Kikosi kilichofanya mauaji leo
 Erasto Nyoni mfungaji wa bao la ushindi
Shomary Kapombe aliyesawazisha

Kaseja akiokoa moja ya hatari langoni Stars
Mwinyi Kazimoto akiwaongoza wenzake kutoka uwanjani baada ya mechi

Taifa Stars jioni hii imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Gambia kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, katika mechi ya pili ya Kundi C, kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Stars ilitoka nyuma kwa 1-0 kipindi cha kwanza na kuibuka na ushindi huo- kwa mabao ya kipindi cha pili ya Shomari Kapombe dakika ya 60 na Erasto Nyoni dakika ya 87 kwa penalti, baada ya beki mmoja wa Gambia kuunawa mpira kwenye eneo la hatari.

Stars ambayo mechi ya kwanza ilifungwa 2-0 na wenyeji Ivory Coast mjini Abidjan Jumamosi iliyopita, kipindi cha kwanza ilicheza ovyo kidogo, lakini kuingia kwa Haruna Moshi ‘Boban’ aliyechukua nafasi John Bocco ‘Adebayor’ kipindi cha pili, kuliifanya Tanzania icheze kwa uhai na kulitia misukosuko lango la Gambia hatimaye kupata mabao hayo mawili.

Gambia walitangulia kupata bao lililofungwa na Mamadou Ceesay dakika ya nne. Stars sasa imejinasua mkiani mwa kundi C na kupanda nafasi ya pili badaaye Morocco kutoa sare ya 2-2 jana na Ivory Coast inayoongoza kwa pointi zake nne.


Kwa Stars huu ni ushindi wa kwanza nyumbani tangu waifunge Jamhuri ya Afrika ya Kati Machi 26, mwaka jana.
Picha na Habari na  Bin Zubeiry


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 10, 2012

    Goo Taifa Star.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 11, 2012

    stars kaza buti

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 11, 2012

    Ushindi sawa lakini, kuulinda kwa mechi ya marudiano hapo huwa kibarua kigumu. Stars sikuzote wakitakiwa angalau droo ya aina yoyote huwashinda.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...