historia Yake Hapa















































Poleni sana. Mungu aiweke roho ya marehemu pema peponi. Inauma sana.
Mungu aiweke mahala pema peponi roho yake.
Maisha kweli hayajahaidiwa kwa mtu hatujui lini wala muda tunaweza kuondoka. Mimi na jamaa wengi kwenyi hii blog tuliguswa na story huyu jamaa tukatoa michango ya mali na mawaidha lakini sasa inakuwa kama si kweli ya kwamba amefariki dunia. Namuombea kwa Mungu amlaze pema peponi.
Mwenyezi Mungu amjalie pumziko jema la milele. Amina.
Tafadhali rekebisha lugha. Badala ya "Ningependa kuwajulisha...." andika "Ninasikitika kuwajulisha...." Namna hii sio utamaduni wetu wa kupashana habari za misiba.
DAH POLENI WAFIWA.INASIKITISHA SANA. Na azizdi kuwapa wanafamili moyo mzuri zaidi . AMLAZE MAHALI PEMA.AMIN.
Inna lillah wainna ilaihi raajiun.Mwenyezi mungu awape subra kwa familia yake Inshaallah.Na mwenyezi mungu amuhifadhi peponi.Amin
Inalilllah wainailaih rajiuun, hakika sote ni waja wa mwenyezimungu na kwake tutarejea. Tumuombe Mungu ampe njia ya salama na amani ndugu yetu aliyetangulia na ziada awalipe ujira wale wote waliojitolea kumsaidia hasa dada Ana ambaye alikuwa mstari wa mbele ingawa Said hakuwa ndugu yake. Huu ndio upendo wa dhati ambao sote Watanzania tunapaswa kuwa nao.
rm
INNALILAHI WAINAILAYHI RAJIUNNN
INNALI LLAH WAINNA ILAHI RAJIUUN!
Mwenyezi mungu ampumzishe mahala pema,na azidi kuifariji familia...too sad!
Simjui Saidi, lakini lazima nikiri kuwa matone ya machozi yalinitoka niliposoma taarifa hii. Poleni wafiwa. Mungu amuweke Saidi Tamimu mahali pema peponi. Amin.
Very sad news. Poleni wafiwa. RIP Said Tamimu.
Poleni wafiwa mungu akupeni nguvu..katika wakati huu mgumu...na pia inasikitisha kuona mtoto akiwa katika hali kama hiyo..hospitali zote zinashindwa kuonyesha ujuzi wao hata bure ili kuokoa maisha ya mtoto..dhani kusubili michango inauma saaaana..ni .mimi tembo dume..waosha midomo mnakaribishwa.
poleni sana wafiwa na mwenyezi mungu amlaze pahala pema peponi
INNALI LLAH WAINNA ILAHI RAJIUUN!
AALLLLAH MAGHFIRLAHU MARHAMHU FIL JANAH
Wadau waliochangia Mungu awabariki sana, hii ndio maana ya DINI SAFI, KUWASAIDIA WENYE MAHITAJI NA SHIDA.
Unaweza usiwe unaenda msikitini au kanisani, lakini iwapo binadamu atafanya hivi basi anamzidi hata yule ashindaye katika majumba ya ibada.
Inauma sana.
Mungu ampumzishe kwa amani.
Poleni sana wafiwa. Roho ya marehemu ipunzike mahali pema peponi. Amen
Mungu amlaze mahala pema peponi. Amina.