MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

1.            Mheshimiwa Spika, tumekuwepo hapa Bungeni, Dodoma kwa takriban siku 11 ambapo leo tunahitimisha shughuli zilizopangwa katika Mkutano wa Kumi wa Bunge lako Tukufu. Nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutufikisha salama siku ya leo.

2.            Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba nitumie nafasi hii kutoa pole kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki waliopoteza Wapendwa wao katika ajali mbalimbali zilizotokea hapa Nchini, ikiwemo ajali ya Jahazi la Sunrise iliyotokea Wangwi katika Bahari ya Hindi na Ajali ya Lori kule Mbarali ambapo Watu wamepoteza maisha na kupata majeraha. Aidha, tunawapa pole Majeruhi wote na Abiria waliopoteza mali katika ajali hizo. Kwa kipekee kabisa napenda kutoa pole kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Askofu Thomas Laiser wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Kati - Arusha ambaye amefariki jana Mchana na Askofu Mstaafu Amedeus Msarikie wa Kanisa Katoliki, Jimbo la Moshi ambaye  amefariki Usiku wa kuamkia leo huko Nairobi alikokuwa anapata matibabu. Wote tunawapa pole sana!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...