THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Gazeti la Mwananchi la leo, Jumatatu, Julai 27, 2015, kwenye ukurasa wake wa 26 limechapisha habari yenye kichwa cha habari, “Marais watano wanaotajwa kuongoza kwa mishahara minono barani Afrika ni hawa hapa”.

Katika habari hiyo ambayo gazeti hilo linadai chanzo chake ni “uchambuzi wa mtandao wa African Review” inadaiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, anashilikia nafasi ya tano miongoni mwa viongozi 38 wa nchi za Afrika wanaolipwa mshahara mnono zaidi.

Gazeti hilo linadai kuwa Rais Kikwete analipwa Dola za Marekani 192,000 kwa mwaka, ikiwa ni malipo ya Dola za Marekani 16,000 kwa mwezi.

Habari hizi siyo za kweli. Ni uongo na uzandiki. Ni uzushi mtupu na ni uzushi wa hatari.

Mshahara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwezi ama kwa mwaka haufikii na hata wala kukaribia kabisa kiwango kinachotajwa na Gazeti la Mwananchi.

Tangu Uhuru, mwaka 1961, Rais wa Tanganyika na baadaye tangu mwaka 1964 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa miongoni mwa viongozi wanaolipwa mishahara ya chini kabisa duniani.

Mshahara wa Rais wa Tanzania kwa mwezi ni wa chini kiasi cha kwamba mshahara wake unazidiwa, tena kwa mbali, na mishahara wanayolipwa baadhi ya watendaji wakuu wa baadhi ya taasisi za umma nchini.

Aidha, ni jambo la kushangaza kwamba Gazeti la Mwananchi, linalochapishwa hapa nchini, linaweza kupata kiasi cha uongo anacholipwa Rais wa Tanzania katika mitandao ya nje badala ya kuuliza rasmi na kupewa majibu sahihi.

Kwa kujiingiza katika uzushi wa kupindua kiasi hiki, Gazeti la Mwananchi haliwezi kuwa na nia nyingine yoyote isipokuwa nia ya kuwachochea wananchi na kuwajengea chuki dhidi ya Serikali yao na Kiongozi wao Mkuu.

Ni matarajio yetu, kuwa Gazeti la Mwananchi litafanya jitihada za makusudi, kama taaluma ya uandishi wa habari inavyoelekeza, kutafuta usahihi wa jambo hili na kuwaambia Watanzania ukweli.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
27 Julai, 2015



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Kwanini imeshindwa kuweka wazi Raisi analipwa kiasi gani kwa mwezi

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 27, 2015

    Semeni. Basi kiiasi inashangza kwa hili mmejibu haraka sans. Toba
    Kuna shida ngapi za watanzania mbona ikulu hamjibu

    ReplyDelete
  3. Namkumbuka mwaka 2013, mtoto wa mkulima alituambia kwamba mshahara wake ni TSh milioni 7 kila mwezi; na kati na yeye na Makamo wa Rais na Rais - haizidi Miliono 1.. kwa hiyo nashangaa kusoma gazeti la kitaifa ikichapisha habari za kupotosha umma..

    Ila, ingekuwa vizuri pia.. in the spirit of full disclosure, ikulu nao wangetuambia mshahara halisi... hakuna kitu cha kuficha.. Kikwete ni mfano wa kuigwa tunapojadili mambo za Open Government!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 28, 2015

    sasa kama ni uongo si mseme huo mshahara? mnapofanya siri ndio mmaendekeza uvumi...kwa ninini siri?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 28, 2015

    Mwananchi amekopi tu kama vilivyokopi vyombo vingine vya habari chanzo halisi cha habari hii kipo ktk lugha ya kingereza.Kanusho zuri ni lile lenye kuonesha uhalisia wa kiwango anacholipwa ili kuwaweka sawa watu haitoshi hata kusema eti tangu uhuru marais wa Tanzania ni miongoni mwa wanaopkea mshahara wa chini kabisa huku kiwango kikifichwa....kuweni wakweli kama HONOROUBLE JOCE MUJICA PRESIDENT OF URUGUAY dunia nzima zinamjua mtu huyu kwa uthubutu wake.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 28, 2015

    Huyu aliyekanusha taarifa hizi mbona ametumia mipasho badala ya kutumia fact figure reflecting reality to clear the atmosphere?????? hahahahaha ni kama ametumia nadharia kujibu swali la vitendo au kwa lugha nyepesi yenye kueleweka na wengi ni kwamba amebwabwaja badala ya kuelezea

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 28, 2015

    ILI KUZIMA KABISA UWONGO MKUBWA WA GAZETI HILO, NINGESHAURI KWAMBA, SERIKALI IPIGE PICHA " SALARY SLIP" YA MH. RAIS NA KUONYESHA HAPA KWENYE TAARIFA HII AU BASI SERIKALI ITAJE " EXACTLY" KIASI GANI MH. RAIS ANAPOKEA.
    HAPO SERIKALI ITAKUWA IMEKATA KABISA SIO TU UWONGO HUU NA WONGO ZINGINE AMBAZO ZIMESEMWA WAKATI MWINGINE KUHUSU MH. RAIS.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 28, 2015

    Wajinga ndio watakaokubali kuwa raid analipwa mshahara mdogo kuliko watendaji wengine. Raid ndio anayepokea mahahara mkubwa kuliko MTU yeyote katika nchi take kwenye upande was serikali

    ReplyDelete
  9. Ben Toronto.July 28, 2015

    Michuzi kwa heshima na taadhima naomba niseme haya yafuatayo : Huenda hiyo habari iliyoandikwa na gazeti la mwananchi inaweza kuwa ya kweli au siyo ya kweli ila kitu cha msingi hapa ni hawa watu wa ikulu kutoa taarifa na kisha kushindwa kuulezea umma kile ambacho wao wanakisema ni cha kweli.
    Kama walikuwa wanapingana na taarifa ya gazeti la mwananchi kwanini wao wasiseme mshahara halisi wa Rais wa JM Tanzania? watoe vigezo vyote halisi ili kuthibitisha tuhuma zao dhidi ya gazeti la mwananchi.
    Au mshahara wa mtumishi wa umma, anayelipwa pesa na walipa kodi wa Tanznia ni siri ? !!
    Nashangaa sana hawa watu wa habari wa ikulu wanaota taarifa ndefu lakini isiyo na vielelezo vyovyote. Au hiyo makala ya gazeti la mwananchi ina ukweli ndani yake ? !!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 28, 2015

    Tatizo liko wapi? si mtoe hizo figa!! tuambieni raisi wetu mshahara wake ni kiasi gani kwa mwaka? in dollars and shs. Vitu kama hivi vinahitaji UWAZI. Mbona mishahara ya waalimu tunaijua!!!!
    Lowassa is paying a lot of money to be a president!!! haiwezekani kukawa na mshahara mdogo. KUWENI WAWAZI

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 28, 2015

    Kwa ufafanuzi tu, mshahara wa Rais wa Tanzania ni dola 190,000 tu, sio 192,000 kama African Review walivyozusha kwii kwiii kwiii.

    Kama Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais ilitaka Watanzania waambiwe ukweli kulikuwa na haja gani tena ya kulitaka gazeti la Mwananchi lianze kutafuta usahihi? Mambo mengine bwana...

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 28, 2015

    Twambie TUNAMLIPA shilingi ngapi? Badala ya kuweka mlolongo wa maneno, ingekuwa vyema ukasema "Mheshimiwa Raisi halipwi $192K kwa mwaka, ila nalipwa $XXXK kwa mwaka." Hii ingefunga majadiliano na malumbano.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 28, 2015

    Taja basi analipwa shs ngapi? Mbona nimesoma habari yote hakuna sehemu inasema Raisi wa Tanzania analipwa shs ngapi. Tupeni taarifa wananchi ili tusisome habari za uongo.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 28, 2015

    WATANZANIA WENZANGU, MSHAHARA NI SIRI YA MTU, HAWEZI MTU YEYOTE KUTANGAZA MSHAHARA WAKE HADHARANI HATA SIKU MOJA, ILI IWEJE? HALAFU MKISHAJUA ANALIPWA SHILINGI NGAPI IWASAIDIE NINI? VITU VINGINE HAVIPASWI KUJADILIWA MITANDAONI, NA HUYO ALIYETOA SIRI ZA SERIKALI MITANDAONI ANATAKIWA ACHUKULIWE HATUA ZA KINIDHAMU. MAANA NI KOSA KUBWA KUTOA SIRI ZA MTU MTANDAONI. AIDHA WAFANYAKAZI WA IKULU WAAPISHWE UPYA KAMA NI WAO NDO SOURCE OF INFORMATION. NARUDIA NDUGU ZANGU MTANIONA MPUUZI MSHAHARA NI SIRI YA MTU, SIRI KATI YA MWAJIRIWA NA MWAJIRI, RAIA MWINGINE HATAKIWI KUJUA MSHAHARA USIOMHUSU. .

    HALAFU MSIWE NA MASHAKA MISHAHARA YA SERIKALI SI MIKUUUBWA KIASI HICHO MNACHODHANIA. KUWENI NA AMANI WAPENDWA. TUJADILI MAMBO YA MSINGI SIYO MSHAHARA WA RAIS.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...