Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Cosmas Swai, akizindua kampeni mpya ya kuhamasisha Faida na Matumizi ya Uzazi wa Mpango jijini Dar es Salaam jana, kampeni itakayotekelezwa mkoani Kigoma. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la, World Lung Foundation (WLF), Nduke Mwakatundu (mwenye tai) na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dk.Leonard Subi (watatu kulia) na baadhi ya wafanyakazi wa (WLF).
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la World Lung Foundation (WLF), Nduke Mwakatundu, akijibu maswali ya waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya kuhamasisha faida na matumizi ya uzazi wa mpango jijini Dar es Salaam jana, mpango utakaotekelezwa mkoani Kigoma. Kushoto ni Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga Wizara ya Afya, Dk.Cosmas Swai na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dk.Leonard Subi.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dk. Leonard Subi, akizungumza wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa kampeni mpya ya kuhamasisha faida na matumizi ya uzazi wa mpango jijini Dar es Salaam jana, mpango utakaotekelezwa mkoani Kigoma chini ya Shirika la World Lung Foundation (WLF).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...