Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila,wa pili toka kushoto akikabidhiwa msaada wa Kompyuta Tano zenye thamani ya shilingi Milioni 6 na mshindi wa”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho kwa niaba ya Vodacom Foundation.Wanaoshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation Bi.Grace Lyon na Mwenyekiti wa bodi wa Chuo hicho Askofu Dkt Gerald Mpango watatu toka kushoto.
Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila pamoja na Mwenyekiti wa bodi wa Chuo hicho Askofu Dkt Gerald Mpango wakiwa na nyuso za furaha wakiinua moja ya Kompyuta juu kati ya tano zenye thamani ya shilingi Milioni sita,walizopewa msaada na mshindi wa ”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha(kulia) ambae ni mwanafunzi wa chuo hicho kwa niaba ya Vodacom Foundation.anaeshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation Bi.Grace Lyon.
Mkuu wa Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoa wa Kigoma Mwl.Joseph Mwangamila(kulia)akimkabidhi sehemu ya msaada wa Kompyuta Tano zenye thamani ya shilingi Milioni 6,Mwanafunzi wa chuo hicho,Rehema Romani,baada ya kukabidhiwa na mshindi wa”Vodacom Mahela”Bw.Valerian Kamugisha,wa pili toka kushoto,kwa niaba ya Vodacom Foundation.Anayeshuhudia kushoto ni Meneja wa Vodacom Foundation, Bi.Grace Lyon.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 03, 2013

    Ama kweli nanianasema sio tamu Fedha?

    Suti imetulia tofauti na alivyokuwa hapo kabla wakati akienda chukua 'mzigo' wake 100Mil. akiwa katika mashati ya kawaida.

    Bwana Mapesa Vodacom Mahela Valerian Kamugisha anazidi kung'ara!!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 03, 2013

    Maisha bwana, MUNGU akiamua basi!

    Kijana ndio hivyo tenaaaaa!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 03, 2013

    kwa hiyo sasa zimebakia milioni 94. Mungu amusaidie kijana kwani ana roho nzuri.

    ila aangalie asitoe misaada mingi halafu akaishiwa

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 04, 2013

    Mdau wa 3

    .......
    kwa hiyo sasa zimebakia milioni 94. Mungu amusaidie kijana kwani ana roho nzuri.

    ila aangalie asitoe misaada mingi halafu akaishiwa
    .......

    Usiwe na wasiwasi MUNGU NI TAJIRI SAAANA Ndugu V.Kamugisha kamwe hawezi kuishiwa tayari amesha chaguliwa na Mwenyezi, kwa kuwa akitoa sana ndio atapata nyingine zaidi!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 04, 2013

    Kwa kweli SIR GOD hama Mshirika!

    Nchini Tanzania tupo takribani 45Mil. miongoni mwetu wengi walipenda wazipate Tsh. 100.Mil lakini SIR GOD akamchagua ndugu Valerian Kamugisha !!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 04, 2013

    Wadau ni kama anavyosema Madu wa 5 hapo juu,

    Riziki haina kigezo cha kuwa na ujanja wala haraka ya kuwa mjanja sana ndio utafanikiwa ama kuwa na haraka sana na kutumia nguvu nyingi ndio vigezo vya mafanikio la hasha!

    Ni kama ndugu yetu Kamugisha hakuwa na haraka wala hakutumia Mabavu kuzikamata Tsh. 100Mil. ila ni kutokana na uwezo wa MWENYEZI ASIYEKUWA NA FITINA WALA MAJUNGU!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...