Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Emmanuel Nchimbi aliwasili nchini Zambia tarehe 22 Novemba 2013 na kuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Zambia, Dkt. Edgar Lungu siku hiyo hiyo.
Mazungumzo baina ya Mawaziri Hawa yaljikita katika kuendeleza ushirikiano kwenye maeneo mbalimbali yanayohusu Wizara zao. Aidha wamekubaliana kuagiza mapema iwezekanavyo wataalam wa Wizara zao wakutane kwa majadiliano ya kuweka misingi ya ushirikiano huo.
Waziri Mambo ya Ndani wa Tanzania, Mhe Dkt. Nchimbi (kushoto) na Mhe. Edgar Lungu (kulia) kwenye Ofisi za Waziri wa Mambo ya Ndani wa Zambia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...