MAREHEMU DAFROSA KWEKA MSENGI 
11-05-1970 - 24-10-1999

Leo umetimiza miaka kumi na tano(15) tangu ulipoitwa mbinguni kwa BABA. Kweli ua zuri limerudi kwenye Bustani ya Eden.

Hatuna cha kusema, tumebaki kushukuru tuu maana imeandikwa tushukuru kwa kila jambo. Tunakumbuka sana Upendo na Ushirikiano uliokuwa nao, Uchapakazi na Uzuri uliokuwa nao. Kweli ulikuwa mfano wa kuigwa, hata kazini kwako wanakukumbuka.

Dafrosa, tupo kama ulivyotuacha ila tumepungukiwa tena na mama yako URSULA ambaye tumemzika hivi karibuni baada ya kuugua kwa muda mrefu sana. Imani yetu ni kuwa ipo siku wote tutakutana tena paradiso. 

 Unakumbukwa sana na mumeo mpendwa DR. IBRAHIM MSENGI, mwanao wa pekee JESCA, nduguzo JANE,FESTO,EUGENIA,ELIZABETH,CECILIA na THADEI,shangazi yako mpendwa SR. DEVOTHA KWEKA CDNK, Wajomba,Mashemeji na Mawifi wa kwa BASI wote,WAKWEKA wote wa NARUMU,kina MSENGI wote wa MKALAMO – SINGIDA,Wafanyakazi wa idara ya fedha za Kigeni – Benki kuu,Majirani wa TEMEKE –MIKOROSHINI na TABATA ,Ndugu,Jamaa na Marafiki wote. 

“RAHA YA MILELE UMPE Eee Bwana…….”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ohh Dafroza!!!!!!!!! Sisi bado tunapambana!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...