Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akihutubia Mkutano wa pili wa Kimataifa kuhusu Lishe na
Virutubisho (ICN2) uliofanyika katika ukumbi wa Makao Makuu ya Shirika
la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) jijini Rome, Italia juzi
Novemba 19, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akijadiliana jambo na baadhi ya wajumbe kutoka Tanzania wakati wa
mkutano huo wa ICN2 (kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Italia,
James Nsekela na Msaidizi wa Rais katika Masuala ya Lishe Dkt. Wilbald
Lorri.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mpango Maalum wa
Chakula Duniani (WFP) Ethria Cousin (kushoto) na Balozi Wilfred Ngirwa
wakati wa mkutano huo wa ICN2, uliofanyika juzi Novemba 19, 2014, Jijini
Rome Italy.
Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, akifuatilia hotuba mbalimbali za viongozi
walioshiriki katika Mkutano huo wa ICN2. Kulia ni Mfalme Letsie III wa
Lesotho.
Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal (katikati) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi
Mtendaji wa FAO Jose Graziano da Silva, wakati alipomtembea ofisini
kwake na kufanya naye mazungmzo, juzi Novemba 19, 2014. Kushoto ni
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid. Picha na OMR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...