Jaji Mkuu wa Tanzania  Mhe.Mohamed Othman Chande yuko ziarani nchini Marekani ziara ambayo imejumuisha Majaji Wakuu wengine kutoka Afrika Kusini,Ghana,Namibia,Zanmbia,Malawi,Kenya,Uganda na Msumbiji, Ziara hii ya aina yake imeratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na madhumuni yake makubwa ni kujionea jinsi mfumo wa Sheria na Utoaji Haki katika mahakama vinafanya kazi pamoja na maeneo ya Utawala Bora. Katika ziara hii Jaji Mkuu Chande ametembelea mahakama ya Rufaa ya Marekani jijini Washington DC pamoja na Chuo Endelevu cha Majaji Chicago na leo hii alionana na Mhe.Hilary Clinton, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani pamoja na Majaji wengine waalikwa na kuwa na mazungumzo nae katika Wizara ya Nje ya Marekani Washington DC.

Mhe.Mohamed Othman Chande PIA alipata wasaa wa kutembelea Ubalozi wa Tanzania Washington DC.Katika picha Mhe. Chande akipokelewa na Bw. Suleiman Saleh,Afisa Ubalozi wa Tanzania Washington DC na pia akisaini kitabu caha wageni Ubalozini hapo. Mhe.Chande akiwa na Bw.Suleiman Saleh mara baada ya kumaliza ziara yake Ubalozini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Katika tovuti ya Ubalozi wetu uliopo Washington, kuna maelezo ya kuwa Watanzania waliopo Marekani wanaweza wakajiandikisha kwa njia ya TEKNOHAMA na hivyo kuweza kutumia nguvu kazi yao katika fani mbalimbali. Lakini kwa bahati mbaya sijaweza kufanikiwa kuiona hiyo link kweye tovoti hii.
    Kama wahusika wa ubalozi wataiona hii naomba watueleweshe katika hilo ni nini cha kufanya

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...