Jamaa kaingia Bar na kukuta watu wametulia wanapiga mambo yao,nae akaanza kutoa oda kwa mkwara kama ifuatavyo:-

Jamaa: "Muhudumu, nipe kinywaji na mpe kila mtu humu ndani kinywaji,
maana wakati napata kinywaji lazima kila mtu apate kinywaji."

Haraka sana muhudumu akagawa vinywaji,

Jamaa: "Muhudumu nipe supu na kila mutu humu ndani mupe supu maana
ninapokunywa supu kila mtu lazima anywe supu."

Watu wakapewa supu,tena safari hii wakapiga makofi kumpongeza.

Jamaa: "Muhudumu nipe bili, na kila mtu humu ndani mupe bili maana wakati
nalipa bili yangu kila mutu lazima alipe yake."

Zogo lilianzia hapooo.....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 29, 2012

    Hapo kwenye bili patakuwa hapatoshi, Ankal loh!

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 29, 2012

    haaaa haaaaa haaaaaaa, u made my day

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 29, 2012

    Ofa kama hizi ndio pale unapoambiwa:

    1.Bure ghali !
    2.Gusa unase !
    3.Kula uliwe !

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 29, 2012

    Fundisho hapa ni tusipende offer za bure... wazungu wanasema "There is no free lunch" au Usifikiri umepata kumbe umepatikana... hapo piga mahesabu kama ulikuwa hauna hela alafu ukaparamia offer kwa kujimwaya mwaya... ndipo kibao kinageuzwa... duh... hiyo kali...

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 29, 2012

    duu hii imepoa sana ha ha ha michuzi shukran kwa kunichekesa

    mdau washington D.C

    ReplyDelete
  6. Hahahahaha! Nothing is for free kwahakika.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 30, 2012

    Jamani mbavu zangu nimecheka mpaka maumivu ya kubeba box yamepotea khaah!.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 30, 2012

    Ha!ha!ha!ha!ha!ha!ha!ha!ha! Nimefurahi sana - Niliamka na unyonge ndani ya moyo wangu lakini yote nimesahau nimeongeza japo pumzi za kuendelea na maisha - SAFI SANA!!! Kila mtu atie akili Wabongo wengine wapenda sana BURE ona walimpigia makofi ya furaha!!! sasa sijui mwisho walirusha chupa au kila mmoja alianza!!!!!

    ReplyDelete
  9. duh huyo naona watamuua... ni kali hiyo ya mwaka
    http://staryte.ucoz.com/

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...