Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais wa China Xi Jinping wakiweka mashada ya maua katika makaburi ya wataalamu wa China waliofariki wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA.Viongozi hao waliweka mashada hayo ya maua katika makaburi hayo yaliyopo katika kijiji cha Majohe,Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa China Mama Peng Liyuan wakiweka maua katika makaburi ya wataalamu wa China waliofariki wakati wa ujenzi wa Reli ya TAZARA huko katika kijiji cha Majohe,Ukonga nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wa Rais Xi Jinping wakishuhudia(picha na Freddy Maro).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Wadau naomba kuuliza swali. Kwanini rais wa taifa kubwa kama China anatumia ndege ya ki-Marekani?

    ReplyDelete
  2. we anony wa 10:59pm Jibu ni kwa sababu kila mtu akitengeneza ndege nani atanunua ndege kwa mwenzake...ni mambo ya kawaida tu ya kibiashara, huzalishi kila kitu unazalisha kile ambacho unakizalisha kwa ufanisi na gharama ndogo zaidi kuliko mwingine.

    ReplyDelete
  3. Mtoa Maoni wa 2 umenena Kiuchumi sana.

    Ni kwa Kimombo 'Comparative advantage' na 'Comparative costs'

    ReplyDelete
  4. HAKUNA "we anony wa 10:59pm"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...