Waziri wa Ujenzi ,Dkt John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mkuu wa wilaya ya Same  Mhe. Herman Kapufi wakati akifanya ukaguzi wa barabara kutoka Korogwe/Mkumbara hadi Same yenye urefu wa  Kilomita 172, inayojengwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia (WB).
Waziri wa Ujenzi Dkt ,John Magufuli akizungumza na wakandarasi kutoka kampuni ya Dot Services ya nchini Uganda inayo jenga barabara ya Korogwe/Mkumbara hadi Same.
Waziri wa Ujenzi Dkt Magufuli akizungumza jambo wakati alipokutana na watenadji wakuu wa kampuni ya Dot Services wanaojenga barabara ya Korogwe/Mkumbara hadi Same.

Na Dixon Busagaga wa
Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI imetaka wakandarasi wa barabara nchini, kutekeleza miradi ya barabara kwa wakati na ubora unaokubalika  ili kuwaonesha wahisani namna ambavyo fedha  wanazotoa zinafanya kazi iliyokusudiwa kwa kuonesha thamani halisi ya mradi husika.
 Hayo yalielezwa juzi na waziri wa Ujenzi, Dkt John Magufuli wakati akifanya ukaguzi wa barabara kutoka Korogwe/Mkumbara hadi Same yenyeurefu wa  Kilomita 172,inayojengwa kwa fedha za mkopo kutoka benki ya 
dunia (WB).
Dkt Magufuli  alisema changamoto mbalimbali  zinazojitokeza katika ujenzi wa barabara hazina budi kutafutiwa ufumbuzi wa mapema, ili kutoa nafasi kwa rais Jakaya Kikwete kuifungua na kuruhusu wananchi kuendeleza shughuli za uzalishaji mali.
Alisema katika kuhakikisha barabara hizo zinadumu ni vyema kwa Tanroad  kutafuta mizani inayohamishika (Mkeka) ili kuwadhibiti wasafirishaji wasio waaminifu ambao wamekuwa wakibeba mizigo mikubwa kwa tamaa ya fedha.
" Kukamilika kwa barabara hizi kutarahisisha shughuli za kiuchumi kwa mikoa hii inayopitika ,Nikuombe katibu mkuu kwa kushirikiana na wahandisi, kuhakikisha hizi Bil 200 ambazo ni mkopo hazipotei, nataka mdhibiti magari yanayobeba mizigo mikubwa....wakati fulani tulishika magari yenye uzito wa Tani 96 hadi 102, uzito unaokubalika kisheria ni
Tani 56 tu"alisema Magufuli..

Naye mtendaji mkuu wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mhandisi Partick Mfugale alimweleza Wazri Magufuli kuwa barabara ya kutoka Korogwe/Mkumbara hadi  Same yenye urefu wa  Kilomita 172 inajengwa kwa
awamu mbili tofauti.
Alisema barabara hiyo ambayo  sehemu ya barabara inatoka Dar es salaam ,Chalinze,Arusha  hadi Nairobi, imegawanywa mara mbili, Korogwe/Mkumbara  Km  76 kinachojengwa na kampuni ya Strabag  ya Ujerumani na Mkumbara/Same  Km 96 inajengwa na kampuni ya Dott services ya Uganda.

Mfugale alisema   ujenzi  wa kipande cha Korogwe/Mkumbara ulianza Mei,2012 na kumaliza Desemba 3,2014 na uligharimu Bil sh 87.805 kwa mkandarasi na kiasi cha Sh Bil 6.787 kwa mhandisi msimamizi kampuni ya Nicholas O'Dwyer Ltd ya nchini Ireland kwa miradi yote miwili. 
Alisema Kazi alizofanya katika mradi huo ni kubandua na kusaga lami iliyokuwepo na kuweka lami nyingine mpya kwa mfumo imara zaidi,kuimarisha daraja la Mombo, kujenga makalvati  makubwa 18 na madogo 175 na sasa kazi imekamilika na yupo katika muda wa uangalizi.
Mradi wa pili ni Mkumbara/Same Km 96 wenye gharama ya Bil 103.8kupitia mkandarasi wa Dott services ya Uganda ambao walikubwa na changamoto kadhaa ambazo sasa zimerekebishwa na sasa ameanza ujenzi kwa kasi.
Alisema makubaliano ni kujenga angalau Km 4 kwa kila mwezi ambapo sasa amekamilisha asilimia 67 ya mradi husika na matarajio ni kukamilishamradi wote hadi kufikia muda wa mkataba ambao ni Disemba mwaka huu.
Mfugale alisema mkandarasi huyo tayari amelipwa kiasi cha Sh Bil 44.5na kazi inaendelea vizuri ingawa alitaka mkandarasi huyo kuhakikisha kasi ya ujenzi anayofanya sasa  ilingane na ubora wa barabara inayojengwa.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...