Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio akimpa maelezo Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo alipotembelea katika banda la PPF katika maonyesho ya 37 ya kimataifa ya biashara katika viwanja vya Sabasaba.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bi Joyce Mapunjo, pembeni yake ni Kaimu Mkurugenzi wa TanTrade Bi Jacqueline Maleko.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio akimsindikiza Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue na ujumbe wake mara baada ya kutembelea banda la PPF.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira Mh. Eric Shitindi akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa PPF Bwana Thomas Chissanga. Katikati ni Meneja Uhusiano na Masoko wa PPF Bi Lulu Mengele.
Meneja Uratibu wa Ofisi za Kanda za PPF Bwana Mbaruku Magawa akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira Mh. Eric Shitindi alipotembelea banda la PPF. Kulia ni Meneja Uhusiano na Masoko Bi Lulu Mengele.
Afisa wa Sheria wa PPF Bi Nyambilila Ndoboka akimpa maelezo Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi na Ajira Mh. Eric Shitindi. Pembeni ni Mameneja wa PPF, Bwana Mbaruku Magawa na Bi Lulu Mengele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...