Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana Taasisi ya Malaria No More na THT(Tanzania house of talent) leo wameitangaza rasmi nambari maalum ambayo wateja wanaotumia huduma za Vodacom wanaweza kuitumia kupata taarifa zinazohusiana na ugonjwa wa malaria.

Ili mteja kuweza kupata taarifa hizo zinazohusisha jinsi ya kujikinga, tiba na masuala mengine mbalimbali ya Malaria anachopaswa mteja kufanya ni kujiunga kwa kutuma neno "Malaria" au "Mzinduka" kwenda nambari 15760 bila malipo.

Ujio wa huduma hii ni sehemu ya kampeni kabambe ya Mzinduka inayolenga kuongeza kasi katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria hapa nchini ambayo Vodacom Foundation ni mshirika wake.

Nambari hiyo imetangazwa jijini dar es salaam kwenye uwanja wa taifa muda mfupi kabla ya kuanza kwa mechi kati ya Simba na Yanga kwa lengo la kuwashirikisha washabiki wa soka nchini kuunga mkono kampeni hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...