Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisaini moja ya
leseni za uchimbaji madini kwa wamiliki waliokidhi vigezo vya kuapatiwa
leseni. Anayeangalia ni Mwanasheria Wizara ya Nishati na MadinI Phines
Sijaona.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza mmoja
wa waombaji wa Leseni za uchimbaji madini, Mark Stanely mmiliki wa
kampuni ya Bafex Tanzania Limited (Kanda ya Kusini Magharibi) wakati wa
kikao cha kusaini leseni za uchimbaji madini zilizokidhi vigezo.
Kamishna Msaidizi anayeshuhgulia Leseni, Wizara ya Nishati na Madini,
Mhandisi John Nayopa, akifafanua jambo wa wamiliki wa kampuni ya
Gemini Exploration & Mining Service Limited mara baada ya Waziri wa
Nishati na Madini, Sospeter Muhongo kumaliza kusaini leseni hizo.
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amewataka
wamiliki na waombaji wa leseni za kuchimba madini kuhakikisha
wanayaendeleza maeneo yao kwa kufanya kazi katika muda walioomba
kulingana na leseni hizo la sivyo watafutiwa leseni zao kwa mujibu wa
sheria ya madini.
Waziri Muhongo ameyasema hayo wakati akisaini leseni za Kampuni
mbalimbali zilizokidhi vigezo vya kupatiwa leseni za uchimbaji madini
katika maeneo mbalimbali nchini na kuongeza kuwa, kuanzia sasa Wizara
haitaruhusu wamiliki wa leseni za madini kuuza maeneo yao kwa wamiliki
wengine na kubadilisha majina ya kampuni kutoka kwa mmiliki mmoja
kwenda mwingine badala yake itaruhusu endapo pande mbili zitaingia ubia.
“Hatutakubali wamiliki wa leseni kuuza maeneo yao na kubadili jina kutoka
kwa mmliki mmoja kwenda mwingine badala ya kuyaendeleza, lakini kama
wanaingia ubia hilo linakubalika” alisisitiza Muhongo.
Kauli ya Waziri imekuja baada ya kubaini kuwa, baadhi ya wamiliki wa
leseni za uchimbaji madini kutokuyaendeleza maeneo yao kwa muda
mrefu pindi wanapopewa leseni na badala yake kuyauza na kubadili majina
ya kampuni jambo ambalo linachochea migogoro katika maeneo husika.
“Wananchi wanategemea mara baada ya kampuni kupewa leseni
waombaji waendeleze maeneo yao lakini badala yake maeneo yanakaa
bila kuendelezwa jambo ambalo linaibua migogoro”, aliongeza Muhongo.
Aidha, ameongeza kuwa, hatua hiyo inalenga kuwafanya waombaji na
wamiliki kuwajibika na kufanya kazi kisasa badala ya kufanya kwa mazoea.
“Hatutaki waombaji wafanye kazi kizamani, hatutaki kupotezeana muda
katika hili”, alisisitiza Waziri.
Kampuni zilizopata leseni za uchimbaji, ni pamoja na Bafex Tanzania
Limited (Kanda ya Kusini Magharibi) Autrad Mining Company Limited,
Nyang’wale Diamonds Limited (Kanda ya Kati Magharibi) na Paulo
Sungura na Joyce Abinel Sekwao (Kanda ya Magharibi).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...