MAREHEMU RICHARD AZZA MGAYA
04. 04 , 1939 - 22. 05, 2015.
Familia ya Marehemu Mzee Richard Azza Mgaya inawaarifu ndugu, jamaa, marafiki na jirani kwamba shughuli ya kumaliza msiba itafanyika Jumapili hii ya tarehe 02 agosti, 2015 nyumbani kwa marehemu Njiro, Arusha.
Misa ya shukurani na sadaka itaanza saa tatu za asubuhi na baadaye chakula cha mchana.
Familia inatoa shukurani kwa wote walioshiriki kikamilifu katika shughuli za mazishi toka mwanzo hadi mwisho wa kumuweka kwenye nyumba yake ya milele. Familia inasema haina cha kuwalipa zaidi ya kusema AHSANTE SANA kwa yote na Mola awajaalie afya na uzima zaidi.
SISI TULIMPENDA, LAKINI BWANA ALIMPENDA ZAIDI.
HIVYO JINA LAKE BWANA NA LIHIMIDIWE - AMINA
Marehemu Mgaya atakumbukwa daima kama Mfanyabiashara maarufu aliyekuwa akimiliki duka pekee lilikokuwa linauza bidhaa zitokanazo na maliasili za wanyama pori kama vile pembe na ngozi pamoja na vinyago. Duka lake lilikua mtaa wa Samora wakati huo ukiitwa Independence Avenue na duka lake likiitwa National Trophy and Carvings Co Ltd.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...