MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA |
1.
Mheshimiwa
Spika, tumekuwepo
hapa Bungeni, Dodoma kwa takriban siku 11 ambapo leo tunahitimisha shughuli
zilizopangwa katika Mkutano wa Kumi wa Bunge lako Tukufu. Nitumie nafasi hii
kumshukuru Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutufikisha salama siku ya
leo.
2.
Mheshimiwa
Spika, awali
ya yote naomba nitumie nafasi hii kutoa pole kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki
waliopoteza Wapendwa wao katika ajali mbalimbali zilizotokea hapa Nchini,
ikiwemo ajali ya Jahazi la Sunrise
iliyotokea Wangwi katika Bahari ya Hindi na Ajali ya Lori kule Mbarali ambapo
Watu wamepoteza maisha na kupata majeraha. Aidha, tunawapa pole Majeruhi wote
na Abiria waliopoteza mali katika ajali hizo. Kwa kipekee kabisa napenda kutoa
pole kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Askofu Thomas Laiser wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini
Kati - Arusha ambaye amefariki jana Mchana na Askofu Mstaafu Amedeus Msarikie
wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Moshi ambaye
amefariki Usiku wa kuamkia leo huko Nairobi alikokuwa anapata matibabu. Wote tunawapa pole sana!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...