Na  Bashir  Yakub.

Katika  migogoro  ya  ardhi  yapo  mambo  mengi  ambayo  hujitokeza. Yumkini  hii  yote  huwa  ni  katika  kusaka  haki.  Liko  jambo  moja  ambalo  ni  muhimu  watu  kulijua  hasa  wale  ambao   tayari  wamejikuta  katika  migogoro  ya  ardhi.  Mara  nyingi  imekuwa  ikitokea  pale  ambapo  mtu  fulani  ana  mgogoro  wa  ardhi  na  mtu  mwingine  kumwendea  polisi  na  kumshitaki  kwa  jinai  ya  kuvamia  ardhi  yake( criminal trespass). Ni  kweli  jambo  hili  lipo  kisheria   lakini  haliko  moja  kwa  moja   kama  ambavyo  watu  wamekuwa  wakilichukulia kama  ambavyo  tutaona  badae.

1.JINAI  YA  UVAMIZI  WA  ARDHI.

Nimesema  hapo  juu  kuwa  jinai  ya  uvamizi  wa  ardhi  huitwa  “criminal trespass”.  Kosa  hili   huhesabika  limetendeka  pale  ambapo  mtu  huingia  katika  ardhi  ya  mtu mwingine  bila  ruhusa  au  mamlaka  yoyote  ya  kisheria  kutoka  kwa  mmiliki  au  penginepo  huku  akiwa  na  nia  mbaya.  Mtu  anapokuwa  amefanya  hivi  tayari huhesabika  ametenda  jinai  ya  uvamizi  wa  ardhi. Ardhi  kwa  maana  hii  hapa  hujumuisha  nyumba, shamba, kiwanja   na  kila  kitu ambacho  huitwa  ardhi.  

2.  KESI  YA MADAI   YA  UVAMIZI  ARDHI.

Hapo  juu  nimeeleza  kosa  hili  la  uvamizi  ardhi lakini  katika   upande  wa  jinai. Yafaa  tujue  kuwa  kosa  hili  pia  ni  madai.  Kwa  hiyo  kama  hapo  juu  tumeona  anayevamia  ardhi  ya  mtu  anaweza  kufunguliwa  kesi  ya  jinai  basi  tuelewe  kuwa   kwa  kosa hilohilo  waweza  fungua  pia  kesi  ya  madai.  Tofauti  ya  kesi  ya  madai  na  jinai  katika  kosa  hili  ni  kuwa  katika  kesi  ya  jinai  mtuhumiwa  akipatikana  na  hatia  basi  atatakiwa  kwenda jela au  adhabu  nyingineyo  wakati  katika  kesi  ya  madai  mlalamikiwa  akipatikana  na  hatia  basi  atatakiwa  kulipa  fidia   kwa  mtendewa.  Kwa  hiyo  uamuzi  wa  kesi  gani  mlalamikaji  afungue  uko  mikononi  mwake. Aidha  yawezekana  pia  kufungua  kesi  zote  mbili  kwa  pamoja  yaani mahakama   fulani  ukafungua  kesi  ya  madai  na  mahakama  nyingine  ukafungua  kesi  ya  jinai  kwa wakati mmoja.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...