Sehemu ya Magunia ya Dagaa yakiwa yamepangwa vyema ndani ya soko hilo tayari kwa kusafirishwa sehemu mbalimbali kwa matumizi ya binadamu na mifugo.
 Dagaa 'wachafu' wakiwa wameanikwa chini kwa ajili ya kukaushwa.!Globu ya Jamii pia ilipata nafasi ya kuzugumza na mmoja wa wafanyabishara wa dagaa,kuhusiana na bei,akaeleza kuwa dagaa wazuri kwa sasa wanauzwa kati ya elfu 8 mpaka 12 kwa ndoo ya plastiki,"Lakini pia hawa walioanikwa hapa chini sisi wakazi wa Mwanza huwa hatuli,tunatengeneza maalum kwa ajili ya kuwauzia watu wenye mifugo,lakini pia kuna baadhi ya wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali nje ya jiji la Mwanza wamekuwa wakija kuwanunua dagaa hawa "wachafu" kwa ajili ya matumizi ya chakula na kwenda kuwauza huko mikoani ikiwemo jijini dar es salaam kwa bei yao"alisema mfanyabiashara huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe hapa mtandaoni. 
 Sehemu ya soko kuu la Kimataifa la Samaki-Kirumba Mwaloni jijini Mwanza kama lionekanavyo mapema leo mchana
 Wakina mama wakijishughulisha na biashara yao ya ndizi ndani ya soko kuu la Kimataifa la Samaki-Kirumba Mwaloni jijini Mwanza
Baadhi ya Wafanyabiashara hao wakiwa bize kuwachambua Dagaa wasiofaa na wanaofaa kwa matumizi mbalimbali. 
Sehemu ya bango la soko hilo kama lionekanavyo pichani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...