Manispaa ya Kinondoni ni moja ya wateja wakubwa wa NMB lakini pia Manispa ya kinondoni inaongoza kwakua na wakazi wengi zaidi ya manispaa nyinginezo. Hivyo basi kwa kulizingatia hili na kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri kati ya NMB na Manispaa ya Kinondoni NMB imedhamini mashindano yanayoendelea katika wilaya ya kinondoni . Mashindano ambayo yanawahamisisha vijana katika kuimarisha ulinzi na usafi.Michuano hii ambayo inazinduliwa katika awamu tatu tofauti na katika sehemu tatu tofauti, mwishoni mwa wiki ikiwa ndio uzinduzi wa pili ulishirikisha kata ya Mzimuni na Ndugumbi ambapo Ndugumbi waliibuka kidedea kwa 1-0

Mheshimiwa Iddi Azan Mbunge wa Jimbo la kinondoni akikagua vikosi vya mpira wa miguu kata ya Ndugumbi na Mzimuni mwishoni mwa wiki ambao wapo katika michuano ya kinyang’anyiro cha Kinondoni Meya Cup 2013 inayoendelea katika kata tofauti wilayani humo.Mashindano haya yakiwa na kusudi la kuhamasisha Usafi na ulinzi Benki ya NMB ikiwa ndio wafadhiri wakuu na TVS King watatoa zawadi ya pikipiki ya miguu mitatu kwa mshindi wa kwanza

Mchezaji Abdul Hussein wa timu ya Ndugumbi akiwakabili vilivyo wachezaji wa timu ya Mzimuni katika michuano ya kuwania kombe la meya wa kinondoni 2013 katika mechi zinazoendelea kwenye wilaya ya kinondoni Katika mechi zilizochezwa mwishini mwa wiki Ndugumbi waliibuka kidedea kwa 1-0

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. kweli tutafika katika viwabgo vya kimataifa? viwanja vyetu ni vumbi mtindo mmoja.Wizara mpo?Serikali tengeni viwanja vya michezo.Playing parks or Recrations parks.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...