Uongozi
wa Kampuni ya Reli Tanzania -TRL unaWAtaARIFU WAKAZI WA JIJI NA
WANACHI KWA JUMLA kusitishwa kwa huduma ya treni ya jiji hapo kesho Jumamosi
Julai 19, 2014, ili kupisha ukarabati wa miundo mbinu ya reli KATI ya Dar
Stesheni hadi Ubungo Maziwa itakayofanyika kwa siku za Jumamosi na Jumapili.
Hata
hivyo huduma hiyo itarejea tena kama kawaida kuanzia Jumatatu Julai 21, 2014 . Atakayesikia
AU KUSOMA TAARIFA HII amuarifu na mwenziye.
Uongozi
wa TRL unasikitika kwa usumbufu utakaojitokeza.
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa
niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Mhandisi Kipallo Aman Kisamfu,
Dar es Salaam,
Julai 18, 2014
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...