Mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga,Mkoani Iringa kupitia tiketi ya chama cha CCM,Godfrey Mgimwa akiwa amebebwa juu na wananchi/Wanakijiji wa kijiji cha Ilala Simba kilichopo Kata ya Nzihi,Iringa Vijijini mapema leo jioni,alipokwenda kuzungumza nao na kuomba ridhaa yao ya kuwaongoza kama Mbunge.
Mgombea
Ubunge Jimbo la Kalenga,Mkoani Iringa kupitia tiketi ya chama cha
CCM,Godfrey Mgimwa akizungumza na Wananchi/Wanakijiji wa kijiji cha
Ilala Simba kilichopo Kata ya Nzihi,Iringa Vijijini mapema leo
jioni,akiomba kura na ridhaa yao ya kuwaongoza kama Mbunge. Ndugu Mgimwa
alisema kuwa Wananchi Wamuamini kwani anafahamu changamoto zilizopo na
majibu ya kuzitatua anayo "Nimefanya utafiti wa kutosha hivyo najua
changamoto zinazotukabili,nipeni nafasi ili niweze kuzitatua kupitia
Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010" alisema Mgimwa.
Naibu
Meya wa Manispaa ya Iringa,Mh.Gervas Ndaki akiwa amepiga magoti
ikiashiria kutoa heshima kwa wananchi kwa ajili ya kuwaomba kura kwa
ajili ya Mgombea wa CCM,kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika
kijiji cha Ilala Simba kata ya Nzihi mkoani humo.
Baadhi ya Wazee wa kijiji cha Ilala Simba kilichopo Kata ya Inzihi,Iringa Vijijini,wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga mapema leo jioni.
Wanachama wa chama cha CCM na wananchi wakishangilia jambo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanywa na CCM mapema leo jioni,ambapo mgombea wa chama hicho,Godfrey Mgimwa alifika na kujinadi kuomba kura na ridhaa ya kuongoza jimbo hilo.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga,Mkoani Iringa kupitia tiketi ya chama cha CCM,Godfrey Mgimwa akipokelewa kwa shangwe mapema leo jioni katika kijiji cha Magubike,kabla ya kuzungumza nao kwenye mkutano wake wa hadhara,katika safari nzima ya kuomba kura na ridhaa ya kuwaongoza kwa nafasi ya Ubunge.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Mwigulu Nchemba akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika mapema leo jioni katika kijiji cha Magubike,ikiwa ni sehemu ya kumnadi mgombea wa chama hicho,Ndugu Godfrey Mgimwa ambaye anagombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Kalenga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...