June 2013
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiandamana na Mheshimiwa Inagosi Bulo kutoka DRC (kushoto) na Inkhosikati Lambikiza wa Swaziland na Mama Charlotte Scott wa Zambia wakiwa nje ya banda la Zanzibar mara baada ya kutembelea banda hilo.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Maendeleo Mama Salma Kikwete akiangalia bidhaa mbalimbali za aina ya shanga zilizokuwa zikionyeshwa kwenye banda la SIDO wakati walipotembelea maonesho hayo tarehe 30.6.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na wageni wake wakiangalia mashine ya kutengeneza nguo aina ya vikoi kwenye banda la SIDO wakati walipotembelea banda hilo tarehe 30.6.2013.
Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiagana na Mke wa Makamu wa Rais wa Zambia Mama Charlotte Scott ambaye aliondoka uwanjani hapo kwenda uwanja wa ndege kuungana na mume wake kwa ajili ya safari bya kurudi nchini Zambia.

Na Salum Vuai, Maelezo

WATU 52 wamepoteza maisha na wengine 332 wamejeruhiwa kutokana na ajali 175 za barabarani zilizotokea katika Mkoa wa Kaskazini Unguja kati ya Januari mwaka 2011 hadi katikati ya mwaka 2013.

Takwimu hizo zimetolewa leo na Mkuu wa Usalama Barabarani wa jeshi la Polisi mkoani humo Ali Muhsin, wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya ‘Safiri Salama’, yaliyofanyika katika viwanja vya Mahonda, Wilaya ya Kaskazini B.

Mkuu huyo alisema, ajali za barabarani ni tishio kubwa kwa watumiaji wote wa barabara, wakiwemo madereva, abiria na watembeao kwa miguu, na kwamba tahadhari kubwa inahitaji kuchukuliwa kuziepuka.

Alieleza kuwa, endapo watumiaji wa barabara hawatakuwa waangalifu, majanga ya maafa, ulemavu wa kudumu, majeraha, hasara kwa mali na uharibifu wa miundombinu, vitaendelea kuliandama taifa.

Alitaja sababu mbalimbali zinazochangia ajali hizo, kuwa ni uhaba wa miundombinu imara, ubovu wa vyombo vya moto, mabadiliko ya hali ya hewa, utendaji mbaya wa wasimamizi wa sheria za usalama barabarani na kasoro za kibinadamu.

Umeonaa! Hivi ni kazi yangu nikimaliza najiajiri. Ndivyo anavyoelekea kusema mwanafunzi Paulina Emmanuel anayejifunza masuala ya ubunifu wa mavazi na mitindo katika chuo cha VETA Chang’ombe Dar es Salaam, akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa soko la ajira, mipango na maendeleo wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Bw. Enock Kibendela alipotembelea banda a VETA kwenye maonyesho ya SabaSaba, Dar es Salaam.
Mwanafunzi Ernest Maranya wa VETA Chang’ombe akitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda la VETA kwenye maonyesho ya Sabasaba Dar es Salaam akionyesha kifaa cha elimu ya mfumo wa jua na sayansi ya anga jinsi kinavyofanya kazi.
Mkufunzi wa masuala ya hoteli na Utalii katika chuo cha VETA Njiro, mkoani Arusha Theonestina Raphael akitoa maelezo kwa askari polisi waliotembelea banda la VETA kwenye maonyesho ya SabaSaba, Dar es Salaam.
Tukiongeza ufundi kidogo tutakuwa tumemaliza kazi! Ndivyo anavyoonekana kusema Mkurugenzi wa soko la ajira, mipango na maendeleo wa VETA, Bw. Enock Kibendela mwenye kofia alipokuwa akikagua bidhaa za Mamlaka hiyo kwenye maonyesho ya sabasaba, Dar es Salaam.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mrtibu wa vyuo vya ufundi stadi kanda ya Dar es Salaam Florence Kapinga na Mwenyekiti wa Kamati ya maonyesho Abdul Mollel na Afisa Uhusiano wa VETA Dorah Tesha.
Mafunzo kwa watu wenye mahitaji maalum yanatolewa hivi! Mwalimu Kintu Kilanga mwenye kofia akimueleza Mkurugenzi wa Soka la ajira, mipango na maendeleo wa VETA Bw. Enock Kibendela kuhusu mbinu wanazotumia kumfundisha mwanafunzi Range Jackson (kushoto) mwenye tatizoo la Hyperactive. Hyperactive ni tatizo ambalo linasababisha mtoto kuwa na uelewa dhaifu wa masuala mbalimbali.
Moja ya bidhaa zilizotengenezwa na Range Jackson mwanafunzi wa VETA Chang’ombe anayesoma mafunzo maalum ya uchomeaji.
 Msanii wa Muziki wa Hip Hop,Roma Mkatoliki akipanga na kupangua vina vyake wakati wa Onyesho Kabambe la Kilimanjaro Tanzania Music Tour 2013,lililofanyika usiku wa Kuamkia leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani,jijini Tanga.
 Mkali wa Hip Hop,Prof. Jay a.k.a a.ka The Heavy Weight  MC akikamua vilivyo mbele ya Wakazi lukuki waliofika kwenye viwanja vya Mkwakwani kuona Onyesho la Muziki linaloongozwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia Bia yake ya Kilimanjaro maarufu kama Kilimanjaro Tanzania Music Tour 2013.
Mwana FA a.k.a Binamu akiimba wimbo wake wa Yalaiti na Mwanadada aliepanda jukwaani kuimba badala ya Msanii alieimba nae wimbo huo.

Binamu akikamua huku shangwe zikitawala.
Msanii wa Muziki wa Taratibu,Maarufu kwa jina la Recho akiimba nyimbo zake mbali mbali wakati wa Onyesho la Kilimanjaro Tanzania Music Tour 2013,lililofanyika usiku wa Kuamkia leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani,jijini Tanga.
Mamaa wa Majanga aitwae Snura akiwapagawisha wakazi wa Tanga na goma lake lililoshika hatamu sana hapa nchini (MAJANGA).
Ali Kiba na madansa wake wakitoa Burudani kwenye Onyesho hilo.
Mkali wa Hip Hop hapa nchini kwa Mwaka 2012/13,Kala Jeremier akifanya mambo yake mbele ya Mashabiki wake Lukuki waliofika ndani ya Uwanja wa Mkwakwani,Jijini Tanga usiku wa kuamkia leo.

 Washiriki katika mafunzo ya uongozi na biashara yananofanyika kwenye Ukumbi wa Nafasi Jijini Dar es Salaam wakifuatilia mafunzo hayo, washiriki hao wametoka katika taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na sanaa na sanaa za maonesho.
Mafunzo haya yanatolewa na Britishi Council, na mwezeshaji ni Faisal Kiwewa kutoka shirika la Bayimba la nchini Uganda.
Wakulima wa zabibu Mkoani Dodoma wametakiwa kutambua kuwa zao la zabibu lina thamani ya kimataifa na siyo ya kimkoa wala kitaifa na hivyo bei yake inatakiwa kuwa ya kimataifa kulingana na masoko ya kimataifa.

Wakulima hao wameshauriwa wasikubali mtu yeyote awapangie bei ya zabibu kimkoa au kitaifa kwa kuwa bei ya zabibu ya hapa nchini inatakiwa kushabihiana na kushindana na bei ya zabibu inayolimwa na kuuzwa kwenye nchi nyingine Duniani kama vile Afrika kusini na Italia.

Ushauri huu ulitolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa zao la zabibu kilichofanyika mjini Dodoma ambapo kiliwajumuisha wakulima wa zabibu kutoka vijiji vinavyolima zabibu hapa Mkoani Dodoma.

Wadau wengine walikuwa umoja wa wafanyabiashara, wakulima na wenyeviwanda TCCIA, Bank ya NMB, Wataalamu wa masuala ya Ushirika kutoka Idara ya Ushirika na Maafisa kilimo wa Wilaya zinazolima zabibu.

Ushauri huo umetolewa kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya wakulima kuonewa, kunyanyaswa na kuhujumiwa hasa kwenye soko la zabibu na baadhi ya wanunuzi kwa bei isiyolingana na hadhi ya kimataifa ya zao la zabibu wakati wanunuzi wenyewe wanauza zabibu hizo kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi kwa bei kubwa hadi kufikia zaidi ya mara sita ya bei wanayonunua kwa wakulima.

Dr. Nchimbi alifafanua kuwa kwa Mkoa wa Dodoma, zao la zabibu ni mojawapo kati ya mazao ya msingi, nguzo na mhimili kwa maendeleo ya Mkoa na Taifa, hivyo ni lazima lilindwe kwa masoko na bei za uhakika. Wataalamu wasaidie kutengenezwa na kupatikana kwa bei na masoko hayo. Vilevile Dr. Nchimbi aliwaagiza Halmashauri za Wilaya Mkoani Dodoma na CDA kuhakikisha wanakuwa na mpango kabambe wa miradi na mashamba ya zabibu na kuhakikisha wanayatolea hati miliki.

Kwa upande wake mwenyekiti wa umoja wa wakulima wa zabibu Mkoa wa Dodoma (DOGCO Ltd) ndugu Omary Ramadhani alisema kwa sasa umoja huo unaundwa na AMCOS sita na bado wakulima kwenye vyama vyao vya msingi wanaendelea kujiunga.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa Agenda za Msingi zilizopo mezani kwa DOGCO ltd kwa sasa ni pamoja na uanzishaji wa kiwanda cha kuongeza thamani ya zao la zabibu na kusindika mchuzi wa zabibu na tayari wameshafanya mazungumzo na na Benki ya Uwekezaji TIB.

Vilevile ni pamoja na kujadili juu ya upatikanaji wa bei elekezi ya zabibu kitaifa ambayo wanapendekeza serikali itangaze bei hiyo kama ilivyo bei ya mazao mengine kama kahawa, chai, korosho, pamba na tumbaku.
Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation receives Tun Dr Mahathir Mohamad, former Prime Minister of Malaysia, who is also a Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) Fellow Emeritus and Companion.  Tun Dr. Mohamad has cooperated with a number of African leaders to articulate the aims of the movement in achieving national visions, inclusivity through financial inclusion, quality and standards as well as innovation.   

Tun Dr. Mohamad is received by Mr. Omary Mjenga, Assistant Director of the Department of Asia and Australasia in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation. 
Hon. Minister Membe (2nd left), walks former Prime Minister of Malaysia Dr. Mahathir Mohamad to the VIP Room at the Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam.   Dr. Mohamad has been participating in the 2013 Global Smart Partnership Dialogue held from June 28, 2013 at the Mwalimu Nyerere Convention Centre in Dar es Salaam.

The Host patron and adviser to the Global 2013 Smart Partners Dr.Jakaya Mrisho Kikwete presents Commonwealth Partnership for Technology and Management(CPTM) Companion award to Sir Martin Laing (Malta) during a dinner he hosted for Smart partner participants held at Mwalim Nyerere International Conference Centre in Dar es Salaam yesterday evening.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete presents CPTM Award to Sir.Charles Masefield UK yesterday evening during the Smart partnership Dinner hosted for participants in Dar es Salaam yesterday evening.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete pose for a photograph with the recipients of Commonwealth Partnership for Technology and management(CPTM) awards.On the lest is Sir.Martin Laing of Malta and on the right is Sir.Charles Masefield United Kingdom.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete and his guest King Mswati III of Swaziland admire a lion trophy on display at Mwalimu Nyerere conference Centre yesterday during a dinner hosted for participants to Smart Partnership International Dialogue held at Mwalimu Nyerere International Conference Centre in Dar es Salaam yesterday evening.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete gives description of a lion trophy to Malaysian Prime Minister Najib Razak (second left) and King Mswati III of Swaziland at Mwalimu Nyerere Conference Centre during a dinner he hosted to the participants of of Smart Partnership International Dialogue yesterday evening.(photos by Freddy Maro).
Naibu Waziri wa Maliasiri na Utalii Mhe. Lazaro Nyarandu akimpatia briefing Spika wa Bunge la Oman Mhe. Sheihk Khalid Bin Hilal Bin Nasir Al Maalawi kabla ya kuanza kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro leo.
Mhe. Nyarandu akimuongoza Spika wa Bunge la Oman Mhe. Sheihk Khalid Bin Hilal Bin Nasir Al Maalawi kuingia lango kuu la Hifadhi ya Ngorongoro leo.
Naibu Waziri wa Maliasiri na Utalii Mhe. Lazaro Nyarandu akiongea na waandishi kuhusu ugeni wa Bunge la Oman uliongozwa na Spika wa Bunge lao Mhe. Sheihk Khalid Bin Hilal Bin Nasir Al Maalawi (kushoto) kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro leo.
Msafara wa Magari yaliobeba ugeni huo kutoka Bunge la Oman ukiwa Ngorongoro.
Mhe. Spika akipata Taswirazz Mbungani.

Wapiganaji walipokutana na mpiganaji mwenzao hivi karibuni katika harakati za kusaka taswira,pichani kulia ni Bashir Nkoromo na kushoto ni Richard Mwaikenda (na pichani kati ni Mwanadada mpiganaji akiwa ameshikiria makini kifaa chake cha kazi,la ajabu hakutaka jina lake lijulikane),lakini alionekana kivutio kikubwa katika utafutaji wa taswira za tukio husika (Picha na Mdau.).
 Mshindi wa droo kubwa ya Promosheni ya Cheka Nao Bw.Mkude Iddi, mkazi wa Morogoro, (kushoto) akioneshwa ujumbe wa M-Pesa wenye  Tsh milioni 2 na Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Morogoro, Kamanda Kasapila, alizotumiwa kwa kushinda katika promosheni hiyo inayoendeshwa na Vodacom Tanzania. Mshindi huyo ni kati ya washindi 5 waliojishindia shilingi Milioni 2 kila mmoja kwenye Promosheni hiyo  inayowawezesha  wateja kuongea na mitandao yote kwa bei nafuu. Ili kujiunga wateja wanatakiwa kupiga *149*01#.
Meneje Mauzo wa Vodacom Tanzania Kanda ya Morogoro, Bw. Kamanda Kasapila (kushoto) akimshuhudia mshindi wa droo kubwa ya Promosheni ya Cheka Nao, Bw.Mkude Iddi, akisaini baada ya kutoa fedha zake kwa njia ya M-Pesa alizotumiwa baada ya kushinda katika promosheni hiyo. Mshindi huyo ni kati ya washindi 5 waliojishindia shilingi Milioni 2 kila mmoja kwenye Promosheni hiyo  inayowawezesha wateja kuongea na mitandao yote kwa bei nafuu. Ili kujiunga wateja wanatakiwa kupiga *149*01#.
 Mshindi wa droo kubwa ya Promosheni ya Cheka Nao Bw.Mkude Iddi, mkazi wa Morogoro (kulia) akihesabu fedha zake baada ya kukabidhiwa na Mejena Mauzo wa Vodacom Tanzania Kanda ya Morogoro, Bw. Kamanda Kasapila. Mshindi huyo ni kati ya washindi 5 waliojishindia shilingi Milioni 2 kila mmoja kwenye Promosheni hiyo  inayowawezesha  wateja kuongea na mitandao yote kwa bei nafuu. Ili kujiunga wateja wanatakiwa kupiga *149*01#.


Baadhi ya waandishi wa habari wakimfanyia mahojiano mshindi wa droo kubwa ya promosheni ya Cheka Nao Bw.Mkude Iddi, mkazi wa Morogoro (kulia) baada ya kukabodhiwa shilingi milioni mbili alizojishindia kupitia promosheni ya Cheka Nao hiyo  inayowawezesha  wateja kuongea na mitandao yote kwa bei nafuu. Ili kujiunga wateja wanatakiwa kupiga *149*01#.
no image
Sekretarieti ya Mkoa wa Dodoma mwishoni mwa wiki ilifanya kikao cha pili cha baraza la wafanyakazi wake ambapo kwa mujibu wa katibu wa baraza hilo Ndugu Paul Masanja wajumbe wa baraza hilo ni pamoja na wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Ofisi zote za Wakuu wa Wilaya Mkoa wa Dodoma, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na Uongozi wa chama cha wafanyakazi wa serikali kuu na Afya TUGHE Mkoa.

Masuala muhimu katika kikao hiko cha baraza la wafanyakazi yalijumuisha Nafasi ya vyama vya wafanyakazi ndani ya baraza hilo, masuala ya mafao kwa watumishi wa Umma. Vilevile mapitio ya bajeti ya mwaka 2012/13, bajeti ijayo ya 2013/14 na kupitia mtiririko wa bajeti kwa kipindi cha kuanzia 2009/10 hadi 2013/14.
Mgeni rasmi katika kikao hiko alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema Nchimbi ambapo miongoni mwa masuala aliyoyapa msisitizo katika salamu zake za ufunguzi wa kikao hiko ni pamoja na yafuatayo:

·        Sera ya “Tenda kwa matokeo makubwa sasa” (Big Result Now). Dr. Nchimbi aliwataka watumishi wa umma kwa nafasi zao kwenye ofisi za serikali na shughuli mbalimbali lazima wajiwekee vipaumbele vya majukumu yao na kuweka mkakati mzuri wa utekelezaji utakaoleta ufanisi mkubwa na kasha kuweka utaratibu wa kupima matokeo ya utendaji.
Alifafanua kuwa lazima wafanyakazi waweke vipaumbele vinavyolenga kuleta mabadiliko makubwa katika kutatua kero na changamoto za wananchi mfano kwenye sekta ya utunzaji kumbukumbu/masijala, Afya na sekta zingine za huduma na uzalishaji.

·        Dr. Nchimbi aliwataka watumishi/wafanyakazi hususani wataalamu wa kilimo kujadili na kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa tatizo la muda mrefu la upungufu wa uzalishaji wa chakula ndani ya mkoa unaoleta tatizo la upungufu wa chakula mara kwa mara mkoani Dodoma ukilinganisha na mahitaji ya chakula yaliyopo kwa hivi sasa.

·        Vilevile aligusia tatizo/changamoto ya Mkoa wa Dodoma kuwa na matokeo yasiyoridhisha katika sekta ya elimu hususani ngazi ya msingi na sekondari. Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa Dr. Nchimbi, wafanyakazi wanaujuzi na utaalamu katika nyanja mbalimbali kulingana na mahitaji hivyo hawana budi kutumia utaalamu na ujuzi wao wote kusaidia Mkoa wa Dodoma kuondokana na tatizo lao la kufanya vibaya kwenye sekta ya elimu.

·        Msisitizo mwingine uliwekwa kwenye suala la kuboresha hali ya makazi ya wananchi/ujenzi wa nyumba bora za makazi za wananchi na uondoshaji wa Tembe. Wataalamu wawasaidie wananchi kuboresha shughuli zao za uzalishaji na kujiwekea utaratibu wa kufanya mavuno kwenye shughuli zao hususani kuvuna mifugo na mazao na kuwekeza kwenye kuboresha makazi yao kuanzia ngazi za vijijini hadi mijini.
  
·        Dr. Nchimbi aliwatahadharisha watumishi wa Umma wenye tabia ya kuhujumu serikali wawe makini, aidha alikemea mahubiri hasa ya siasa yenye  viashiria vya uvunjifu wa amani, utulivu na mshikamano, vurugu na umwagaji damu; aliwaasa watumishi/wafanyakazi wasikubali kujihusisha na suala hili. Badala yake watumishi wa umma wanatakiwa kuzingatia maadili mema ya kazi zao, kuzingatia taratibu, kanuni na sheria ili kuboresha utoaji wa huduma katika sekta zote.

·        Vilevile Dr. Nchimbi aliwasisitiza wafanyakazi waone umuhimu wa kijiendeleza kielimu ili kuzidi kuboresha utoaji wa huduma zao na utendaji wao kwa ujumla. Aliwataka wafanyakazi watumie fursa zilizopo kama vile vyuo kujiendeleza. Aliwaagiza waajiri (Katibu Tawala Mkoa) kutoa kipaumbele cha ruhusa kwa ya kusoma kwa watumishi wa serikali wanaotaka kujiendeleza kielimu kupitia chuo kikuu huria cha Tanzania tawi la Dodoma kwa kuwa hawaaribu ratiba ya kazi kwani wanaweza kusoma huku wanafanya kazi kuitumikia serikali.

Alikemea tabia ya watumishi/wafanyakazi wasiopenda kujiendeleza kielimu kwa kubakia kwenye daraja moja la elimu kwa muda mrefu bila kujiendeleza na kusema kuwa inazorotesha utendaji na ufanisi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza hilo la wafanyakazi wa sekretarieti ya Mkao wa Dodoma  ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa Dodoma Ndugu Rehema Madenge alitoa Rai kwa wafanyakazi wa serikali wawe na desturi ya kubadilika kuanzia sasa na kusisitiza alichokieleza mkuu wa mkoa hususani sera ya Tenda kwa Matokeo Makubwa Sasa (Big Result Now).

Imetolewa na:
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma

Idara ya Habari
WAZIRI wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, akimkabidhi Stashahada mmoja wa wahitimu wa Shule ya Biashara ya Aseki iliyoko Dodoma, ambapo jumla ya wahitimu 158 walihitimu kwa ngazi ya Stashahada na Astashahada.
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu Mzee Constantine Munishi Kyara wakitoa heshima za mwisho kwenye ibada ya mazishi iliyofanyika mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro adre wa Kanisa Katoliki Parokia ya Moshi Mjini, akiongoza ibada ya mazishi ya Marehemu Mzee Constantine Munishi Kyara iliyofanyika eneo la Rau, nje kidogo ya mji wa Moshi, Kilimanjaro juzi Ibada ya mazishi ikiendelea. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA