Na Magreth Kinabo, Dodoma
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuonana na Viongozi wa Vyama vya Siasa vinavyounda Kituo cha Demkrasia Tanzania(TCD) kabla ya mwisho wa wiki kwa lengo la kushauriana.
Kauli hii imetolewa na Mwenyekiti wa TCD,Mhe. John Cheyo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Bunge.
Mhe. Cheyo alisema Rais Kikwete amekubali kuonana nao kufutia kikao chao walichokaa kwa pamoja ambacho kilihusisha viongozi wakuu wa vyama hivyo, Agosti 23,mwaka huu, ambapo walijadili na kutafakari maendeleo ya mchakato wa Katiba Mpya.
Alisema viongozi hao, katika kiako hicho cha pamoja na mambo mengine waliazimia kutafuta nafasi ya kuonana na Rais Kikwete kwa ajili ya lengo hilo, ambapo kufutia azimio hilo, Mwenyekiti huyo aliwasiliana naye alilipokea azimio hilo na kuahidi kufanya hivyo.
“Tutalishauri taifa kwa maoni tutakayokubaliana na Rais,” alisema Mhe. Cheyo bila ya kutaja agenda juu ya jambo hilo.
Aliongeza kuwa watazunguza na kutafakati ili kuhimarisha amani na mchakato huo utoe matunda mema.
Mhe. Cheyo alisema kikao hicho kilifanyika na kuhusisha vyam vyote vilivyoko katika TCD.
Alisema hii ni mara ya kwanza kwa TCD kumwomba Rais Kikwete kuonana naye na kukubali ombi hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...