Katika kuendeleza wajibu wake wa kutoa mafunzo ya muda mfupi, Chuo cha Diplomasia kimeendesha mafunzo ya juma moja ya Itifaki na Uhusiano ‘PROTOCOL AND PUBLIC RELATIONS’
Mafunzo haya yalilenga kuwaongezea uwezo maafisa mbali mbali kutoka serekalini na sekta binafsi. Mafunzo haya ni muendelezo wa mafunzo ya muda mfupi yatolewayo na Chuo cha Diplomasia, mathalan usuluhishi na utatuzi wa migogoro (Conflict Resolution and Mediation skills) na Itifaki na Uhusiano ( Protocol and Public Relations)
Mafunzo hayo yalihusisha
maofisa wa kada mbalimbali kutoka idara za Serikali na sekta binafsi kama Benki
Kuu ya Tanzania, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Baraza
la Wawakilishi Zanzibar, Chuo cha Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Meya Kinondoni, NSSF,
Idara ya Uhamiaji, Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Umoja wa
Mataifa (UN) na Clouds Media.
Mafunzo hayo ya juma moja
yaliyofanyika Kurasini Dar es salaam, washiriki walijifunza jinsi ya kuratibu
itifaki za dhifa, sherehe za kitaifa na mikutano mingine mbali mbali. Pia
walijifunza Diplomasia, uhuisiano wa umma na namna bora ya kuandaa taarifa kwa
ajili ya mawasiliano na umma.
Akifunga mafunzo hayo, Mkuu wa Idara ya Utafiti,
Uchapishaji, Ushauri na Kozi fupi, Bw. Juma M. Kanuwa alisisitiza kwamba
mafunzo hayo yatawasaidia maofisa hao kuboresha utendaji wa kazi zao.
“Kazi zinazohusiana na itifaki na uhusiano wa umma (Protocol and Public Relations) zinahitaji
utaalam ambao utamfanya mtu aweze kutimiza majukumu yake kwa ufasaha na kufikia
malengo na matokeo mazuri. Hivyo mafunzo haya ya Itifaki na mengine yote
yanayotolewa na Chuo cha Diplomasia yana lengo la kuwajengea uwezo na utaalam
washiriki wote ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na kupata matokeo bora,” alisema.
Akaongeza kuwa, kutokana na uhitaji mafunzo haya
yatarudiwa tena Tarehe 18 -22 Agasti 2014 hapa chuo cha Diplomasia,
na kuwataka wale wote wanaohitaji wafike chuoni ama kupiga namba 0713667303 kwa maelezo zaidi na kupewa
utaratibu.
Kwa kawaida wawezeshaji wa mafunzo hayo ya muda
mfupi katika Chuo cha Diplomasia, huwa ni mabalozi na wakufunzi waliobobea
katika mambo ya Diplomasia na hivyo kuwapa washiriki uzoefu na mafunzo ya kiutendaji
zaidi ili kuwajengea uwezo na ufanisi katika kuboresha majukumu yao.
Mshiriki Baby Kabaye wa Clouds Media akionesha cheti chake kwa furaha
Mshiriki Godfrey Makupa wa GRM Productions akifurahia cheti chake
Washiriki wakiwa darasani
Mshiriki Baby Kabaye wa Clouds Media akifafanua jambo.
Imetolewa na Shoo Innocent, Afisa Uhusiano
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...