Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Judith Mtawali (kulia) ambaye amestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma akikata keki wakati wa sherehe iliyoandaliwa na watumishi wa Idara ya Wakimbizi kwa ajili ya kumuaga na kumtakia maisha mema yenye mafanikio maishani mwake. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Michokeni Resort Centre, jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Idara ya Wakimbizi wakipeleka zawadi zao kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Judith Mtawali ambaye amestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Michokeni Resort Centre, jijini Dar es Salaam.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Judith Mtawali ambaye amestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma akizungumza kwa furaha kwa kuwashukuru watumishi wa Idara ya Wakimbizi kwa zawadi nyingi walizompa pamoja na kumtakia heri maishani mwake. Aidha, Mtawali aliwaomba watumishi hao waendelee kufanya kazi kwa uadilifu na hatimaye watakuja kufanikiwa maishani mwao. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Michokeni Resort Centre, jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Idara ya Wakimbizi wakichukua chakula katika hafla hiyo iliyofanyika kwa ajili ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Judith Mtawali ambaye amestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Michokeni Resort Centre, jijini Dar es Salaam.
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Judith Mtawali (katikati waliokaa) ambaye amestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa idara hiyo mara baada ya kupokea zawadi mbalimbali kutoka kwa watumishi hao. Kulia (waliokaa) ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara hiyo, Harrison Mseke. Hafla hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Michokeni Resort Centre, jijini Dar es Salaam. (Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...