Watoto wanaolelewa katika kituo cha yatima cha Umra kilichopo Magomeni jijini Dar es Salaam, wakiangalia simu ya mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Shamsa Hamud(anaewashuhudia) Wafanyakazi wa kampuni hiyo walifika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa msaada wa vyakula mbalimbali na fedha taslimu zilizochangwa na wafanyakazi waislamu na marafiki zao kwa ajili ya watoto hao kusherehekea sikukuu ya Idd.
Watoto wanaolelewa katika kituo cha Yatima cha Umra kilichopo Magomeni jijini Dar es Salaam, wakifurahia moja ya zawadi walizopewa msaada na Wafanyakazi wa Kiislamu na marafiki zao wa Vodacom Tanzania, Vikiwemo vyakula mbalimbali na fedha tasilimu kiasi cha shilingi 380,000 kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Idd
Iman Abdalah (wapili kushoto) wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Umra akiongoza swala kwa ajili ya watoto wenzake kuwashukuru wafanyakazi wa Kiislamu na marafiki zao wa Vodacom Tanzania waliowachangia vitu mbalimbali vikiwemo vyakula na fedha taslimu Tsh 380,000. Kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Idd.Kushoto ni mfanyakazi wa kampuni hiyo Shomari Shomari na kulia ni Salum Mwalim.
Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania ,Shomari Shomari akimkabidhi fedha taslimu kiasi cha Tsh 380,000 Mkuu wa Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Umra kilichopo Magomeni jijini Dar es Salaam,Bi.Rahma Kishumba,Fedha hizo zilichangwa na wafanyakazi waislamu wa kampuni hiyo na marafiki zao kwa ajili ya kuwanunulia viatu vya sikukuu ya Idd watoto wa kituo hicho.
Mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha yatima cha Umra Iman Abdalah ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza akipokea msaada wa ndoo ya mafuta ya kupikia kutoka kwa Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Yessaya Mwakifulele wakati walipopelekewa msaada wa vitu mbalimbali na fedha taslimu kiasi cha Tsh 380,000 zilizochangwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo na marafiki zao kwa ajili ya watoto hao kusherehekea sikukuu ya Idd,Kulia ni Salum Mwalim.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,Shomari Shomari (kushoto) na Salum Mwalim(kulia) wakiwakabidhi moja ya gunia la mchele watoto wanaolelewa katika kituo cha Yatima cha Umri kilichopo Magomeni Jijini Dar es Salaam kwa ajilia ya kusherehekea sikukuu ya Idd, Jumla ya Vitu mbalimbalikii ikiwemo fedha taslimu kiasi cha Tsh 380,000.zilizochangwa na wafanyakazi wa Kiislamu wa Vodacom na marafiki zoa vilitolewa msaada katika kituo hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...