Mhe. Balozi Tuvako Manongi, Muwakilishi wa Kudumu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, jana Jumatano ameungana na Mabalozi wengine wanaoziwakilishi Nchi zao katika Umoja wa Mataifa, kutia saini kitabu cha maombolezo kilichofunguliwa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Udachi ( Netherlandes) katika Umoja wa Mataifa kuwakumbuka watu 298 waliopoteza maisha baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria ya MH17 inayomilikiwa la Shirika la Ndege la Malaysia kuangushwa katika eneo la Mashariki ya Ukraine wiki iliyopita. Idadi kubwa ya abiria hao walikuwa ni raia wa Udachi.

 Balozi Tuvako  Manongi,akiandika katika kitabu  cha maombolezo kilichofunguliwa katika Uwakilishi wa Kudumu wa  Udachi ( Nertherlands) kuomboleza familia 298   ambazo maisha yao yamekatishwa baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria MH17 kuangushwa nchini Ukraine wiki iliyopita.
 Balozi Manongi akiwaombea marehemu
 Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi, akizungumza machache na  Muwakilishi wa Kudumu wa   Udachi katika Umoja wa Mataifa,  Balozi  Karel van Oosterom mara baada ya Balozi Manongi  kusaini kitabu cha maombolezo.
 "Asante sana kwa kuja  kutufariji katika kipindi hiki kigumu, asante sana, natambua vema ushirikiano  mzuri uliopo baina ya  serikali zetu".  ndivyo aliyosikika akisema  Muwakilishi wa Kudumu wa Udachi Balozi  Karel van Oosterom

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...