Na Mahmoud Zubeiry
MSHAMBULIAJI Reuben de La Red amefunga mabao matatu peke yake, wakati magwiji wa Real Madrid wakiiangusha Tanzania Eleven 3-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo.
De la Red alimfunga bao moja kipa Mwameja Mohamed kipindi cha kwanza na kipindi cha pili akamtungua mara mbili Manyika Peter, wakati bao pekee la Stars lilipatikana baada ya  Real kulijifunga wenyewe kupitia kwa Roberto Rojas.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alimkabidhi mpira uliotumika De La Red baada ya kuutia saini yake juu yake, kabla ya kuwakabidhi Kombe Real Madird kwa ushindi wao huo.
Katika mchezo huo, ambao wachezaji waliingia na kutoka, Real Madird walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 10, kupitia kwa De La Red ambaye alimalizia pande tamu la Luis Figo.
Mpira uliozaa bao hilo, ulianzia kwa kiungo Christian Karembeu, aliyezuia shambulizi la Tanzania na kuanzisha shambuizi zuri lililozaa matunda, akiuvuka msitu wa wachezaji wa wenyeji kwa umahiri mkubwa.
Tanzania Eleven ilisawazisha dakika ya 45 baada ya kona ya Mecky Mexime kuzua kizaa langoni mwa Real na Roberto Rojas akajifunga katika harakati za kuokoa baada ya Kali Ongala kuuparaza kwa kichwa. 
Kipindi cha pili, De la Red alifunga bao la  pili kwa penalti dakika ya 81 baada ya yeye mwenyewe kuchezewa rafu na Habib Kondo kwenye eneo la hatari.
Awali ya hapo, Figo alimtoka vizuri beki Mecky Mexime na kuingia hadi kwenye eneo la hatari akiwa kwenye nafasi ya kufunga akampasia De La Red ambaye alipiga nje.
De la Red alikamilisha hat trick yake dakika ya 88 baada ya kuwazidi maarifa mabeki wa Tanzania Eeleven. 
Wachezaji wa timu zote mbili wanatarajiwa kula chakula cha usiku na Mheshimiwa Rais Ikulu baadaye leo. 

Luis Figo akimtoka Athumani China
Beki wa Tanzania, Nsajigwa Shadrack kushoto akimtoka Fernando Sanz wa Real Madird
Reuben De La Red kushoto amefunga mabao matatu peke yake Real ikishinda 3-1 Uwanja wa Taifa

 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Real Madrid Legends. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Sio mbaya tujipange nasi tukienda kwao tuwapige 6 kwa nunge

    ReplyDelete
  2. Wakongwe wameperfom kuzidi starz

    ReplyDelete
  3. Mm nashauri tim yao ya wakongwe wasiivunje kila likitokea tamasha wawe wanacheza itawasaidia kuwa na mazoezi na vile vile upendo vile vile kama watakuwa na mfuko maalum kwa wachezaji wastaafu ikiwa moja wao kapata matatizo utawasaidia

    ReplyDelete
  4. How wrong can one be.Niliposikia ni wakongwe nilidhani kuwa ni vibogoyo na wana mikongojo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...