Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
JAMII imeaswa kutumia elimu sahihi ya matumizi ya vyandarua katika kuweza kupambana na ugonjwa wa malaria.
Hayo ameyasema leo Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Michael John wakati akitangaza siku ya malaria duniani inayoadhimishwa kila mwaka Aprili 25 iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini ,Dar es Salaam,amesema jamii imetakiwa kutumia elimu sahihi katika kupambana na malaria.
Amesema malaria imepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2012 na kufikia asilimia 10 mwaka huu hiyo imetokana na juhudi za wizara ya afya na mashirika mbalimbali kutoa elimu juu kujikinga ugonjwa huo ambao awali ulikuwa ikichangia vifo vya watoto chini ya miaka mitano kutokana na kutokana na kukosa vyandarua.
John amesema katika madhimisho ya siku ya malaria ambayo itaadhimishiwa jijini Dar es Salaam yatakwenda sambamba na uzinduzi wa ugawaji wa vyandarua milioni 24 vilivyotolewa na Wizara ya Afya ikiwa lengo kupambana na ugonjwa wa malaria. Amesema mikoa ambayo iko katika viwango vya juu vya ugonjwa wa Malaria ,Lindi,Geita ,Kigoma pamoja na Mara hali ambayo elimu inahitajika kwa mikoa hiyo katika matumizi sahihi ya vyandarua kuweza kufikia asilimia sifuri.
John amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya Maralia ni Wekeza kwa Maisha ya Baadae ,Tokomeza Malaria na maadhimisho hayo itatumika sehemu ya kuelimisha juu ya kutambua dalili za malaria kuwahi katika kituo cha kutolea huduma,ili kupima na kudhibitisha uwepo wa vimelea kabla ya kuanza kutumia dawa kwa kuwa sio kila homa inasababishwa na Malaria.
KAIMU
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Michael John
akiandika maswali aliyeulizwa na waandisshi wa habari (hawapo pichani )
juu ya maadhimisho ya siku ya malaria duniani iliyofanyika leo katika
ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini ,Dar es Salaam,Kushoto ni Mwakilishi wa
Shirika la Afya Duniani -Tanzania ,Dk.Ritha Njau ,Kulia ni Naibu
Mkurugezi Kituo cha Utafiti cha Ifakara,Dk.Abdulrazq Badru.
Kaimu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Michael John
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitangaza
siku ya malaria duniani inayoadhimishwa kila mwaka Aprili 25
iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini ,Dar es
Salaam,Kushoto ni Naibu Mkurugezi Kituo cha Utafiti cha Ifakara
(IHI),Dk.Abdulrazq Badru.
Meneja
wa Mpango wa Kudhibiti Malaria wa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii,DK.Ben Mandike akisisitiza jambo kwa waandishi habari juu ya
maadhimisho ya siku ya malaria Duniania iliyofanyika leo katika ukumbi
wa Mwalimu Nyerere jijini ,Dar es Salaam.
Watalaam
na watafiti wa malaria wakifatilia mada mbalimbali katika mkutano wa
tano wa taarifa ya miaka mitano ya utafiti wa Malaria na hali halisi ya
sasa iliyoandaliwa na Kituo cha Utafiti cha Ifakara na Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere
jijini ,Dar es Salaam.
Hatutendi haki kuongelea vyandarua tu wakati hoja ya msingi ya mbinu za kutokomeza mmbu kama vile kurejesha matumizi ya DDT ambayo wakubwa duniani baada ya kumaliza mbu kwao wakaipiga marufuku nasi tukaunga bogi kama wendawazimu.
ReplyDelete