ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Fredrick Mwakalebela Desemba 26 anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Krismasi mkoani Iringa.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama Mwakalebela anatarajia pia kuwaongoza waumini mbalimbali mkoani humo kwa lengo la kumtukuza Mungu kupitia waimbaji mbalimbali hapa nchini.

Msama alisema Mwakalebela atafanikisha lengo la kusaidia wenye uhitaji maalum kama Yatima, Wajane na walemavu ambao wanahitaji msaada mkubwa kutoka kwa wadau mbalimbali.

Msama alisema Mwakalebela ni mdau ambaye anatakiwa aendane na kauli mbiu ya Tanzania ni yetu, Tuilinde na Kuipenda ambayo inachochea wadau ambao wanatakiwa kusaidia wadau hao.

Tamasha hilo linatarajia kuanza Desemba 25, kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kabla ya kuhamia Iringa  na kumalizia Desemba 28 Wilayani Songea kwenye uwanja wa Majimaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...