Na Dixon Busagaga
wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
MAHAKAMA kuu
kanda ya Moshi imetoa adhabu ya
kunyongwa hadi kufa kwa washtakiwa wawili raia wa Kenya katika
kesi ya mauaji ya askari Polisi, Pc Michael
Milanzi, wakati wa tukio la uporaji wa
fedha katika benki ya NMB tawi la Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Mbali na hukumu
hiyo iliyosomwa na Jaji mfawidhi wa
Mahakama kuu, Kakusulo Sambo kwa zaidi ya saa, nne ,Mshatakiwa wa tatu katika
kesi hiyo ,Karisti Kanje(Mtanzania) yeye amehukumiwa kutumikia kifungo cha
miaka mitano(5) jela kwa kosa la kuhifadhi na kutorosha watuhumiwa wa mauaji ya
askari polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...